Unataka kuagiza gari??... pitia hapa kwanza

Asante wachangiaji Wote Raha ipo hapa kwangu Niliagiza Gari 3 aina ya Mitsibishi Grandis Cheriot 2 za 99 iliobaki 98 ajabu zile za 99 nimelipa Mil3.2 kwa kila moja ila ya 98 niliandikiwa ktk accesmnt ya kulipa 2.6 Hivi hawa jamaa wanafuata vigezo gani? Sielewi

Kwa gari ya zaidi ya miaka 10, yenye cc 2400, na ambayo umilipia CIF 3.2M, unatakiwa kulipa kodi 3,030,400 . Naona kama walikupunguzia vile? Hiyo ya pili, ili ulipe ushuru 2.6M inabidi CIF iwe 2.8M. Mbona bado naona kama wamekupunguzia?

Wataalamu wa haya makokotozi wako wapi? Maana hizi ndio hard data tunazozihitaji kujua ukweli pale jikoni.

Naanza kuhisi saa nyingine hata makadirio hayo huwa yanasababisha watu kulipa kodi pungufu ya inayotakiwa.
 
Last edited:
Dullymo,nataka kununua toyota noah rangi yoyote.je nijiandae shilingi ngapi kakangu?
hlw sis!
unajua kwanza watu wengi wanachanganya kuna toyota NOAH na kuna toyota litehiace NOAH. but kwa upeo wa haraka haraka nishajua unayoitaka wewe. ukiitaka gari hiyo andaa milioni 5.5 mpaka 6.5 kutegemea na options kama vile alloy rims, cdplayers, body kits, spoilers nk. kama unahitaji let me know then nitakutumia picha na full quotation best. gud day
 
hlw sis!
Unajua kwanza watu wengi wanachanganya kuna toyota noah na kuna toyota litehiace noah. But kwa upeo wa haraka haraka nishajua unayoitaka wewe. Ukiitaka gari hiyo andaa milioni 5.5 mpaka 6.5 kutegemea na options kama vile alloy rims, cdplayers, body kits, spoilers nk. Kama unahitaji let me know then nitakutumia picha na full quotation best. Gud day

duh how comes jamaa mmoja alinunua kwa milioni 9? Watu wanapata faida kweli. Gari ya mili 6 wanauza mil 9? Huu si ufisadi
 
hlw sis!
unajua kwanza watu wengi wanachanganya kuna toyota NOAH na kuna toyota litehiace NOAH. but kwa upeo wa haraka haraka nishajua unayoitaka wewe. ukiitaka gari hiyo andaa milioni 5.5 mpaka 6.5 kutegemea na options kama vile alloy rims, cdplayers, body kits, spoilers nk. kama unahitaji let me know then nitakutumia picha na full quotation best. gud day

Mi so sis,,,,ila nipo interested na hii aina ya gari. Nitumie picha zake nione pia capacity ya engine na aina ya engine pia. Respect mkuu
 
Mi so sis,,,,ila nipo interested na hii aina ya gari. Nitumie picha zake nione pia capacity ya engine na aina ya engine pia. Respect mkuu
gari hiyo hapo. ni noah ya mwaka 2000. CC2000 na odo ni 92,000km
mpaka kuitoa na full registration pamoja na comm yangu ni 7ml
 

Attachments

  • 02.jpg
    02.jpg
    21.3 KB · Views: 164
gari hiyo hapo. ni noah ya mwaka 2000. CC2000 na odo ni 92,000km
mpaka kuitoa na full registration pamoja na comm yangu ni 7ml


mkuu Dullymo, nimekupm naomba details za bei za Rav4 kwenye showroom za bongo kwa sasa, ili nisitake risk ya kuagiza.
 
Splendid!!

Dully sina haja ya kuagiza nitakutumia wewe, nitakutafuta january, please naomba unitumie details contact zako kwenye PM, NIMETUMA ZANGU
 
Tatizo ni kwamba hao wanaofanya hiyo inspection wakati gari linashuka ndio hao wanaochomoa hivyo vitu na kuweka X kwenye kisanduku husika kwamba hicho kitu kwa mfano radio haimo. Ukweli ni kwamba inakuwepo lakini wakiishaonyesha kwamba haikuwemo basi wanapokwenda kuweka gari kwenye maegesho wanatoa vitu vyote walivyoonyesha kwamba havimo. Agent akienda kupewa gari anaona kabisa kwamba radio hamna na karatasi ya Bandari inaonyesha kwamba wakati wanapokea gari radio haikuwemo. Wakati huo meli imeisha ondoka ukimuuliza supplier anakwambia kila kitu kilikuwemo.

Nimeyakubali maelezo ya aliyepost hii habari kuhusu some companies huko .

Tiba

Ukweli ni kwamba document hii inabidi isainiwe na bandari pamoja na shipper. Sasa sidhani kuwa shipper anaweza kukubali kuwa kakabidhi gari haina radio wakati inayo. Mimi nilipewa hiyo inspection certificate yenye X kwenye radio/TV/DVD player na nilifuatilia kwa shipper hiyo radio (Gari ilikuwa CIF) mpaka akanitumia ingine ingawaje ilikuwa ya low quality.
 
Ukweli ni kwamba document hii inabidi isainiwe na bandari pamoja na shipper. Sasa sidhani kuwa shipper anaweza kukubali kuwa kakabidhi gari haina radio wakati inayo. Mimi nilipewa hiyo inspection certificate yenye X kwenye radio/TV/DVD player na nilifuatilia kwa shipper hiyo radio (Gari ilikuwa CIF) mpaka akanitumia ingine ingawaje ilikuwa ya low quality.

Umegusa kunako! Na hiyo inazidi kuonyesha kwamba kuna vitu tunadhani tunavijua kumbe la, halafu tunakaa tunalalama tu.

Maana nilikuwa nashangaa iweje mtu wa TRA tu ndiye asign kwamba hakuna radio? Hiyo ingekuwa bonge ya loophole ambalo sidhani kwamba lingeweza kuwepo kwa miaka yote hiyo ... maana watu wangekuwa wanaibiwa hovyo zaidi bila kuwa na la kufanya.

Tokea nimeanza kufuatilia hili swala ninazidi kupata picha kwamba tatizo pengine ni watu tu kutokujua taratibu hasa, na haki zao mpaka pale wanapokabidhiwa mzigo. Na jinisi ninavyoendelea kukusanya taarifa ndio nazidi kugundua kwamba baadhi ya watu ambao saa nyingine ndio tunaamini wanajua vizuri hizi taratibu na wanaweza kutusaidia, ndio hawana clue kabisa.

Maagenti wengi hawajui kabisa kodi inakalculatiwa vipi na TRA. Kwa hiyo kwao bado ni muujiza tu. Kufanya jaribio lingine, jana tukampigia dalali mmoja na kumuuliza HRV yangu ya mwaka 2002 ambayo iko njiani inakuja itakatwa kodi kiasi gani akasema 3M mpaka 4M. Nikimuuliza unaipataje, anasema ni kwa uzoefu wake. Kama angekuwa ana clue, pengine angeniuliza CIF ni kiasi gani. Kwa hiyo vitu vinaenda kwa makisio tu. Baadaye unakuta kodi tofauti unawalalmikia TRA badala ya kumuuliza dalali wako.

Siku zote nilikuwa nashangaa iweje vitu vinyofolewe kutoka kwenye gari bandarini halafu kusiwe na utaratibu wowote wa kulalamika na kuwa companseted. Kila "agent" ninayemuuliza analiongelea kama ni swala la kawaida tu, na kwamba ikitokea kubali tu imekula kwako. Kumbe zipo taratibu, na wapo watu wanaofuatilia na kupata haki yao.

Bado kuna maswali mengi tu, na bahati mbaya wale unaodhani ndio wanafahamu na wanaweza kukusaidia hawana ufahamu wa kutosha, na ningetamani sana wangefuatilia kwa undani maana wao ndio wanaoagiza magari mara kwa mara. Mimi naagiza mara moja tu kwa matumizi yangu.

Gari yangu inakuja. Ingawa kodi nikubwa, nitalipa kihalali kabisa.

Sasa ngoja ifike hapa halafu mtu achomoe kitu pale bandarini, au TRA wajifanye wana uplift. Nasema hapatakalika pale na patachimbika ... Kudadeki! Hiyo kesi hata kama itaisha miaka 50 ijayo. Nimehakikisha vielelezo vyangu vyote nnavitunza vizuri.

Eti mtu anaambiwa gari yako si ya bei hiyo halafu anakubali tu kwa sababu TRA wameenda kuangalia gari hiyo hiyo wakakuta bei ni tofauti. Haulizi hata wameangalia wapi huko ambako ndio reference ya bei za magari duniani. Yaana nitawapeleka mpaka mahakama kuu wakaonyeshe hiyo reference ya bei za magari duniani iko wapi. Kudadeki!

Sisi ndio tatizo saa nyingine. Watu vihiyo kabisa wanatengeneza mitandao michafu ya kutunyonya, na si tunakaa na kuafiki kama madunya hivi. Hatujui kwamba TRA wakilipishwa zaidi kwa vifaa vinavyopotea pale ndio hivyo wao watalipa hilo swala umuhimu, sio mpaka JK akawaambie.
 
Thanks Dullymo for this useful information especially for those interested in importing different vehicles. Keep it up!!!!
 
kaka fisadi, me nakuombea 2 gari lako lifike salama halafu ukauone mshike mshk wa tra na bandari kwa ujumla.maana bandari na tra ni bb m1 na mama m1.
 
Nataka kuagiza gari nimeshaingia mkataba na beforward co ltd ya Japan kuptia [URL="http://www.tradecarview.com"]www.tradecarview.com[/URL] Sasa nasubiri wadau mnipe taarifa Gari ya mwaka 1994 Suzuki Escudo Nomade je mpaka Bongo JAAI Inspection na Insurance USD 3800. Je nitalipia Ushuru kiasi gani maana mimi nimeipenda sana gari hii. Naombe msaaada wadau
 
kaka fisadi, me nakuombea 2 gari lako lifike salama halafu ukauone mshike mshk wa tra na bandari kwa ujumla.maana bandari na tra ni bb m1 na mama m1.



Nataka kuagiza gari nimeshaingia mkataba na beforward co ltd ya Japan kuptia[URL="http://www.tradecarview.com/"]www.tradecarview.com[/URL] Sasa nasubiri wadau mnipe taarifa Gari ya mwaka 1994 Suzuki Escudo Nomade je mpaka Bongo JAAI Inspection na Insurance USD 3800. Je nitalipia Ushuru kiasi gani maana mimi nimeipenda sana gari hii. Naombe msaaada wadau
 
Dully mjibu pastor hapo juu,

Na je bei ya escudo ina vary kutoka ngapi mpaka ngapi, iliyotengenezwa kuanzia 1998 mpaka 2005
 
dullymo,
ebu tusaidie kuhusu tradecarview maana hawa watu wanauza magari kwa bei poa sana na kuna makampuni mengi saana, sasa hayo ambayo wameyawekea lable kwamba ni ya kitapeli ni yapi???????????? Msaada kaka.

hii trade carview ndio haifai kabisa kwa sasa..nilikuwa japan mwaka jana..wa russia na wa nigeria wamejaa na wamefungua kampuni za kuuza magari..

Ila wanachofanya wanachukua picha za magari toka kwa watu au kampuni zingine kisha wanaweka kwenye website zao.

Na kama utauziwa gari tazama sana kilometer wanarudisha nyuma na pia mwaka wa gari wanarudisha nyuma hasa kwa gari za kimarekani.

Biashara za magari japan imekuwa cheusi chekundu siku izi..tunaita pata potea.

Alichoeleza jamaa hapo juu ni ukweli tupu.
 
Inaelekea wewe si mtaalam sasa katika ili CIF sio COST INCLUDING FREIGHT bali ni COST INSURANCE FREIGHT- umenipata nipo katika fani hii zaidi ya miaka 12.

Mkuu Mayolela,

Point of correction, CIF ni abbreviation ya Cost, Insurance and Freight na wala sio cost insurance freight. Hii ni kwa ufafanuzi kwa wale wasiojua.

Tiba
 
Back
Top Bottom