sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 3,679
- 9,839
Tukizungumzia vijana wanaoshikiliwa kwa uhaini wengi wanalifahamu jina la binti strong Niffer.
Lakini kuna huyu mwamba anaitwa Mika Chavala.
Sikuwa namfahamu ila nilim-google baada ya kuona jina lake kwenye media ya kimataifa akitajwa.
Nimekuta profile yake ni kijana hodari, jasiri, mbunifu, mpambanaji , mwelevu, mcha Mungu, anaipenda sana Africa na msomi.
Ana degree ya uchumi kutoka Seoul university.
Ni mjasiriamali.
True son of Africa.
Anaamini katika Africa moja na passport moja.
Hakukaa kimya alipoona nchi inakosa haki, alikemea dhulma bila kuficha ID yake.
Siku ya maandamano ya amani 29-10-2025 aliiomba serikali isimwage damu za raia.
Ukipata nafasi ingia kwenye DM yake Instagram umuandikie neno fupi la ku-appreciate commitment yake kuakikisha Tanzania inakuwa nchi nzuri ya kuishi. Siku akitoka atakutana na ujumbe wako.
History itamkumbuka Mika Chavala