*TUMSIFU YESU KRISTO*. Uongozi wa TMCS-DIT unasikitika kutangaza kuwa; Mwana-TMCS mwenzetu *EFRAIM MABENA* amefiwa na kaka yake mpendwa *EVANCE MABENA* usiku wa kuamkia jana jumanne.[emoji24][emoji24]
Taarifa zinasema kuwa EVANCE alikuwa akiishi South Africa tangu mwezi march 2017.
Kifo kilimkuta baada ya kunyang'anywa gari na pesa alizokuwa nazo kisha akapigwa risasi.[emoji24][emoji24]
Tunaombwa kumwombea mwenzetu katika kipindi hiki kigumu
Na pia tuiombee roho ya marehemu, Mwenyezi Mungu aipokee katika nuru ya uso wake.AMINA
Msiba upo nyumbani kwao *BUGURUNI-DAR ES SALAAM.*
_tutaendelea kutoa taarifa zaidi_
*Raha ya milele umpe Ee Bwana; na mwanga wa milele uwaangazie Marehemu wote wapumzike kwa Amani. AMINA*
kwa niaba ya uongozi wa TMCS-DIT
imetolewa na John Alex
_katibu_
Nimeinukuu taarifa hii kutoka kwenye group moja la wanafunzi DIT. Ndugu wamarehemu wameshapatikana shukrani kwa muanzisha uzi huu na kupelekea kupatikana kwa ndugu wa marehemu.