Unam-treat FAIRLY house girl wako?

Duh, hii ni nyanja nyingine ambayo ni pasua kichwa sana.

Ili umsaidie mtu, lazima na yeye ajitambue ndipo mtu mwingine waweza msaidia.

Unakuta mwingine hataki kabisa kujiendeleza na hayuko tayari, inakuwa ngumu sana kumsaidia.
Suala la kumwekea akiba ya uzeeni, kinadharia linawezekana ila kiuhalisia ni gumu. Mshahara wa wewe mwenyewe uliyemwajiri kukufikisha mwisho wa mwezi ni kwa mawazo, sasa utakumbuka NSSF ya msaidizi wa home? Achia mbali mshahara?
Kongosho,
Kwa sabau huduma nyingi anapata hapo hapo nyumbani si mbaya ukakata sehemu ya mshahara kila mwezi ambayo utamwekea akiba ili mkataba wake unapokatika awe na kiasi cha kufikia kwao. Ni vema kumfungulia akaunti ili kiasi hicho kiwe kinaingia benki moja kwa moja. Katika hili ni vema umshirikishe yeye japo unatakiwa kukaa na kadi yake ya benki ili ku-control matumizi yake.
 
Mimi wangu anakama miezi 3 au 4 hivi na anaishi kama famili member,tunampenda na yy anatupenda sana hata mtoto anayemlea kwa kweli anampenda sana km mdogo wake kwa vile tunamjari,kuhusu kumfungulia account nilipata wakati mgumu coz hana cheti cha kuzaliwa na kadi ya kupigia kura alikua hana but niko kwenye mchakato wa kumtafutia affidavit mahakamani ili niweze kumfungulia account,familia yao huwa wanakuja home na wanafuraha sana.
Nawashauri wenzangu wanaoishi na wadada wa kazi wawapende km wanavyowapenda watoto wao coz wanatusaidia sana
Ni vema kuwapenda na kuwathamini, japo vile vile ni muhimu kuangalia nyendo zao hasa kuhusu malezi ya familia yako, hasa katika muda ambao wazazi hampo nyumbani.
 
He mie nilishapitia dizaini nyingi tu, kuna mmoja alikuja kwangu siku ya kwanza iterview akaomba advance ili akatoe mimba yake ili afanye kazi vizuri, huyo sikumtendea haki kwani nilimtimua.
mwingine tuklikaa nae tangu hajui hata jinsi ya kushika kitasa cha mlango wa kawaida miaka6 tulielewana sana, namkumbuka milele alitoka kwangu na pikapu imejaa assets zake. Kwa ajili ya kumpa free kuzurura kila j2 alipata mchumba feki, akampa mimba na akamuambia awahi kwao ili aje ajitambulishe kumbe ilikuwa gia ya kumtoa mjini, masijini dada saa hizi ni wa kuonea huruma, tunampa misaada tunapoweza ila wanaume acheni kudanganya wasichana wa kazi!!! Sometimes hio kazi ndio the only chance ya kutokea. Kama huyo wangu alikuwa anasoma QT, anashona na alikuwa assets zote basic, wazazi wamantegemea, kauza vyote!
Very sorry to what happened to poor lady. Wapo wengi ambao huingia mjini hawajui kitu lakini baadaye wanadanganyika kwa namna tofauti kama ambavyo alidanganyika huyo.

Ni vema kuwaongoza wasaidizi wetu katika maisha ya kila siku ili wasije wakaangamia. Huo ni upendo pia. Japo ni vema kuwa makini katika namna ya kuwapa muongozo kwani wakati mwingine ni vigumu kutofautisha Upendo na Manyanyaso.
 
unadhani hawastahili malipo ya uzeeni? unaposema majibu yote hapana hapan ina maana humpi likizo wala mapumziko hg wako?

badili tabia,kawaida yangu mi ni mkweli wala sijifichi!ktk dunia hii unachokipata ndio thamani yako!most wa hg wanapatikana kienjeji na wanaendeshwa kienjeji!ndivyo ilivyo!kwa jinsi walivyo na wanavyopatikana wanachopata ndio stahiki yao!nakuambia hivyo sababu nimeshawahi kwenda kwa well off families!mpishi ni typical chef wa hotel,na package yao inafanana nao!they worth what they get!sasa hawa walioko majumbani mwa wabongo wengi do they worth mtoa mada anachotaka?watu na mavyeti yao hawapati maofisini mwao sembuse wao?huu ndio ukweli na watanzania hatujazoea kusikia ukweli!
 
kweli ma hg wengi hawatendewi haki hasa na wakna mama wenye umri mdogo,atleast kwa walioenda age au wanaume ndio wanaonekana kuwajali hao ma HG ila wanawake ni ugonjwa wa moyo kiukweli inabidi wabadilike kwani ukimtreat house girl wako vizuri utapungukiwa nini sanasana atakuwa anakupenda na kulea vizuri mtotot wako badilikeni nao pipa ni binaadmau aaaaaaaghhhhhhhhhhhhh
kama hawana umuhimu muwaache waondoke basi alafu muone kama utaweza kuiangallia nyumba peke yako
 
wengine hata uwasaidie na kuwapa vision nzuri za maisha hawakuelewi.ni wachache sana waelewa
 
Hivi na sisi wanaume hatuwanyatii kweli hawa mabinti pindi mama mwenye nyumba asipokuwapo nyumbani?
 
nakubaliana na wewe, mahsegl akili zao zimejaa *****. watu wengi wameshatendwa sana na hawa binadamu. yote kukosa elimu.
hata umpende vipi kudanganywa akaleta watu wakasomba vitu ni kawaida sana. kuna yule mama wa kihindi aliuwawa upanga, na hsegl akakomba magold yote na mapesa akakimbilia iringa alikotoka, lakini alikamatwa. kuna aliyeanza kazi mahali wakati ametoka kujifungua ila mtoto wake alikufa, akawa ananyonyeshga mtoto wa watu anayemlea kisa maziwa yanatoka na yanamuuma, mama mwenye mtoto si amfume siku ya siku akionyesha mtoto asiye wake. tukae nao tu vile tuna shida lakini usijipe matumaini eti ni mzuri.
akiamua kukutenda anakutenda kisawasawa maana akili yake ndogo. mwingine anasahau kazi zake anadhani kaja kuangalia TV, mwingine mchoyo, akiona mgeni anakuambia chakula bado, ili mradi wana vitimbi vya kila aina. Ukipata mzuri shukuru mungu ila usijisahau.




naandika kwa masikitiko sana...mahaucgel wachache sana wana akili za kiukwel lakin waliojaaa hata ukiwapenda vp ni kaz bure utamfanya km familia,utamweka usawa kwa wote wa familia, so beta vingne ukamchinjia njia panda tu...niwape mkasa mdogo tu.......ndugu yangu wa karibu kabisa imemkuta hii.alikuwa anampenda sana haucgel wake na tena ukuifika mgen hutajua km ni hausigel,na katika nyumba ile alikuwa na kaz ya kuangalia mtoto.baba na mama kazin,gafla wakashangaa yule mtoto alikuwa na miaka kama miwili na nusu hv,akawa na fangasi za mdomo haziishii hangaika na mtoto hakuna mabadiliko,siku ya siku yule mama alirud gafla home,akaingia ndan kaona kim,apite aelekee chumban kwake inabidi aupite mlango wa hausigeli,akasikia saut y mguno (kimahaba zaid)akasukuma mlango kwa nguvu akakuta mtoto ananyonya sehem za siri za HAUSIGELI....baada ya kumbana hausigel akasema alimfumdisha mtt kufamya hivyo..............so hawa watu aiseee hapana heri umlaze tu kwenye banda la kuku hata akijafanya upuuz utajiridhisha nawe aaaaah!
 
Sina housegirl, sijawahi kuwa na housegirl, na sitarajii wala kupanga kuja kuwa na housegirl kwa siku za usoni!
 
Sina housegirl, sijawahi kuwa na housegirl, na sitarajii wala kupanga kuja kuwa na housegirl kwa siku za usoni!

Really?! Never say never.. Utakuja kuoa and have kids. Mke yupo kazini na wewe busy pia. Watoto wataangaliwa na nani at home? au Day care?
 
alizaa,pale pale nyumbani yupo na mtoto wake.

alizalia kwako bado useme anatabia njema?
Lokissa Mkuu, kuzaa hakumaanishi kuwa na tabia chafu. Pengine tungejua kwanza mazingira yaliyomfanya afikie kuzaa.
Sio kila anayezaa anagawa kama njugu, kuna mazingira na sababu nyingi za kukutwa na huo mkasa. Majaribu ni mengi na mkasa na mikosi ni mingi. Kitu cha muhimu zaidi ni kujiuliza kwa mfano, kama mkasa kama huo umemfika mtoto wako wa kumzaa ungefanya nini, hata baada ya kutambua kuwa ni kutokana na tabia mbaya? Utamfukuza au utamsaidia kumtoa katika shimo?

Tendo la busara lilofanywa na familia ya Kisukari la "kukubali uhalisia", ndilo linalomfanya huyo binti kuwepo hapo miaka 10 sasa.

BTW, signature yako inabeba maana nzima ya hili tukio.
 
Dah, mimi bosi wangu ananitreat vizuri. Ananipa hadi muda wa kuperuzi jf. Mabosi wote wangekuwa kama wangu mahg tusingepata shida.
Jirekebisheni nyie mnaoitwa mabosi halafu mna manyanyaso.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom