Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Wakuu,
Imekuwa ni kawaida au tuseme fashion kwa wazazi/walezi kupost picha au video za watoto mtandani.
Picha au video hizo zinaweza kuwa za vichekesho, matukio mbalimbali ya maisha au mtoto anaambiwa afanye tukio fulani huku akirekodiwa na kisha kupostiwa mtandaoni au hata vitendo vya aibu ambavyo watu wazima huona kama vichesho/utani na kuweka mtandaoni kwa lengo la kufurahi tu kutokana na maudhui hayo.
Umeshawahi kufikiria mtoto wako atajihisi vipi akikutana na picha/video zake unazoweka mtandaoni, umeshawahi kujiuliza itaathiri vipi uhusiano wake na majirani, watu wa rika lake, kwenye ajira nk?
Mfano, umeweka video ya mtoto wako kafanya tukio analia, kamasi zinamtoka, au tukio lolote lile la aibu, mtoto huyu anakuja kuwa mkubwa yuko ofisi fulani siku ya siku ameteleza watu wanakuja kuibuka na picha yake akiwa kwenye hali hiyo na kutumia kumdhalilisha, hata ingekuwa wewe ungejisikia vizuri?
Huo ni mfano mdogo tu, lakini kuna watu wanarekodi watoto wao au kupiga picha ambazo hazifai, za aibu, zinazoweza kusababisha msongo wa mawazo kwa mtoto wako baadae na kwa hatua mbaya zaidi mtu anaweza hata kujiua ili tu kuondokana na kadhia ya kuchekwa, kudharauliwa, kutukanwa kutokana na ulichopost mtandaoni akiwa mdogo.
Wewe unatakiwa kuwa wa kwanza kumlinda mtoto ambae hawezi kujitetea na sio kumdhalilisha.
Imekuwa ni kawaida au tuseme fashion kwa wazazi/walezi kupost picha au video za watoto mtandani.
Picha au video hizo zinaweza kuwa za vichekesho, matukio mbalimbali ya maisha au mtoto anaambiwa afanye tukio fulani huku akirekodiwa na kisha kupostiwa mtandaoni au hata vitendo vya aibu ambavyo watu wazima huona kama vichesho/utani na kuweka mtandaoni kwa lengo la kufurahi tu kutokana na maudhui hayo.
Umeshawahi kufikiria mtoto wako atajihisi vipi akikutana na picha/video zake unazoweka mtandaoni, umeshawahi kujiuliza itaathiri vipi uhusiano wake na majirani, watu wa rika lake, kwenye ajira nk?
Mfano, umeweka video ya mtoto wako kafanya tukio analia, kamasi zinamtoka, au tukio lolote lile la aibu, mtoto huyu anakuja kuwa mkubwa yuko ofisi fulani siku ya siku ameteleza watu wanakuja kuibuka na picha yake akiwa kwenye hali hiyo na kutumia kumdhalilisha, hata ingekuwa wewe ungejisikia vizuri?
Huo ni mfano mdogo tu, lakini kuna watu wanarekodi watoto wao au kupiga picha ambazo hazifai, za aibu, zinazoweza kusababisha msongo wa mawazo kwa mtoto wako baadae na kwa hatua mbaya zaidi mtu anaweza hata kujiua ili tu kuondokana na kadhia ya kuchekwa, kudharauliwa, kutukanwa kutokana na ulichopost mtandaoni akiwa mdogo.
Wewe unatakiwa kuwa wa kwanza kumlinda mtoto ambae hawezi kujitetea na sio kumdhalilisha.