Mzazi/ mlezi kabla hujaweka picha, video ya mtoto mtandaoni jiulize kama ataifurahia akikua

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,116
Ni kama fashion sasa hivi watu kuwarekodi watoto kwa video fupi au kuwapiga picha wakiwa katika harakati zao za maisha ya kitoto.

Kwa kuwa mtandao imekuwa mbadala wa albam kwenye kutunza kumbukumbu ni jambo jema kutunza kumbukumbu za makuzi ya mtoto iwapo unaona ni lazima ukatunze mitandaoni kwani bado zipo njia nyingine za kutunza bila kuwapost mitandaoni.

Ila naona hali inazidi kuwa mbaya sana kwa wazazi na walezi kutafuta watoto wao kutrend kwa kuwarekodi video mbaya ambazo natumai hazina wema kwa dunia inakokwenda kwa kuwa mtandao hausahau zitamrudia hata atakapokuwa mkubwa.

Wapo wazazi wanawapa script watoto wameze ili warekodiwe, wakati mwingine ukipima maudhui anayotoa mtoto na umri wake unaona kabisa mtoto anafanyishwa jambo ambalo linamkuza kiumri sana hakuoaswa kutamka au kufanya kitendo hicho katika umri huo, mfano wapo wanaowachezesha nyimbo zinazoimba mapenzi, ivyo huwaweka jinsia mbili tofauti na kuwafundisha kukumbatiqnq kushikana kukiss nk.

Lakini wapo wanaowaacha watoto wapande, waingie sehemu ambazo unaoana kabisa zilikuwa hatarishi kwa watoto ili tu wapate video za kuweka mitandaoni, ipo siku litawakuta jambo na hamtapata wa kumlilia.

Unakuta katoto kadogo kanaimba nyimbo ambazo hata mtu mzima napata ukakasi kuimba mbele ya watu mbaya zaidi kanaima kqnakata viuno na kulala chini kanabinua kalio na mzazi anarekodi na kushangilia wakati mwingine anamsisitiza akate zaidi, jamani mnawapeleka wapi watoto? Mnaanda jamii ya aina gani?

Kabla hujaweka maudhui yoyote yanayomuhusu mtoto, jiulize.
  • Je, mtoto akikua atafurahia kuona alifanya/ au kufanyishwa kitendo hicho?
  • Je, haitaharibu mtazamo wa watoto wenzake watakaoona video hiyo na kumuona hana maadili?
  • Je, Video hiyo ikibaki mtandaoni haitatoa picha ya malezi au makuzi mabovu na kusababisha akaja kukosa fursa fulani ukubwani, maana kuna nyadhfa wanaangaoia hata malezi ya familia aliyokulia wanaotaka kumwajiri.
  • Je, hautakuja kumtengenezea mtoto chanzo cha kupata dhihaka kutoka kwa jamii yake ya baadae?
Ni vyema kumlinda mtoto kwa kutokumfanyia kitu ambacho pengine akikua atabaki anakijutia.

Screenshot_20230312-073610_Instagram.jpg

Mtoto akiyamwaga mauno na watu wazima wanamshangilia😭

Screenshot_20230311-221557_Instagram.jpg

Mtu anawaza kupiga picha bila kuangalia huenda ataumizwa na mashine ya kufulia anayoingia.
 
Kuna mtu alipost video akimuogesha mtoto wake, nilimsihi aitoe. Wamatumbi wa Tandahimba wamepata smartphone imekua tatizo.
 
Ni kama fashion sasa hivi watu kuwarekodi watoto kwa video fupi au kuwapiga picha wakiwa katika harakati zao za maisha ya kitoto.

mkubwa.

Wapo wazazi wanawapa script watoto akate zaidi, jamani mnawapeleka wapi watoto? Mnaanda jamii ya aina gani?
Mungu akubariki kwa kuliona hili mkuu, mimi nahitimisha kwa kusema; Wazazi wengi hawana akili.. japo sio wote
 
Niliachana na kimada ambaye alinipatia mtoto wa kike kwa upumbavu huu wa kuweka clip ya mtoto wa kike wa 4 years old akicheza "kwangaru" huko "instagrammu".
Na mpaka leo, anamuona mtoto mara moja kwa mwezi sababu niliwahusisha Ustawi wa Jamii.
Safi kabisa
 
Kuna mtu alipost video akimuogesha mtoto wake, nilimsihi aitoe. Wamatumbi wa Tandahimba wamepata smartphone imekua tatizo.
Japo hili sio kwa "Wamatumbi" tu. Mitandao ya kijamii imetengeneza uraibu mbaya sana wa watu kutaka sifa za watu. Na miongoni mwa waathirika wakubwa ni watoto wadogo.

Kuna mdada Mmarekani mweusi alirekodi video yuko na mwanae mchanga wa kiume anasema "katika maisha yangu nilikuwa naogopa sana kuwa na mtoto "ugly", sasa oneni nilichokipata, oneni sasa" halafu anamuonesha mtoto wake. Aliirekodi Facebook. Unasikitisha sana ule udhalilishaji. Ila watu walimshambulia sana huyo dada.

Kuna mwengine mpaka watu walianzisha kampeni Tiktok imfungie sababu waliogopa mwanae alikuwa anadhalilika kingono. Alikuwa anamrekodi mpaka wakati mwenigne anavishwa vinguo vya kuogelea. Ikagundulika video ambazo anamuweka wazi kimavazi mtoto huyo wa kike zilikuwa saved sana kuliko kawaida. Watu wakamkalia kooni mpaka ile vuguvugu ya kutaka awe banned ikawa maarufu.

Hivyo haya mambo sio Bongo tu.
 
Japo hili sio kwa "Wamatumbi" tu. Mitandao ya kijamii imetengeneza uraibu mbaya sana wa watu kutaka sifa za watu. Na miongoni mwa waathirika wakubwa ni watoto wadogo.
Ni hatari sana. Inabidi watu wajue athari wa wanachofanya la sivyo watoto wakija kukua watakuja kuwalaumu sana wazazi au walezi wao, na wengine kuathirika kisaikolojia kabisa.
 
Hakika umesema vema sana, huko maofisini wanawake wakirudi likizo ya kunyonyesha ndo utachoka kwa zile developement stages za watoto, unakuta mzazi yuko veeeeery proud mwanae wa 1 or 2yrs anacheza sijui kama Diamond au anaimba vitu vya hovyo na hapo staff wanakazi ya kupongezana bili.kujua huyo mtoto wanamharibu.

Nakumbuka kipindi cha Magufuli kuna yule mtoto alitrend sijui anajua kutaja majina ya mawaziri wa Tanzania na watu wakaona kama kitu cha ajabu bila kusahau mtoto hua kulingana na what you feed in his brain.

Mbaya zaidi sisi wazazi wa kipindi hiki hatuna kizuri tunachofeed kwa watoto wetu zaidi ya upuuzi na ukikuta mzazi anamkazania mwanae ajue mambo ya mola wake watu wanakuona umepoteza ramani kabisa. Mungu atuongoze ktk malezi hasa sisi wanawake ambao ndio tunapaswa kua walimu wa kwanza kwa watoto
 
Ni hatari sana. Inabidi watu wajue athari wa wanachofanya la sivyo watoto wakija kukua watakuja kuwalaumu sana wazazi au walezi wao, na wengine kuathirika kisaikolojia kabisa.
Inasikitisha.

Watoto inapaswa walindwe.
 
Back
Top Bottom