GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Mwanamke! Kiumbe wa kipekee ambaye wanaume wengi hawajamfahamu kiusahihi!
Mwanamke, kiumbe "dhaifu" lakini mwenye nguvu ajabu!
Mwanamke ni kiwanda kinachoishi!
Mpe mchele, atakurudishia ukiwa umegeuzwa na kupewa jina jingine, wali!
Mhuzunishe, naye atakufanya "ulie" bila kupigwa!
Mwanamke! Mpe tabasamu...
Sitaki kukuambia athari ya tabasamu lako kwa mke wako, kama hujui! Itapendeza ukigundua mwenyewe. Na ukigundua, utaendelea kugundua na zaidi, na zaidi!! Ugunduzi mmoja utakupeleka kwenye ugunduzi mwingine. Itakuwa ni furaha baada ya Furaha!!!
Nakushauri kitu gani? Kugundua athari ya tabasamu lako kwa mke wako? Kwa jinsi gani? Fuata maelekezo hapa chini.
Kwa siku thelathini mfululizo, hakikisha Unafanya haya kila siku:
1. Kila umwonapo, tabasamu bila kujali kama anakuona au hakuoni
2. Uamkapo Asubuhi na hata urejeapo Jioni toka "kazini", n.k., msalimie kwa tabasamu!
3. Umalizapo kula chakula alichokupikia au kukutengea, mshukuru kwa maneno yanayosindikizwa na tabasamu!
4. Akiwa anapika, fanya kupita jikoni umwongeleshe neno lo lote zuri, likisindikizwa na tabasamu.
Na ukiona, labda umekaa sebuleni na yeye yupo, labda jikoni, halafu ukaona kama anapita uliko mara kwa mara, inawezekana akawa anahitaji umwongezee "dozi", tabasamu. Ukiweza, umfuate huko huko aliko ukapige naye stori kwa muda, au "full time", lakini hakikisha stori zinasindikizwa na tabasamu!
Fanya hivyo, na kabla ya mwezi kuisha, utaanza kugundua ambayo hukuwa ukiyafahamu kuhusu mwanamke. Hata kama ulidanganywa "jandoni" kuhusu mwanamke, ugunduzi wako utakuwa mwanzo wa kuanza kuujua ukweli halisi, wa "nguvu" ya mwanamke.
Katika kipindi hicho cha zoezi la kutabasamu, epuka kumwongelesha maneno ya kumvunja moyo au kumhuzunisha! Usimkosoe, na ikibidi kukosoa, ufanye hivyo kwa hekima na upendo mkubwa sana.
Ukiweza, uwe na diary ya kuandika kila siku kuhusu mke wako. Kila siku, uhakikishe unaandika jambo lo lote zuri linalomhusu, iwe ni sura yake, tabia yake, matendo yake, cho chote kile.
Kwa maneno mengine, uwe unayawinda mazuri yake kwa ajili ya kuripoti kitabuni, kwenye diary yako maalum kuhusu mke wako.
Fanya hivyo, na ndani ya mwezi mmoja unaweza ukagundua ugunduzi mzuri kumhusu mke wako, na mwanamke kwa ujumla, ugunduzi utakaokuacha kinywa wazi kwa furaha!
Unaweza kufanya hivyo?
Ni zoezi la siku thelathini tu lakini linaweza kukuletea manufaa makubwa sana!
Mwanamke, kiumbe "dhaifu" lakini mwenye nguvu ajabu!
Mwanamke ni kiwanda kinachoishi!
Mpe mchele, atakurudishia ukiwa umegeuzwa na kupewa jina jingine, wali!
Mhuzunishe, naye atakufanya "ulie" bila kupigwa!
Mwanamke! Mpe tabasamu...
Sitaki kukuambia athari ya tabasamu lako kwa mke wako, kama hujui! Itapendeza ukigundua mwenyewe. Na ukigundua, utaendelea kugundua na zaidi, na zaidi!! Ugunduzi mmoja utakupeleka kwenye ugunduzi mwingine. Itakuwa ni furaha baada ya Furaha!!!
Nakushauri kitu gani? Kugundua athari ya tabasamu lako kwa mke wako? Kwa jinsi gani? Fuata maelekezo hapa chini.
Kwa siku thelathini mfululizo, hakikisha Unafanya haya kila siku:
1. Kila umwonapo, tabasamu bila kujali kama anakuona au hakuoni
2. Uamkapo Asubuhi na hata urejeapo Jioni toka "kazini", n.k., msalimie kwa tabasamu!
3. Umalizapo kula chakula alichokupikia au kukutengea, mshukuru kwa maneno yanayosindikizwa na tabasamu!
4. Akiwa anapika, fanya kupita jikoni umwongeleshe neno lo lote zuri, likisindikizwa na tabasamu.
Na ukiona, labda umekaa sebuleni na yeye yupo, labda jikoni, halafu ukaona kama anapita uliko mara kwa mara, inawezekana akawa anahitaji umwongezee "dozi", tabasamu. Ukiweza, umfuate huko huko aliko ukapige naye stori kwa muda, au "full time", lakini hakikisha stori zinasindikizwa na tabasamu!
Fanya hivyo, na kabla ya mwezi kuisha, utaanza kugundua ambayo hukuwa ukiyafahamu kuhusu mwanamke. Hata kama ulidanganywa "jandoni" kuhusu mwanamke, ugunduzi wako utakuwa mwanzo wa kuanza kuujua ukweli halisi, wa "nguvu" ya mwanamke.
Katika kipindi hicho cha zoezi la kutabasamu, epuka kumwongelesha maneno ya kumvunja moyo au kumhuzunisha! Usimkosoe, na ikibidi kukosoa, ufanye hivyo kwa hekima na upendo mkubwa sana.
Ukiweza, uwe na diary ya kuandika kila siku kuhusu mke wako. Kila siku, uhakikishe unaandika jambo lo lote zuri linalomhusu, iwe ni sura yake, tabia yake, matendo yake, cho chote kile.
Kwa maneno mengine, uwe unayawinda mazuri yake kwa ajili ya kuripoti kitabuni, kwenye diary yako maalum kuhusu mke wako.
Fanya hivyo, na ndani ya mwezi mmoja unaweza ukagundua ugunduzi mzuri kumhusu mke wako, na mwanamke kwa ujumla, ugunduzi utakaokuacha kinywa wazi kwa furaha!
Unaweza kufanya hivyo?
Ni zoezi la siku thelathini tu lakini linaweza kukuletea manufaa makubwa sana!