ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
- Thread starter
-
- #61
Utafanyaje uspy pasipo regulations? Lazima ziwepo regulations za kumbana spy ili asimchochee anayemspy kufanya makosa ambayo kimsingi mpelelezwa hakua na dhamira ya kuyafanya. It was a dirt mission.
Limefungwa huko kwenye saccoss yenu huku mitandaoni na mitaani ndio habari ya mjini. Cc Matola. Hizo rasilimali kajadili na mkeo.
ZeMarcopolo is a natural calamity
Lema is a natural disaster...
By Balali
Kwanza geuka nyuma angalia chama chako ccm na madhila kwa raia wasio na makosa
Tuambie nini kilitokea baada ya Ramadhani Ighondu kumjeruhi Dakitari bwana Ulimboka
1. Ramadhani yuko wapi na Bwana Pinda na Nchimbi walisema nini kuhusu usalama wa Taifa nanini kilitokea
2. Gazeti la mwanahalisi likowapi baada ya kuchapisha mtiririko mzima wa madhambi ya Rama Ighondu kwa ulimboka?
3. Nini maana ya neno upelelezi kwa chama au Taifa............
i) kuathiri chama kwa kukiendeleza (+ve impact)
ii) kuathiri chama kwa kukiangamiza (-ve impact)
Ukinijibu haya tutaendelea kujadili hoja yako
Muulize Anna makinda kwanini amekalia ushahidi wa jinsi Pinda alivolidanganya Bunge na watanzania kwa ujumla wake
kuhusiana na mauwaji ya watanzania wasio na hatia Mjini Arusha?
!
!
kiuamnifu kabisa nimechoka kusikia habari za chadema jamani, khaaaaaaaaaaaaa kila thread chademaaa chadema chademaaa chadema loh aaaaah inatosha jamani
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai...
By Balali
Kwanza geuka nyuma angalia chama chako ccm na madhila kwa raia wasio na makosa
Tuambie nini kilitokea baada ya Ramadhani Ighondu kumjeruhi Dakitari bwana Ulimboka
1. Ramadhani yuko wapi na Bwana Pinda na Nchimbi walisema nini kuhusu usalama wa Taifa nanini kilitokea
2. Gazeti la mwanahalisi likowapi baada ya kuchapisha mtiririko mzima wa madhambi ya Rama Ighondu kwa ulimboka?
3. Nini maana ya neno upelelezi kwa chama au Taifa............
i) kuathiri chama kwa kukiendeleza (+ve impact)
ii) kuathiri chama kwa kukiangamiza (-ve impact)
Ukinijibu haya tutaendelea kujadili hoja yako
"Mida Eight anatumiwa na Dr. Slaa kugombanisha viongozi" - waraka
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai...
Hakika. Nikikumbuka Lema alienda UK akapiga picha na helcopter na kuwadanganya misukule kuwa ameinunua kwa ajili ya M4C. ni miaka miwili imepita lakini mpaka kesho hakuna cha chopa wa nini.
Vijana wa chadema wanatumika kama Kondom,hususan wa kanda yao ndio kabsaaaaa!!!! hata ukuadi wanakubali hata kama ana elimu Chuo,mfano Mrombo Ben saa 8.
Huyo ni mlaghaika. Baada ya ID yake ya Jason Bourne kugundulika ameona aje na hii ya Asha Mohamed wa Doha!
Huyu ni mtu wa ajabu anayestahili kuonewa huruma...
Dr Slaa amesema suala la zitto na CDM limefugwa sasa tuongelee suala la rasilimali zetu kama gesi, Umeme kupanda, hali mbaya ya maisha na wizi wa mali , wabakaji kama yle mbunge wa huko Tabora. kwahiyo tusubiri siku 14 tusikilizie maamuzi magumu ya CC
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai.
Miezi kadhaa iliyopita jumuiya ya vijana ya Chadema, Bavicha, ilitangaza kumvua uongozi na kumfukuza uanachama aliyekuwa makamu mwenyekiti wa jumuiya hiyo Bi. Juliana Shonza. Kosa lake lilitangazwa kuwa ni "usaliti".
Aliyefichua "usaliti" huo ni Ben Saanane a.k.a Mida Eight ambaye alielezwa kuwa alipewa kazi maalum ya kuspy vijana wenzake.
Katika katiba na kanuni za chama HAKUNA kazi hii ya uspy aliyopewa Ben Saanane.
Vijana wengi wa bavicha hasa hapa JF walimpongeza Ben Saanane na kumuona shujaa. Mpaka leo uspy huo alioufanya Ben Saanane ndio jambo pekee linalomfanya aonekane insider wa Chadema.
Mkakati wa siri wa kumpa Ben Saanane kazi ya kuspy ndani ya chama haukuhusisha vikao halali vya chama. Ndio maana viongozi wakuu wa Chama na wajumbe wa Kamati Kuu hawakuwa na taarifa yoyote juu ya kazi hii ya Ben Saanane. Hii ilikuwa ni kazi binafsi ya Dr. Slaa. Ben Saanane alikiri kwenye kikao halali cha Bavicha kuwa alifanya kazi ya uspy na kikao hicho kikampongeza kwa kazi nzuri!
Ni UNAFIKI wa hali ya juu kuona vijana waliounga mkono uwepo wa mikakati ya siri ya Dr. Slaa kumtumia Ben Saanane wakipinga mwanazuoni Dr. Kitila Mkumbo kuwa na mikakati ya siri.
Je, kuna mtu mwenye hati miliki ya mikakati ya siri ndani ya Chadema?
Jumuiya ya vijana katika chama chochote ndio nguzo na dira ya chama. Unafiki huu unaotawala Bavicha unadhihirisha kuwa Chadema sasa haina dira na nguyo yake imeliwa na mchwa.
ZeMarcopolo and WanajaJF,
Mosi,Hakuna mahali popote iwe kwenye vikao au mahali pengine nilipowahi kutamka haya yaliyoandikwa hapa.Labda mleta mada alete ushahidi hapa
Pili,Tamko langu kuhusu PM-7 lipo huku.
Tatu,Kama nilipongezwa kwa kiwango anachodai mleta mada hapa sasa iweje nipewe adhabu ya kusimamishwa kugombea nafasi yoyote kwa muda wa mwaka 1 sambamba na onyo kali
Nashukuru Mungu uchaguzi haukufanyika mwaka huu kama ilivyopangwa maana ningekosa haki ya kuchaguliwa.Mipango ya Mungu si kama mipango yetu wanadamu
Nne,Naomba niweke hili very clear.Sijawahi kuwa au kutumiwa na Dr.Slaa au kiongozi yeyote wa CHADEMA kwa maslahi binafsi.
Hizi ni hoja mufilisi na visingizio vya washirika wangu wa Zamani katika mkakati haramu waliokasirishwa na kitendo changu cha kusimamia maslahi ya chama na kuwaanika hadharani baada ya mimi binafsi kufanya kazi kubwa ya kuwasihi waache mpango huo maana wangekivuruga chama
Kwa muda wa takribani siku 345 hadi leo hii wamekua wakinishambulia na kunitukana lakini mwisho wa siku walikiri kupanga njama chafu.Ukweli siku zote husimama juu ya unafiki,usaliti na njama ovu za kuuficha ukweli.Kilichotokea Alhamisi iliyopita ni Matokeo ya jitihada za ukweli uliofanikiwa kulipa kisasi baada ya kupuuzwa kwa muda mrefu
Tano,WANACHADEMA,Wapendamabadiliko na watanzania kwa ujumla nawaahidi kuendeleza mapambano na wale wote wanaozuia harakati za mabadiliko ndani na nje ya chama chetu
Nitaendelea kusimamia misingi ya chama chetu na taifa bila kuchoka hadi tone langu la mwisho la damu.Namuomba mwenyezi Mungu anipe nguvu na ujasiri katika mapambano haya.Tuwapuuze wale wote wanaojaribu kututoa katika mstari wa mapambano.
Katika harakati hizi za mabadiliko na malengo ya CHADEMA kitaasisi katika kuongoza vuguvugu hili Doctrine yangu ni 'It's either you are with us or against us'.Hakuna middleground hata kama dunia ni three dimension.Kipimo nitakachompimia msaliti yeyote wa mabadiliko haya ndani ya chama hakitakua na tofauti na kile nitakachotumia dhidi ya wapinzani na maadui wa mabadiliko nje ya chama.
CC: Invisible, Fang, Buchanan, Paw, PainKiller Moderator