Unafahamu nguvu ya Wazo?

Apollo mkuu unaweza vipi kukaa bila kuwaza....nataman kujua namna ya kufungua mind,je unaweza tumia third eye kuangalia ndani ya subconscious,


#Limit is ur imagination.

I can see you soul inavyopenda kuwa huru. Ni swali zuri sana mkuu.

Ili kuweza kujua jinsi ya kukaa bila wazo, ni vyema kwanza kufahamu "wazo" ni nini na "akili" ni nini. Ili kutambua kipi kinatoka wapi na kinakua vipi.

Akili (mind) ni kisima cha mawazo ambacho mawazo hutokea. Unaweza ukatuliza kisima hicho kitulia mpaka maji yake yakawa kioo kwa mazingira yanayozunguka. Sawa na mto ulio na maji yaliyotulia mpaka unaweza kuitazama na kujiona utazamapo maji yake.

Unaweza kukaa bila mawazo kwa kufocus katika kitu kimoja. Mfano meditation inamfanya mtu asiwaze bali atazame mawazo. Unakuwa unayatazama mawazo yanavyotoka akilini.

Wazo sio kitu chochote, wazo likiwa kichwani usipolipa kipaumbele lenyewe linapotea kwa kukosa nguvu. Hivyo badala ya kuwa mtumwa wa thoughts unakuwa mfalme wake, unakuwa unaweza kuamua kulipa wazo nguvu kwa kulifuatilia au kwa kuliacha. Pia unaweza kufanya Yoga, Mantra Chants, Music (hasa classic musics au melodies zilizotulia).

Kukaa bila thoughts ni taabu sana mwanzoni. Ni sawa na kuacha tabia ambayo umeizoea tangu ulipozaliwa.

mfano elimu dunia inasema kitu halisi ni kile unachokiona,kukishika,kukinusa au kutumia ile milango ya faham,unaweza vipi kutoa kitoa kitu kwenye imarginary world to real world.


Milango ya ufahamu inakusaidia kuingiza informations katika akili. Akili imegawanyika katika pande kuu hasa 2. Akili ya Conscious na Sub conscious. Milango ya ufahamu ni milango ya information kwenye akili ya Conscious Mind na sio Subconscious mind. Akili ya sub conscious haijui logics, haifahamu nyakati wala haifahamu sayansi na facts zinasemaje, whatever unachoimagine na kuamini nayo inaamini. Ndio akili ya VISUALIZATION, Na ndio akili ambayo artists wengi, painters, poetry masters, n.k wameweza kuitumia kwa kuvisualize kazi zao na kuweza kukufanya ukapenda kazi yake kupitia creativity yake ya subconscious. Mfano mchoraji, ili achore creativity yake lazima aiweke katika Subconscious mind na hapo inajitokeza katika physical world.

Hauwezi kuiacha the present world moja kwa moja, labda mpaka ukishauacha mwili wako baada ya kifo cha mwili. Lakini unaweza kuishi katika dunia zote (Ya sasa na dunia ya imagination/visualization).
 
Labda niseme kauli hii kwa umakini na aliye na macho aweze kufunguka:

MAISHA SIO KINACHOTOKEA NJE YAKO BALI MAISHA UNAVYOYAONA NA KUYA-EXPERIENCE NI MATOKEO YA KITU FULANI KILICHOKO NDANI YAKO. UKIWEZA KUBADILI CHA NDANI YAKO BASI HATA MAISHA YA NJE UTAYABADILI KIKAMILIFU.

Mfalme suleiman aliwahi kusema kuwa, moja kati ya kitu alichojifunza katika maisha yake ni kuwa,
As the man thinketh in his heart so is he.
 
naendelea kufuatilia hii kitu muhimu sana ingawa wengi wetu hatuzingatii vitu kama hivi ndio maana wale wachache waliojua umuhimu na maana yake ndio wanaotuendesha na wengine tunafuata kama mkumbo eg,..kina mwingira,lusekelo,tb joshua na wengine wa aina yake.
 
naendelea kufuatilia hii kitu muhimu sana ingawa wengi wetu hatuzingatii vitu kama hivi ndio maana wale wachache waliojua umuhimu na maana yake ndio wanaotuendesha na wengine tunafuata kama mkumbo eg,..kina mwingira,lusekelo,tb joshua na wengine wa aina yake.

kweli kabisa na Gwajima pia!
 
Apollo pole na shughuli za siku,kwenye soma soma yangu ya kuweka mind free kuna sehem niliona kuwa mawazo ni takataka ya kufungua subconscious,nielezee namna ya kufungua na kuweka wazo au taka nzuri na kuacha taka chafu.
kuhus third eye na subconscious na mtu within au mtu wa ndani au nafsi je viko connected au kila kitu kina kaz tofauti??..samahani kama niko nje mada ila napenda kufaham zaid uwezo mind with all
 
Last edited by a moderator:
Mi somo nimelipenda ila mujue jambo hili kwa wacha Mungu sie tunaita utulivu hapo ndipo utatambua aina ya mawazo. 1.wazo la Mungu ni la utulivu na huambatana na neno la Mungu. 2.wazo la shetani huwa la haraka hujirudia rudia na huwa lina pingana na neno la Mungu. 3.wazo lako huwa ni lile linalotaka matakwa yako. Mfano huwa hivi 1. Wewe kwa nini kanikosea? Kanionaje 2. Shetani huyu amekuzoe. Amekudharau ili kumkomesha lazima umfanyie akukome.3. Kumbuka nawe unakosea wengine hapo huambatana na vifungu ila mara shetani tena huja kwa maneno ya kupunga. Somo hili ni zuri linaitwa somo la moyon. ila unakini ni muhimu bila hivo utaambulia kuwa mchawi huko huko au kichaa kama huwezi kupambanua sautia na kutulia na maanisha kutuliza mawazo usijaribu. labda kama unataka utulie ili uwaze mambo ya dunia ila usitumie muda mrefu na kuhamisha mawazo mbali wachawi watakuchukua hayo tu
 
nimeipenda hii mada, katika pitapita yangu niliwahi kutana na documentary moja imeandikwa bob prata ambayo aliita thoughts are things, yani kila kitu tukionacho duniani ni zao la fikra na pia alisema kua fikra zimegawanyika katika makundi mawili yani positive thoughts and negative thoughts ingawa binadam wengi wamejawa na negative thoughts thats why wanafeli ktk maisha na mipango yao, positive thoughts zinalazimishwa while negative zinakuja zenyewe so we are the products of what we think
big up kwa mleta mada
 
naendelea kufuatilia hii kitu muhimu sana ingawa wengi wetu hatuzingatii vitu kama hivi ndio maana wale wachache waliojua umuhimu na maana yake ndio wanaotuendesha na wengine tunafuata kama mkumbo eg,..kina mwingira,lusekelo,tb joshua na wengine wa aina yake.

Asante sana kwa kuamka. Very true.
 
Apollo pole na shughuli za siku,kwenye soma soma yangu ya kuweka mind free kuna sehem niliona kuwa mawazo ni takataka ya kufungua subconscious,nielezee namna ya kufungua na kuweka wazo au taka nzuri na kuacha taka chafu.
kuhus third eye na subconscious na mtu within au mtu wa ndani au nafsi je viko connected au kila kitu kina kaz tofauti??..samahani kama niko nje mada ila napenda kufaham zaid uwezo mind with all

Asante sana Neo. Nitajaribu kukujibu vyema.

Kwa lugha rahisi wengi husema kuwa mawazo ni kama vile bubbles zinazotoka kwenye kisima cha akili. Au ni sawa na kusema kuwa Subconscius part inatazama kioo, kioo hicho ni conscious mind, na mawazo ni kama ukungu unaozuia subconscious kutazama conscious part.

Ili kuelewa vyema mawazo ni nini, chukulia mfano wa redio. Mwanadamu ni redio, mawazo ni mawimbi yako ya umeme. Kila wazo lijapo, ukilikubali na kulishikilia basi wazo hilo hutuma waves/mawimbi kwenye ulimwengu (To The Universe) na hufanya mpangilio wa universe kujiweka katika reality hiyo ya wazo hilo. Hivyo mawazo sio mabaya bali ubaya ni kuwaza mawazo mabaya na mawazo yasiyo na umuhimu katika safari ya maisha. Kama utajishikilia na mawazo na kuamini kuwa wewe sio kiongozi wa mawazo yako basi mawazo yatakutawala na utakuwa mtumwa wa kuitikia mawazo yako bila kujijua. Wengi sana wanatenda, wanaongea, au wanawaza kile kijacho akilini bila kuwa na time na space ya kujichunguza.

Hivyo ni vyema kuwa askari wa kutazama mawazo unayoyatazama bila kujishikilia nayo. Na ili kuweza kufanya hivyo ni kuweka mawazo yako au akili yako katika jambo moja. Ni kitu ambacho unaweza kuona ni rahisi lakini ni kigumu sana kwani hapo mwanzo katika dakika za mwanzo unaweza kumudu lakini baada ya muda akili itakudanganya kuwa its booring to do that na itaanza kuama na kuanza kuona kuwa
ni vigumu kuweka akili kwenye wazo moja.

Miaka ya kale watu walikuwa wanapata busara, hekima, nguvu ya maajabu, kuona nguvu za Mungu, na Kufunuliwa kupitia mafunzo yaliyokwepo ya kufundisha watu kuongoza akili zao.

Mfano mzuri unaotumika ni sala, nyimbo, meditation, yoga, n.k vyote hivi lengo lake kuu ukichunguza ni kukuongezea concentration. Unapoweka akili kwenye jambo moja na kuweza kumudu katika hali hiyo kwa muda mrefu kama lisaa, siku n.k unaongeza nguvu yako ya asili. Thats the fact. Ndio maana watu walioweza kufunuliwa hapo kale walishapitia kipindi cha kujitesa mfano kufunga, meditation, kuwa mbali na watu (kujitenga) n.k Katika kipindi hiko wanapata strength.

Third Eye ni sehemu ya nyuma ya macho na juu kidogo katikati ya macho yako. Ndani kuna peneal gland. Hii ni gland ambayo inatoa kemikali maalumu mara mbili tu katika maisha yako kemikali hii inatoka yenyewe.
Inatoka
  • Siku ukizaliwa
  • Na wakati unakata roho.
Kemikali hii imegundulika kuwa kwa watu wanaofanya meditation huwa inatoka pale mtu anapokuwa katika very deep meditation. Au pale unapoweka akili kwenye kitu kimoja au wazo moja tu basi unaamsha kemikali hii.

Pia ni vyema kufahamu Chakra ni nini. Ni sehemu kuu saba za nguvu ya mwili. Sehemu hizi hufunguka moja moja kutoka chini ya uti wa mgongo mpaka kwenye utosi. Nazo zinahusika sana ili kuelewa Third Eye.
 
nimeipenda hii mada, katika pitapita yangu niliwahi kutana na documentary moja imeandikwa bob prata ambayo aliita thoughts are things, yani kila kitu tukionacho duniani ni zao la fikra na pia alisema kua fikra zimegawanyika katika makundi mawili yani positive thoughts and negative thoughts ingawa binadam wengi wamejawa na negative thoughts thats why wanafeli ktk maisha na mipango yao, positive thoughts zinalazimishwa while negative zinakuja zenyewe so we are the products of what we think
big up kwa mleta mada

Asante sana kwa kuwa mfuatiliaji mzuri. Asante sana.
Karibu.
 
Najaribu kufanya zoezi la kukaa bila wazo.... Japo n ngumu....

Ni gumu. Lakini ukiendelea kujituma na kuzidisha muda wa kukaa bila kujishikilia na mawazo yako utakuja kuona ni raha na utaipenda hali hiyo. Pia utaona maisha yanabadilika na uelewa wako unazidi kuongezeka.

Labda nikupe ushauri ambao utakusaidia kwani wengi wanakosea wasipoambiwa hili.
Lengo sio kukaa bila wazo, huwezi kukaa bila wazo kwani mawazo huja kwani hutoka katika akili. Ongoza akili katika kitu kimoja, mfano pumzi, sauti, ukimya, au sauti za asili (Ndege, wanyama, sauti za maji kwenye mto, au mawimbi ya maji, au baharini/beach n.k). Unapoweka akili sehemu moja mawazo yanapungua. Halafu kama itazame akili yako na sio mawazo yako, hakikisha akili ipo sehemu moja na ukiona akili imeanza kujishikilia na mawazo urudishe katika sehemu yako ya concentration. Baada ya muda ukiweza kukaa bila kuruhusu akili kuama au akili kurudi kujishikilia na mawazo utaona sensation au waves zinakujia, ni ishara ya kuwa mwili umetulia na meditation inafanya kazi. Katika stage hii wengi wanashindwa kuendelea na kuweka akili kwenye sehemu moja na kuanza kuenjoy sensation ya meditation, ukiamisha akili na kuanza kuwaza au kuweka akili kwenye sensation utaona concetration imepungua na akili itaama, unachotakiwa ni kuwa, ukianza kuona raha kufanya meditation usihamishe akili kwenda kwenye raha inayokujia kwani itaondoka. Ili kuishikilia raha hiyo unapaswa kuendelea kuconcentrate kwenye breath, sauti au chochote ambacho ulikuwa unaconcentrate. Dont be fooled na raha itakayokuja, ukianza kuiona iache, na endelea kufocus. Hapo haitaisha itaendelea kuwepo. Hivyo cha muhimu ongeza concentration more and more.

Asante
 
Tena tujue kuwa wazo ni creative.Wazo ndio huumba. Uumbaji mkuu ni absolute creative power ambayo ndio Omnpotent.Unapowaza intelligently unaunganika na Mungu ambaye ndiye Abslolute creator, the Omnipotent.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom