Unafahamu nguvu ya Wazo?

Unafahamu nguvu ya Wazo?

Umesema Kuwa Ulijifunza kukaa bila kufikilia, pia ukagundua kuwa unapokaa bila kufikilia ndipo mtu anaweza kupata furaha halisi na kujitambua pia kunaongezeka.. swali ni kwamba mtu asiye waza chochote anawezaje kuwa na furaha na kujitambua kama unavyodai, wakati mawazo ndio source ya kutengeneza uhalisia wa vitu anavyovitaka binadamu? au usipo waza vitu unavyo vihitaji vitakuja automatically? maana ninavyojua mimi kama nahitaji kuwa na nyumba nzuri lazima niiwaze kwanza kabla sijaanza ku_implement effort kuipata, sasa utasemaje kuwa usipowaza chochote ndipo utakua na furaha!! How does it work? explain..

Habari Elimringi. Umeuliza swali bora sana.

Tatizo sio kuwa na mawazo. Tatizo ni aina ya mawazo uliyo nayo, pia tatizo sio tamaa bali tatizo ni aina ya tamaa uliyonayo.

Kukaa bila wazo ni hatua ya furaha kwani mawazo sio sisi, bali mawazo ni kama energy inayotengenezwa na kifaa tulichonacho kinachoitwa UFAHAMU (Consciousness) kwenye akili zetu. Mawazo ni energy kama energy nyingine, tunafahamu sheria ya energy - Haiishi bali hubadilika form moja kwenye nyingine lakini haiwezi kupotea kamwe ikishakwepo. Hivyo ukitaka kwenda vyema na maisha ni kuweka fikra sahihi na kutojishusha. Ni kutambua kuwa kama wewe upo basi hakuna kinachoshindikana. Ni kutambua bahati na zawadi uliyonayo na umerithi zawadi hiyo tangu evolution ya ufahamu wako.

Mawazo sio sisi, mawazo au wazo lipo nje yako na sio ndani yako. Ukiweza kufanya meditation utagundua kuwa meditation haina lengo la kutokuwa na mawazo bali ni lengo la kuweza kujifunza kuswitch aina ya mawazo na wazo moja kwenda lingine. Hongera sana kwa kujifunza kuongoza akili yako. Naamini ni step ya muhimu sana katika kujitambua.

Asante
 
Hakika mkuu nakumbuka nilipokua form 6 baada ya matokeo kuja tofauti na matarajio nilipata div 3.11 ila nilikua napenda sana kusoma udakitari au maabara ila nikapangwa nursing lakini nilisoma semester 1 nikaacha nikaomba upya,hapa ndipo nilikua napita sana JF na Facebook nikakutana na page ya JITAMBUE SASA nilijifunza mengi na nakumbuka nilikua naomba ushauri ili nitimize haja ya moyo wangu nikaanza meditation huku nikinuwia kabisa nitapa kozi ya udakitari au maabara kwa chuo cha kcmc moshi kwani ndio niliviomba na st joseph ikawa ya mwisho,lakini majibu yakatoka nimechaguliwa st joseph nikasema sitaenda ila kadri ninavyo jitahidi kutuliza akili naona kcmc nafasi nitapata kweli baada ya wiki mbili tu nafasi za uhamisho zikatoka na kozi zote zipo basi nikaomba maabara na nikaipata...ubize wa masomo nilishindwa kuendelea na meditation ila naanza upya maana inaonekana kuna vitu vingi kwenye meditation....shukrani jitambue sasa,shukrani apolo na pia mshana nawaelewa sana ninaitaji kujua zaidi
 
Mada nzuri lakini mwanzishaji 'kaingia mitini' sasa sijui mawswali atajibu nani?
Nipo hapa msaidizi wake shaka ondoa, huyu Boss ni mutu mukubwa ameenda fanya mengine muhimu, siyo kwamba nadharau kikao cha wana JF, hapana! tulimuomba tu atupe nasaha zake humu. then aendelelee na yake,

Uliza swali!
 
Kama unafanikiwa ukaunganisha thoughts & emotion unakua umefanya kitu kikubwa sana

Conscious na Subconscious hii kitu wengi hawaijui

Na ipo hata ktk biblia

Hongera Mleta Mada
 
Mkuu hiki kitu nime appreciate.
Why?
Kuna siku nilitulia sana kiakili mpaka nikajifeel utulivu usio wa kawaida nikasema ngoja nibet kwa kama dakika 10 hivi nilipata pesa kuanzia 2000/= mpaka 20k hivi gafla nikakosa ule utulivu na ukanipotea ndani ya dk 10 na zaid zilizofuata ile 20k ikapeperuka a/c ikasoma 0.

Nimejaribu kufanya hiki kitu ila inakua ngumu kwel kweli.
Ndani yake kuna furaha kwenye kutuliza akili.

ahsante kwa somo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii kitu inatakiwa ufanye muda gani na inatakiwa ufumbe macho au bila kufumba.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa uelewa wangu haina mda maalum ila inahitaji eneo iliyotulia ili upate concentration na utulivu wa hali ya juu na kuhusu kufunga macho siyo lazima sana ila unaweza kufunga kuongeza concentration,
 
Back
Top Bottom