Unadhani hawajisikii vibaya?

Unadhani hawajisikii vibaya?

Mshana (doto)
Umetoa Maelezo ambayo yanaumiza sana fikra za watu sana hasa kwa watanzania. Gavana wa benki yetu ametoa report za kukua kwa uchumi kama ulivyoeleza.

Mie nina mtizamo tofauti wakifikra na wewe. Kwa maelezo yako inaonesha kwamba unategemea serekali ndio ilete maisha bora kwa watanzani, Viongozi wetu hawana utashi wa kweli kuwahudumia wananchi nia yao ni kwa ajili ya matumbo yao na familia zao, fikiria kidogo tu wewe unalipa payee kiongozi halipi,

Unakatwa Mafao leo wanaleta sheria ya kwamba mafao yako yakajenge viwanda hela utaipata ukifikisha miaka 65, wao hio sheri kwao haitumiki 5 years wakimaliza hela wanachukua bila makato. hivyo basi mfumo wa maisha kwa dunia nzima ni waudanganyifu na kukatisha tamaa sana.

Cha Msingi ni kubadili mtizamo tu, kufanya kazi kwa bidii na kwa malengo kwa wale walioajiriwa watambue hiyo kazi ni daraja la kumpleleka kwenye kazi za kujiajiri. kwa wale majasiriamali ni kujitahidi kwa bidii kufanya kazi sana ili uwe na maisha bora bila kuilalamikia serekali yetu sikivu..
jubilant najua wazi umenifananisha na mtu fulani...
Umeongea vizuri kuhusu walioajiriwa na wale wajasiriamali lakini umewasahau kabisa wale wasio na ajira au kazi yoyote , ambao hao ndio msingi wa mada hii
 
inaumiza unapoona mtu mmoja au kundi la watu wanaojiona wao ndio wenye uchungu na hii nchi,wakati ukiwaambia kama kweli wanauchungu na hii nchi wajaribu kufanya kazi bila malipo kama wataweza,.kama kiongozi mkuu yeye anaowachaguwa na kuwapa ajira anadai anawafahamu je sisi wengine tusio julikana kwake nani atatuajiri?,hii nchi ni yetu sote siyo mali ya mtu mmoja,mtu umekulia nyumba ya kupanga mama akiuza walau vitumbua leo hii unamaliza chuo unakosa welekeo unatamani hata usingesoma usingezaliwa,.na wanao dai tujiajiri asilimia kubwa wameajiliwa,.yaani mifumo ya elimu inamuandaa mtu kuwa muajiliwa alafu leo mnadai tujiajiri....wabadili mifumo ya elimu ili watu waendae na dunia ya sasa na sio kutupa lawama kwa wahitimu ... I have a deep and profound mistrust of all politicians.
Craig Ferguson
 
inaumiza unapoona mtu mmoja au kundi la watu wanaojiona wao ndio wenye uchungu na hii nchi,wakati ukiwaambia kama kweli wanauchungu na hii nchi wajaribu kufanya kazi bila malipo kama wataweza,.kama kiongozi mkuu yeye anaowachaguwa na kuwapa ajira anadai anawafahamu je sisi wengine tusio julikana kwake nani atatuajiri?,hii nchi ni yetu sote siyo mali ya mtu mmoja,mtu umekulia nyumba ya kupanga mama akiuza walau vitumbua leo hii unamaliza chuo unakosa welekeo unatamani hata usingesoma usingezaliwa,.na wanao dai tujiajiri asilimia kubwa wameajiliwa,.yaani mifumo ya elimu inamuandaa mtu kuwa muajiliwa alafu leo mnadai tujiajiri....wabadili mifumo ya elimu ili watu waendae na dunia ya sasa na sio kutupa lawama kwa wahitimu ... I have a deep and profound mistrust of all politicians.
Craig Ferguson
Siasa zisizoakisi uhalisia huwa na matokeo mabovu sana! Kuna mengi ambayo yalihubiriwa kwenye majukwaa ya kisiasa kama yangetekelezwa kama yalivyotajwa hii nchi ingekuwa mbali sana kwenye nyanja zote bila kusahau ajira na makazi
 
1475586722250.jpg
 
Tunapopita mitaani asubuhi kwenda kazini na tunaporudi jioni wale vijana walioko vijiweni yale macho yao yanayotuangalia ukiwa makini kuyaangalia yanaongea mengi sana na kwa sehemu kubwa yamejaa maumivu
Yani hili...kila siku nikitoka kazini, wale vijana pale njiani wananiangalia ....mpk naona aibu..........wasijue kwamba ninakoshinda mshahara hauzidi 350k per month.......
mpk huruma......inauma sana aiseeee.............
 
Ni majanga makubwa sana Mkuu hasa ukitilia maanani utajiri mkubwa wa rasilimali mbali mbali ambazo tumejaliwa nchini.

Mfano ni Tanzanite ambazo nchi pekee duniani yenye madini haya ni Tanzania lakini wanashindwa kuyalinda na kujenga Kiwanja cha kusafisha tanzanite nchini, matokeo yake India ni ya kwanza duniani kwa mapato ya Tanzanite duniani kisha USA, Kenya na sisi ni wanne!!!

Takwimu za kukua kwa uchumi
Takwimu za kuongezeka pato la Taifa
Takwimu za kuanza kulipa deni la Taifa
Habari za kuhakiki watumishi hewa
Habari za kusitisha ajira nknk
Haya mambo yote haya ni kizungumkuti kwa kijana graduate asiye na ajira na mwenye kutegemewa na wazazi pale kijijini achilia mbali changamoto zake mwenyewe
 
kizazi hiki cha masalia ya ccm ndo tatizo.ifikapo 2020 na kuendelea hakutakuepo anaemkumbuka nyerere,hapo tutapiga hatua.
 
Kasie ni kweli kabisa lakini hakuna kitu kibaya kama kukata tamaa nimewaona wengi waliokuwa na ndoto nyingi lakini frustrations za ajira zikazima ndoto zote na leo hii ni watu wa bangi na viroba inauma sana

Ni kweli si vizuri kukata tamaa ila inahitaji ujasiri pale kila unayemuona anahekima na ukimuelezea mawazo yako atakutia moyo usonge mbele inakuwa sivyo. Badala yake anakukatisha tamaa inauma aiseeh.... siwatetei ila kuna waliojiingiza kwenye biashara haramu baada ya kuona kila walifanyalo holaa.
 
nimecheza anga zote mbili..jaribu kuanzisha biashara yako leo hii ili ujikwamue kimaisha baada ya kukosa ajira uone mziki wake
Kupata tu nyaraka za kukutambua kama mjasiriamali unaweza kukata tamaa na kurudi kijiweni ukavute bangi
Michakato migumu kuanzia kupata mtaji mpaka kusimamisha biashara imewashinda wengi
Tatizo la hawa watu wanakaa na visimu vyao na kupost blah blah bila kufika field kwenyewe. Leseni ya biashara hupati bila kwanza kusajili shughuli zako, ukitoka hapo uende TRA wakukadirie utakavyokuwa ukilipa kodi, na ili uende kupata hiyo leseni lazima ulipe kodi kabla hata hujaanza hiyo biashara; kote unakopita ni lazima watu wale ili mambo yaende fasta fasta. Ukija kwenye biashara yenyewe tabu tupu, hakuna hela mitaani!
 
Natumaini mtukufu Raisi anapita humu jukwaani atauona huu Ujumbe na kuufanyia kazi ...

Hata kama sio yy natumaini baadhi ya Viongozi wanapita sana humu kama wakiuona huu Ujumbe wasisite kumfikishia taarifa ...
Mtaani hali mbaya watu tunakula mpakani mwa mchana na usiku..
 
Well said! You are analyst,you have made a clear situational analysis.
I would like to ask for the solution of this problem without being waiting to government's employments.
Ujasiriamali si ndio kimbilio,lakini pa kuanza na huu ukakasi wa nchi ulipo.
 
Back
Top Bottom