Una cha kujivunia mwisho mwa mwaka 2019 ?

Una cha kujivunia mwisho mwa mwaka 2019 ?

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,606
Wanabodi , poleni na majukumu na misoto ya kila namna , kila leo !

Msoto wangu wote na jitihada zangu zote kuanzia January mpaka December 2019 nimefanikiwa yafuatayo :-

1. Kununua shamba la ekari 2 kilomita 15 toka Moshi Mjini kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji lenye maji ya kutosha kutoka kwenye chemchem , na nimeanza kulilima vitunguu msimu wa 1

2. Nimejenga banda la kuku 300 kwa matofali na kuezeka kwa bati. Kuku sijaanza kufuga

3. Beers , kitimoto , kusomesha mtoto mmoja pamoja na kulea familia


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka mambo mengi sana sijui kama nitaweza kukumbuka.

Tuanze na wiki hii tu.

Juzi nimemsaidia mtu Tanzania alipokwama kwenye biashara yake.

Jana nimeokota wallet iliyokuwa na hela, credit cards na drivers licence na kuiripoti. Mwenyewe kaipata.

Haya ni mambo mazuri ya kufurahia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom