Wewe hueleweki! Weka mada yako vizuri ili usije kueleweka visivyo na ulivyokusudia. Unaposema pesa ndiyo msingi mkuu wa mapenzi wengine hatukuelewi kwa sababu tuna ndugu na tumeshawahi kuwa na ndugu ambao kwa kweli hawana na hawakuwa na chochote zaidi ya mapenzi ya kweli.
Wengine wameishi kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 50! Sasa ni wazi walikuwa hawashindi wala kulala njaa lakini pia hawakuwa na 'pesa'. Sasa pesa ndiyo msingi mkuu wa mapenzi...pesa kiasi gani? Za kutosha tu kujipatia mahitaji muhimu au nyingi za kusaza na kumwagia radhi?
Weka kiwango watu tujue unachokiongelea. Kama ni mshahara wa milioni kumi kwa mwezi sema, usiogope.
wewe bana you have outgrown that fairy tale thing acha ligi a ubishi for the sake of ubishi, mambo ya snow white na cinderella tuyaache vitabuni
nimeshakwambia pesa sio kipande cha karatasi au chuma tu, kama hilo huelewi basi tumia tafsiri hii: kuwa na pesa = kuwa na uwezo wa kujikimu/kujitosheleza kiuchumi
The thing is I live in real-ville. Wapo watu ambao nawajua hawana pesa na wamekuwa pamoja kwa zaidi ya miaka 50. Sasa wewe unapokuja na habari zako za eti pesi ndiyo "msingi mkuu wa mapenzi"....come on now? Are you serious? Maybe you are but I'll submit to you that that's not the case for everybody. Some people don't put money ahead of character and moral rectitude and I'm one of them.
kwani kabula alishushwa kutoka mbinguni kama manna?
Kama ni hivyo basi badili kauli yako na useme "uwezo wa kujikimu na kujitosheleza" ni moja ya misingi mikuu au nguzo kuu za mapenzi. Ukisema "pesa" tu ndiyo "msingi mkuu" wa mapenzi mimi nakataa.
hii ni kote (universal) na wakati wote (timeless), toka enzi za kutumia barter trade and cowry shells; hata msingi wa mahari umejikita katika kanuni hii ya pesa posa - haijalishi wewe ni mzungu, mswahili, mhindi au mchina wala haijalishi uko mjini, kijijini; ulaya au afrika.
Hakushushwa toka mbinguni na wala halelewi kutukuza pesa kwa sababu kwenye maisha si pesa tu iliyo muhimu. Hata maadili mema, heshima, taadhima, upendo, n.k. nayo ni muhimu vile vile.
Kamwe siwezi kumfunza kutukuza pesa na kuweka pesa mbele ya utu. Not under my watch.
naona unaliogopa sana neno pesa, mantiki ndiyo hiyo hiyo kwa kuwa sasa kipimo cha uwezo wa kujikimu na kujitosheleza ni pesa tu; kwani unapobeba maboksi unalipwa maziwa ya kumpa kabula? si unapewa benjamins!
Weka figures....mbona unazungumzia broad generalities tu?
hakuna sehemu ambapo tumesema maadili, heshima, taadhima na upendo sio muhimu - vyote hivyo ni muhimu ila pesa ni muhimu na lazima. tatizo bado una taadhira za ujamaa uliodai pesa ni matokeo tu hivyo japo kila kukicha unabeba maboksi upate pesa bado unadhani kuwa kuzipata huko ni matokeo kumbe ndio msingi mkuu wa kubeba maboksi.
Sidhani kama kuna kiwango maalum cha pesa.
Hapa itategemea mtu na mtu na wapenzi na wapenzi na ndipo jana kwenye thread ya Companero niliposema nadhani ni vyema ikiwa kwa viwango vya mwanamke
Love without money is dead - penzi bila pesa limekufa.
Uliposema pesa ndiyo msingi mkuu wa mapenzi hayo mengine hukuyataja kwa hiyo kwako hayakuwa na umuhimu sawa na pesa. Ungeyataja wala nisingekuwa na tatizo na hiyo kauli yako.
Na kwamba katika dunia ya leo pesa ni muhimu, hilo halina ubishi. Ubishi upo kwenye kauli yako ya pesa ndiyo msingi mkuu wa mapenzi. Kama ingekuwa kwel basi mamilionea na mabilionea ndiyo wangekuwa na mapenzi ya kweli.
Companero, mfumo dume unaoongelea unakubalika haswaa! Tatizo lipo katika mfumo kandamizi, kuwekeana limit ya potentials. Kila mtu ana potentials zake, be it a man or a woman. Nisizuiwe kupaa zaidi just becoz I am a woman. Nisipigwe kwa sababu ni mwanamke (tukubaliane anaechelewa nyumbani mwenzie ampige, and see where that gets us!)
Actually sijioni kama naweza kuwa na mwanaume asiye na hizo 3Ps.
My man has to take the lead, kama kichwa cha nyumba. Hata nikisema, kutoa wazo ama kufanya namsaidia. Kuwa provider haimaanishi uwe ndo na hela nyingi ama u-cover kila kitu. Kuna mwanaume anaingia na kutoka nyumbani kwake hajui mwenza wake wala wanae wanakula wala kuvaa nini! Lakini hata kama kipato ni kidogo at least baba anarudi home anapokelewa!