naona unajipinga mwenyewe japo somo linazidi kukuingia taratibu na kwa uhakika- narudia tena, pesa ndio msingi mkuu wa mapenzi; ndio mhimili ambapo hivyo vitu vingine muhimu vinazunguka; ondoa pesa kabisa kila kitu kinavurugika.
unaniangusha, hivi kweli huelewi lojiki ya necessary but not sufficient ?
constant flow of money/pesa ya uhakika wakati wote
unarudi tena kwenye fairy tales za cinderella na sokonoko
Hapa unamuingiza chaka comrade! Hakuna constant flow of money, hata uchumi wa marekani tu unapitiaga mdororo! This is one thing the younger generation needs to know. Maisha ni mlima,lol! Saa ya kupanda I won't easily let go of my man's hand unless ameketi!
NN, nachelea kuwa unamiss the fact kuwa kuwa provider na kuwa na pesa ni vitu viwili tofauti.
Unaweza kuwa na pesa sana na usiwe provider and vice versa. Kutoa ni moyo, usambe ni utajiri.
Mfano tu mdogo among ur friends, kuna mtu kila wakati atakununulia a small gift, it is the thought that counts aisee. Huku kwetu kuna mwanaume kila akitoka kibaruani anakuwa na kirambo kina miguu ya kuku, utumbo wa kuku ama dagaa wa kukaanga. Huyo ni provider. Anaweza asiwe na hela ya kutosha kuacha home lakini walau anawaza wa nyumbani kwake.
Nipe basi hizo pesa zako
Kuna wanaume wangapi wana hizo sifa lakini bado wake/ wanawake zao wana-cheat?
Juzi juzi tu hapa mtaani kuna mkaka mmoja Harvard kauliwa na hawara wa mke wake. The guy has everything going for him....kama "pesa" zingekuwa msingi mkuu wa mapenzi iweje mkewe aanzishe affair na mtu mwingine aliyekuja kumuua mumewe?
Hujanisoma vizuri. Maybe hapo kulikuwa na mfumo kandamizi somewhere. Kuwa provider haimaanishi monetary peke yake. Mwenza (ama ni wanawake pekee?) Needs to be valued, respected and protected. Kama unanirushia hela ya matumizi mezani unatoka bila kuaga then kuna only two things involved. I will leave u, or else nikufanye kamtaji ka biashara and cheat. But mie kwa sababu siogopi na siachi kusaka hela pia, maybe nitakuacha!
Mie naamini wanawake wengi wanacheat for emotional issues, kitu ambacho kinakubaliana na usemi kuwa money isn't everything but surely is something
unachosema kina ukweli kias fulani ila bado kanuni ni universal au unataka kusema kuna wanawake wote wanaona kutibiwa aga khan ni sawa na kutibiwa dispensary ya kata? au wanawake wote wanaona ni sawa watoto wao kusoma shule ya kata na kusoma mzizima? hivi umesahau pia kuwa wapo ambao hawana jinsi kama kule ambako wanasema better half a man than not a man at all?
Hahahaaa funny coz you are playing right into my argument. Jamaa kasema kuwa pesa ndiyo "msingi mkuu wa mapenzi" na mimi nimekataa. Pesa siyo msingi mkuu wa mapenzi. Sasa sisemi kwamba kuwa na pesa ni vibaya. Katika akili yangu huwa napenda kudhani hakuna mtu anayependa pesa kama mimi lakini huwa siachi kujiumbusha kwamba pesa siyo kila kitu hapa duniani na 'pesa siyo msingi mkuu wa mapenzi'.
Nnachosema ni kuwa kiwango kitakachoonekana kinatosha kwa mmoja kinaweza kisionekane kinatosha kwa mwengine. Hakuna universality hapo
Bado unajifunga mwenyewe, kwani injini ndio kila kitu kwenye gari? Si kuna mafuta, matairi na kadhalika. Ila si gari haliwezi kwenda bila injini? Vivyo hivyo mapenzi hayawezi kwenda bila pesa. Kama unabisha leta hizo pesa ambazo umeshakiri ni kwa ajili ya Kabula ambaye ni zao la penzi. Naam ni zao tamu la penzi ambalo injini yake ilikuwa ni pesa.
Hahahaaa funny coz you are playing right into my argument. Jamaa kasema kuwa pesa ndiyo "msingi mkuu wa mapenzi" na mimi nimekataa. Pesa siyo msingi mkuu wa mapenzi. Sasa sisemi kwamba kuwa na pesa ni vibaya. Katika akili yangu huwa napenda kudhani hakuna mtu anayependa pesa kama mimi lakini huwa siachi kujiumbusha kwamba pesa siyo kila kitu hapa duniani na 'pesa siyo msingi mkuu wa mapenzi'.
Mimi mdada akinijia na gia za kupenda penda pesa natupa kule jalalani!!