benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Umoja wa Afrika (AU) umeridhia kumuunga mkono Spika wa Bunge la Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) kuwa Mgombea pekee kutoka Bara la Afrika wa nafasi ya Urais wa Jumuiya ya
Mabunge Duniani (Inter-Parliamentary Union-IPU).
Uamuzi huo ulifikiwa katika Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri la Umoia wa Afrika uliofanyika Jijini Nairobi, Kenya tarehe 13 hadi 14 Julai, 2023 baada ya Baraza hilo kupokea na kuridhia ombi la Seriali ya Tanzania la kumuunga
mkono Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) katika kugombea nafasi hiyo.
Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) tayari ameungwa mkono na Bunge la Afrika (PAP), Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) na Jukwaa la Mabunge ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC PF) katika kugombea nafasi hiyo. Uchaguzi wa Rais wa Jumuiya ya Mabunge Duniani (Inter-Parliamentary Union-IPU) unatarajiwa kufanyika tarehe 27 Oktoba, 2023 chini Angola.
Mabunge Duniani (Inter-Parliamentary Union-IPU).
Uamuzi huo ulifikiwa katika Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri la Umoia wa Afrika uliofanyika Jijini Nairobi, Kenya tarehe 13 hadi 14 Julai, 2023 baada ya Baraza hilo kupokea na kuridhia ombi la Seriali ya Tanzania la kumuunga
mkono Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) katika kugombea nafasi hiyo.
Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) tayari ameungwa mkono na Bunge la Afrika (PAP), Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) na Jukwaa la Mabunge ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC PF) katika kugombea nafasi hiyo. Uchaguzi wa Rais wa Jumuiya ya Mabunge Duniani (Inter-Parliamentary Union-IPU) unatarajiwa kufanyika tarehe 27 Oktoba, 2023 chini Angola.