Umewahi kusoma kitabu, The Richest Man In Babylon? Ulijifunza nini? Kinasaidia?

TIBA YA TANO - Fanya makazi yako kuwa uwekezaji wenye faida.


"Iwapo mtu anatumia tisa ya kumi ya pato lake kwa mahitaji ya msingi na kufurahia maisha, na iwapo sehemu ya hii fedha anaweza kufanya uwekezaji wenye kuleta faida bila kuathiri maisha yake, hazina yake itakuwa kwa kasi sana." Hivyo ndivyo alivyoanza kuongea Arkad kwenye siku ya tano.

"Watu wengi hapa Babiloni hutunza familia zao kwenye nyumba za mbavu za mbwa na zilizo sehemu mbaya kabisa. Nyumba zisizofaa watu kuishi. Huko wanawalipa wenye nyumba kodi kubwa kwa nyumba ambazo hata nafasi ya kupanda maua ya kufurahisha moyo hakuna. Watoto wao hawana hata sehemu ya kucheza bali hucheza kwenye vichochoro vichafu.

"Hakuna familia inayoweza kufurahia maisha bila ya watoto kuwa na sehemu safi ya kucheza na eneo ambalo mke anaweza kupanda si tu maua bali pia mbogamboga kwa ajili ya familia yake.

"Inafurahisha mtu kula matunda kutoka kwenye mti wake na zabibu za bustani yake. Kumiliki makazi yake na kujivunia sehemu yake. Hilo litamfanya ajiamini na aweze kutimiza malengo yake mengine kwa moyo mmoja.

"Hivyo, napendekeza kila mtu amiliki nyumba kwaajili yake na familia yake.
"Kumiliki nyumba si jambo lisilowezekana kwa wale walio na nia. Je mfalme wetu hajatanua kuta za Babeli ili kuwe na eneo kubwa na sasa mtu anaweza kununua kiwanja kwa bei nafuu?

"Pia niwaeleze kitu kingine, wakopesha pesa hutafuta watu wanaokopa kwaajili ya kununua ardhi na ujenzi wa nyumba. Watakukopesha haraka ili umlipe mfyatua tofali na mjenzi, utahitaji tu kuonyesha kiasi kidogo ulichotenga kwaajili ya kazi hiyo.

"Ukishajenga nyumba unaweza kumlipa mkopeshaji kama ulivyokuwa unamlipa mwenye nyumba. Kila unaporejesha unakuwa unapunguza deni na baada ya miaka michache unakuwa umemaliza.
"Hapo utafurahi kuwa na nyumba yako mwenyewe na hutadaiwa na mtu zaidi ya kodi ya mfalme tu.

"Pia mkeo akienda mtoni kufua anaweza kurudi na maji ya kumwagilia bustani. Baraka nyingi huja kwa mtu anayemiliki nyumba yake mwenyewe. Pia hili hupunguza sana gharama za maisha. Pesa nyingi hubaki kwaajili ya kustarehe na kutimiza matamanio mengine. Hii ndiyo tiba ya tano ya pochi iliyo tupu.

Miliki nyumba yako mwenyewe.


TIBA YA SITA - Hakikisha wakati ujao utakuwa na kipato.

"Maisha ya kila mmoja huanzia utotoni hadi uzeeni. Hii ni njia ya maisha na mtu hawezi kuiepa isipokuwa miungu imemuita mapema. Hivyo ninasema kuwa ni muhimu kwa mtu kufanya maandalizi ili wakati ujao awe na kipato. Kipindi ambacho hatakuwa kijana tena. Pia anatakiwa kuweka maandalizi kwaajili ya familia yake ili isihangaike ikitokea Miungu imemuita mapema. Kwa hiyo nasema kuwa ni jambo la muhimu kwa mtu kufanya maandalizi ili aje kuwa na kipato uzeeni, nyakati ambazo hatakuwa kijana tena. Na pia kufanya maandalizi kwaajili ya familia yake iwapo atafariki. Somo hili linafundisha kuhakikisha pochi yako imetuna hata wakati ambapo huwezi kufanya kazi ya kuingiza kipato.

Hivyo ndivyo alivyoanza kusema Arkad katika siku ya sita.

"Mtu ambaye anajua kanuni za utajiri na akaweza kujipatia utajiri ni muhimu akafikiria kuhusu wakati ujao. Anatakiwa kuwekeza kwenye miradi ambayo ni salama na inadumu kwa miaka mingi. Laki mapato kutokana na miradi hiyo yanatakiwa kupatikana kirahisi mara yatakapohitajika.

"Kuna njia nyingi ambazo mtu anaweza kuhakikisha kuwa wakati ujao atakuwa salama. Anaweza kuwa na sehemu ya siri na kufukia hazina yake hapo. Lakini hata afiche namna gani lazima siku moja wezi wataipata. Kwa hiyo sishauri kufanya hivyo.
"Mtu anaweza kununua nyumba au ardhi kwaajili ya wakati ujao. Kama amechaguwa vizuri na kuna uwezekano wa kupanda thamani huko mbeleni, hivi ni vitu vyenye thamani ya kudumu. Mapato yake au mapato kutokana na kuviuza yanaweza kufaa kwa ajili ya wakati ujao.

"Pia anaweza kukopesha pesa zake huku akiziongeza mara kwa mara. Riba inayoongezwa kwenye pesa hiyo itafanya pesa yake ikue haraka sana. Minamfahamu mtengenezaji wa makubazi mmoja anayeitwa Ansam. Ansam aliniambia kuwa kila wiki huweka vipande viwili vya fedha kwa mkopesha pesa. Amekuwa anafanya hivyo kwa muda wa miaka minne sasa. Hivi karibuni ameenda kuona akiba yake na imemfurahisha sana. Pesa yake, ukichanganya na riba ya moja ya nne kwa kila miaka minne imefikia jumla ya vipande elfu moja na arobaini vya fedha.
"Kwa ujuzi wangu wa masuala ya fedha nilimhamasisha kuendelea kuweka kwa kumuonyesha kuwa; akiendelea hivyo kwa miaka kumi na miwili mingine atakuwa anamdai mkopesha pesa vipande elfu nne vya fedha. Kiasi kitakachomtosha maisha yake yote.
"Kiasi kidogo hivyo kikiwekezwa kwa ukawaida huwa kikubwa sana. Hakuna mtu ambaye hawezi kuweka akiba kwaajili ya uzee wake na kwaajili ya wakati ujao wa familia yake. Hilo halijalishi biashara yake ni kubwa kiasi gani au ana miradi gani.

Nategemea siku moja watu wenye akili watabuni bima ya kifo. Watu wengi eaweke pesa kidogokidogo na kisha mmoja wao anapokufa basi familia yake wapewe kiasi fulani. Hili naona kama litakuwa jambo zuri na napendekeza lifanyike. Lakini hili kwa sasa ni gumu kufanyika kwa sababu ni jambo linalofanyika baada ya ya maisha ya mtu au ushirika wowote wa kibiashara. Ila ili ufanye kazi unatakiwa kuwa imara kama kiti cha ufalme.
Lakini siku moja nafikiri hilo litawezekana na kuleta baraka kwa watu wengi. Hata pesa ndogo iliyowekezwa itafanya familia ya marehemu kulipwa pesa za kutosha.

Lakini kwa sababu tunaishi katika siku hizi, basi tunatakiwa kutumia njia zilizopo. Kwa hiyo basi nashauri watu wote kutumia njia zilizothibitika kuwa ni bora ili kujiandaa kwa ajili ya miaka ya uzeeni. Mtu asiye na kitu na hawezi kufanya kazi au familia iliyoondokewa na kichwa cha familia na kuachwa bila kitu ni janga kubwa sana.

Hii ndiyo tiba ya sita, hakikisha una kipato kwajili ya uzee wako, na kwaajili ya ulinzi wa familia yako.
 
TIBA YA SABA - Ongeza pato lako.

"Leo nitazungumza moja ya tiba muhimu kabisa ya pochi iliyo tupu. Sitazungumza kuhusu fedha bali nitazungumza kuhusu ninyi. Nitaongea kuhus nyinyi mliokaa hapa mbele yangu mkiwa mavazi ya kuvutia. Nitazungumza juu ya vitu ambavyo vipo katika akili na maisha ya watu, na kukwamisha mafanikio yao."

Hivyo ndivyo alivyoanza kuongea Arkad kwenye siku ya saba.

"Siku si nyingi zilizopita alikuja kwangu kijana mmoja akiomba mkopo. Nilipomuuliza anataka kwaajili ya nini, akasema kuwa pato lake halitoshi kulipia mahitaji yake. Hilo lilifanya wakopesha pesa wasiweze kumkopesha kwa kuwa hakuwa na kipato cha ziada cha kumuwezesha kulipa mkopo.
'''Nilimwambia, unachotakiwa kufanya,' ni kuongeza kipato. Umefanya jambo gani ili kujiongezea kipato?'

"'Nimefanya kila njia' alijibu. 'Mara sita kwa muda wa miezi miwili nimemfuata bosi wangu na kuomba nyongeza ya mshahara bila mafanikio. Siwezi kwenda zaidi. Hakuna mtu anaweza kwenda zaidi ya hapo.'

"Tunaweza kucheka na kumuona ni mzembe lakini alionyesha jambo muhimu linalohitajika ili kujiongezea kipato. Ndani yake alikuwa na nia ya kujiongezea kipato. Nia yenye nguvu.

"Nia inaanza kisha mafanikio hufuata. Nia yako inatakiwa kuwa yenye nguvu na yenye lengo. Nia ya jumla ni dhaifu na ni kama matamanio tu ya kupoteza wakati. Kutamani tu kuwa tajiri hakutakufikisha popote. Ila kutamani kupata vipande vitano vya dhahabu ni kitu kinachoeleweka na kinaweza fanyiwa kazi hadi kikatimizwa.

"Hapo unaweza kutafuta njia ya kupata vipande kumi, kisha ishirini na baadaye vipande elfu moja. Kuja kutazama, umeshakuwa tajiri. Baada ya kujifunza kutimiza malengo madogo unakuwa umepata uzoefu wa kukuwezesha kutimiza malengo makubwa. Hivi ndivyo utajiri unavyopatikana. Kwanza kwa kuweza kumudu kiasi kidogo na baadaye kiasi kikubwa kadri unavyoongeza uwezo.

"Lengo linatakiwa kuwa rahisi na linaloeleweka. Inakuwa haina maana ya kuwa na malengo uwapo ni mengi, hayaeleweki na yapo juu ya uwezo wa mtu kuyatimiza."

"Kadri mtu anavyotimiza malengo yake ndivyo uwezo wake wa kuongeza kipato unavyoongezeka. Kipindi kile nilipokuwa muandishi niligundua kwamba, wafanyakazi wengine walifanya zaidi na kupata zaidi. Hilo lilifanya niweke lengo la kutozidiwa na yeyote. Haikuchukua muda nikajua siri ya kufanikiwa kwao. Kuipenda kazi, kufanya kazi kwa umakini na kuwa mvumilivu. Baada ya muda ni watu wachache tu ndiyo walioweza kuandika mabamba mengi kuliko mimi. Bila kuchelewa, ujuzi wangu ulianza kunipa faida haraka. Wala hakukuwa na ulazima wa kwenda kwa bosi wangu mara sita ili anitambue.

"Kadri tunavyoongeza maarifa ndivyo tutakavyoongeza kipato chetu zaidi. Mtu anayejitahidi kuijua kazi yake vizuri atapata mafanikio zaidi.
Kama ni fundi sanaa basi anatakiwa kujua mbinu za mafundi bora kabisa wa sanaa. Kama ni mwanasheria au ni mganga basi anatakiwa kuomba ushauri na kubadilishana ujuzi na watu walio kwenye nyanja yake. Kama ni mfanyabiashara, inampasa kuendelea kutafuta bidhaa bora ambazo zina bei ya chini.

"Maisha ya mwanadamu hubadilika na kuwa bora sababu ya watu wenye udadisi na wenye kutafuta ujuzi kwa faida ya wote. Nawahimiza watu wote kuwa mstari wa mbele wa maendeleo na si kukaa kizembe na kuachwa nyuma. Pia mtu anayejieshimu anatakiwa kufanya mambo kama haya yafuatayo:

"Anatakiwa kulipa madeni yake haraka iwezekanavyo, hatakiwi kununua kitu asichoweza kumudu. Anatakiwa kujali familia yake, hilo litafanya imheshimu na imuongelee vyema.

"Anatakiwa kuacha wosia kwa maandishi ili siku akifa mali yake igawanywe kwa utaratibu.
"Anatakiwa kuwa na huruma kwa wagonjwa, wasiojiweza na wale waliopatwa na majanga. Awasaidie kulingana na uwezo wake. Anatakiwa kuwa mkarimu kwa wapendwa wake.

"Kwa hiyo, tiba ya saba na ya mwisho ya kutibu pochi iliyo tupu ni kuwa mtu bora. Kujifunza na kujizoeza kupata maarifa zaidi, kupata ujuzi zaidi na kujiendesha kwa heshima. Hapo unaweza kujiamini na utaweza kutimiza malengo yako.
"Hizi ndizo tiba saba za pochi tupu. Kutokana na maisha yangu marefu yenye mafanikio nawahimiza watu wote wanaotamani utajiri kuwa.

"Kuna dhahabu nyingi ndani ya Babiloni kuliko mnavyodhania. Nyingi za kutosha kila mtu.

"Nendeni mfanyie kazi mambo niliyowaambia nanyi mtafanikiwa kuwa matajiri.
"Nendeni mkafundishe ukweli huu kwa raia wote wa mfalme ili nao washiriki utajiri wa jiji letu kuu."

Mwisho wa sura ya tatu.
 
Jaza wazo hili ndani yako na tunza kiasi unachoona kinafaa ila isiwe chini ya moja ya kumi ya pato lako. Ikiwa kuna ulazima, badili matumizi yako ili kufanikisha hili. Baada ya muda utaanza kuhisi hisia za utajiri. Akiba inayokua itakuletea furaha, furaha ya kumiliki kitu chako mwenyewe. Kadri hazina yako inavyokuwa ndivyo utakavyochochewa kuweka zaidi. Utapata furaha maishani na nguvu ya kutafuta zaidi itakuingia. Je, kadri unavyopata zaidi si na kiasi unachotunza kitaongezeka?

"Baada ya hapo jifunze jinsi ya kufanya akiba yako ikutumikie. Ifanye mtumwa wako. Wafanye watoto wake na watoto wa watoto wake wakutumikie.

"Hakikisha una kipato kwaajili ya siku zijazo. Waangalie wazee na kumbuka kuwa siku zijazo nawe utakuwa mzee. Hivyo wekeza kwa tahadhari ili hazina yako isipotee. Biashara zenye kudai zina faida kubwa ni mtego na udanganyifu. Ni nyimbo zinazoimbwa ili kumvuta mtu asiye makini kwenye hasara na majuto.

Hakikisha familia yako haitateseka iwapo Miungu wakikuita. Unaweza fanya hivyo kirahisi kwa kutunza pesa kidogokidogo mara kwa mara. Mtu mwenye fikra za mbele hasubiri kupata kiasi kikubwa ndiyo akitunze au akiwekeze kwa wakati ujao.

"Jadiliana na watu wenye hekima. Tafuta ushauri kutoka kwa wale wanaofanya kazi zihusuzo pesa kila siku. Hao watakusaidia kuepuka makosa kama niliyofanya mimi kwa kumpa pesa zangu Azmur, mfyatua matofali. Faida ndogo penye usalama ni bora kuliko faida kubwa lakini penye hatari ya kupoteza mali zako.

"Furahia maisha ungali bado upo duniani. Usijibane kupita kiasi ili kutunza pesa, na usijaribu kutunza kiasi kikubwa kuliko uwezo wako. Kama sehemu ya kumi ndiyo unayoweza kutunza bila kupata taabu basi ridhika na kutunza kiwango hicho tu. Ishi kulingana na kipato chako ila usiwe bahili na kuogopa kufanya matumizi. Maisha ni matamu na yana vitu vingi vya kufurahia."

Rafiki zake wakamshukuru na kwenda zao. Wengine walikuwa kimya kwa sababu haikuwaingia akilini na hawakuweza kuelewa. Wengine walidhihaki kwa kusema "mtu tajiri hivyo alitakiwa kugawana utajiri wake na rafiki zake wasio na kitu." Lakini wengine walikuwa wamepata mwanga mpya. Walielewa kuwa, Algamish alirudi kwa Arkad mara nyingi sababu alikuwa anataka kumuona mtu akitoka gizani hadi kwenye mwanga. Mtu huyo alipopata mwanga fursa zilimsubiria, hakuna anayeweza kutumia fursa hizo mpaka afanye bidii kupata uelewa kwanza.

Hawa ndiyo ambao baadaye walikuwa wakimtembelea Arkad kila mwaka. Aliwashauri na kuwapa maarifa yake bure kama ambavyo watu wenye maarifa na busara nyingi hufanya. Pia aliwasaidia kuwekeza akiba zao ili wapate faida nzuri bila ya kuingia katika hatari ya kupoteza pesa zao wala kuingia kwenye uwekezaji usioleta faida. Maisha ya watu hawa yalibadilika siku ile walipogundua ukweli uliotoka kwa Algamish kwenda kwa Arkad. Kutoka kwa Arkad hadi kwao.

Sehemu fulani ya pato unalopata ni yako.

Mwisho wa sura ya pili.
Hongera sana mkuu!! umefanyika baraka sana kwangu!! Mungu akubariki kwa kutumia muda wako mwingi, kushea nasi kitu cha baraka!!
 
KUTANA NA MUNGU WA BAHATI


kama mtu ana bahati huwezi jua inapoishia. Mtupe ndani ya mto Efrati naye atatoka ameshika lulu.
-Methali ya wababiloni


Kila mtu anatamani kuwa na bahati njema. Katika Babiloni, tamaa hiyo ina nguvu leo kama tu ilivyokuwa miaka elfu moja iliyopita. Wote tuna matumaini ya kutembelewa na Mungu wa bahati njema. Je, kuna njia ya kumvuta atutembelee? Siyo tu atuone bali atupatie bahati pia.
Je, kuna njia ya kufanya mtu awe na bahati?

Hili ndilo watu wa kale wa Babiloni walitaka kujua. Na ndilo jambo waliloamua kulichunguza. Walikuwa ni watu wenye hekima na wenye kufikiri kwa makini. Kitendo cha mji wao kuwa tajiri kuliko yote ni ushahidi wa hilo.

Zamani hizo hawakuwa na shule wala vyuo lakini walikuwa na sehemu ya kujifunzia na walipata elimu yenye kufaa sana. Katika majengo makubwa ya Babiloni kulikuwa na moja lililolingana kwa umuhimu na ikulu ya mfalme, bustani zilizoning'inia na mahekalu ya Miungu. Lakini si rahisi kulikuta limetajwa kwenye vitabu vya historia na muda mwingine halitajwi kabisa. Pamoja na hilo, jengo hili lilikuwa na ushawishi mkubwa sana wakati ule.

Jengo hili ni Hekalu la Elimu. Humo maarifa ya kale yalifundishwa na walimu wa kujitolea na ambamo mambo yahusuyo jamii yalijadiliwa kwa uwazi. Ndani ya jengo hili watu wote walikuwa sawa. Mtumwa wa hali ya chini aliweza kubishana vikali na mwana mfalme.

Mmoja wa watu waliopenda kutembelea Hekalu la Elimu alikuwa ni mtu mmoja tajiri sana aliyeitwa Arkad, ilisemwa ndiye mtu tajiri zaidi katika Babeli.

Alipendelea kuingia kwenye ukumbi mmoja ambao kila jioni. Wengine wazee na wengine vijana lakini wengi walikuwa watu wa umri wa kati. Walikusanyika wakijadiliana na kubishana kuhusu mambo yaliyowahusu. Hebu tufanye kama tunawasikia tuone kama wanajua mbinu za kuvuta bahati.

Jioni ya leo jua lilikuwa kama mpira mwekundu likimulika kwa shida kupitia vumbi la jangwani lililojaa angani. Huu ndiyo muda Arkad alikuwa anaingia ukumbini. Tayari watu wanne walikuwa wameshafika. Walikuwa wamekaa kwenye mazuria madogo sakafuni. Wengine wengi walikuwa wakiwasili.

"Tutajadili nini usiku wa leo?" Aliuliza Arkad.
Baada ya kimya kifupi, mtu mmoja mrefu ambaye alikuwa ni mshona nguo akasema, huku akisimama kama ilivyo desturi.
"Nina jambo ambalo ningependa lijadiliwe ila nasita kulisema lisije onekana ni la kijinga mbele yenu."

Baada ya kutiwa moyo na Arkad na wale wengine kulisema, akasema: "leo nilikuwa na bahati, niliokota pochi iliyokuwa na vipande vya dhahabu ndani. Napenda niendelee kuwa na bahati. Nadhani kila mtu anatamani hivyo, kwa hiyo napendekeza leo tujadili jinsi ya kuvuta bahati. Pengine tunaweza kujua mbinu ya kuivuta."

"Hiyo ni mada nzuri sana," akasema Arkad. Inafaa kujadiliwa. Kwa watu wengine bahati ni kama ajali tu. Inatokea bila sababu wala lengo lolote. Wengine waanamini mletaji wa bahati njema ni Mungu wetu mwenye vitu tele, Ashtar. Inasemwa kuwa tamaa yake ni kuwatunza wale wamfurahishao. Tujadili suala hili rafiki zangu. Mnasemaje, tuchunguze iwapo kuna njia ya kuweza kuvuta bahati?
"Ndiyo! Ndiyo! Tuchunguze! Lilijibu lile kundi kwa shauku.

Arkad akaendelea. "Kuanza mjadala wetu, kwanza tusikie kutoka kwa wale ambao wamewahi kukutana na kitu kilichomkuta mshona nguo. Kupata au kupokea kitu cha thamani bila ya kutumia jitihada zozote."

Kulikuwa na ukimya, kila mmoja akitegea labda kuna mtu atasema lakini hakuna aliyesema.

"Hakuna hata mmoja?" Akasema Arkad. "Basi bahati ni kitu adimu sana. Nani atoe muongozo wa jinsi ya kuanza uchunguzi wetu?"

"Ngoja nianze," akaongea kijana fulani aliyekuwa kavalia nadhifu huku akisimama. "Mtu anapoongelea kuhusu bahati si moja kwa moja anakuwa anazungumzia kuhusiana na kucheza kamari? Si huko ndiko tunapata watu wakijitahidi kumfurahisha Mungu wa bahati wakitegemea atawabariki kwa ushindi?"

Alipotaka kukaa akasikia sauti ikisema, "usikae, endelea kutueleza. Je, wewe umewahi barikiwa na Mungu wa bahati wakati wa kucheza kanari? Je aligeuza kete na kufanya upande wenye rangi nyekundu kuwa juu na kujaza mifuko yako na kumpa hasara mchezesha kamari? Au aliruhusu rangi ya bluu kuwa juu na kufanya mchezeshaji kuchukua fedha yako uliyoitolea jasho?"

Yule kijana akacheka kama wengine walivyocheka kisha akajibu.

"Naomba nikiri kuwa ilionekana Mungu wa bahati hata hajui kama nipo pale. Vipi kuhusu ninyi? Mmewahi mkuta akiwasubiri na akigeuza kete Ili mshinde? Tuna shauku ya kujifunza."
 
"Mwanzo mzuri," hatimaye akasema Arkad. Hapa huwa tunakutana kuangalia pande zote za mada. Kutoacha kuongelea kamari itakuwa ni kudharau kitu ambacho watu wanakifanya kila siku. Kupenda kutumia fedha kidogo kwa matumaini ya kupata kiasi kikubwa."

"Hilo limenikumbusha mashindano ya farasi, tena jana tu nilikuwa huko," akasema mtu mmoja kutoka kwa wasikilizaji.
"Ikiwa Mungu wa bahati hutembelea sehemu za kamari bila shaka atakuwa anatembelea na mashindano farasi. Kwanza farasi na magari yao huvutia zaidi. Hebu tuambie Arkad, jana Mungu wa bahati alikunong'oneza kuweka pesa zako juu ya wale farasi wa kijivu kutoka Ninawi? Nilisimama nyuma yako na sikuamini masikio yangu niliposikia ukiweka pesa zako kwa wale farasi. Sote tunaelewa kuwa farasi kutoka Ashuru hawawezi kuwashinda farasi wetu mashindanoni.

" Je, ni Mungu alikuambia uweke fedha zako kwa wale farasi wa Ninawi, maana mwishoni kabisa farasi weusi walijikwaa na kuzuia farasi wetu kusonga na kufanya wale wa Ninawi washinde?"

Arkad akatabasamu baada ya kusikia maneno yale. "Tuna sababu gani ya kufikiria kuwa Miungu inatilia maanani watu wanaocheza kamari za farasi? Mi najua Ashtar ni Mungu wa upendo ambaye anafurahi kusaidia wale wenye uhitaji na kuwabariki wanaostahili. Hapatikani kwenye meza za kamari wala kwenye mashindano ya farasi, sehemu ambazo watu hupoteza pesa nyingi kuliko wanazopata. Bali yeye hupatikana sehemu ambazo watu wanafanya mambo ya maana na wanastahili baraka.
"Kwenye kilimo, kwenye biashara halali na kwenye kazi zote ambazo binadamu hufanya kujipatia kipato. Pengine siyo mara zote mtu atapata kwa sababu mara nyingine mipango yake inaweza kuwa mibaya na nyakati nyingine hali hubadilika na kuwa mbaya. Lakini, akimlilia atafanikiwa hiyo ni kwa sababu uwezekano wa kufanikiwa huwa ni mkubwa.

"Lakini, mtu anapocheza kamari, hali inakuwa ni kinyume chake. Uwezekano wa yeye kushinda ni mdogo kuliko ule wa mchezesha kamari. Mchezo unakuwa umepangwa kumpendelea mchezeshaji. Ni biashara ya mchezesha kamari kutengeneza faida kutoka kwa wachezaji. Ni wacheza kamari wachache hutambua jinsi mchezo unavyompendelea mchezeshaji huku ukiwa dhidi yao.

"Chukulia mfano wa wanaocheza kamari za mezani. Kila mara kete ikirushwa anasema ni upande upi utakuwa juu. Kama ni mwekundu basi mchezesha kamari atamlipa mara nne ya kiasi alichoweka. Lakini kama ni pande nyingine kati ya pande zake tano ikaja juu basi atapoteza pesa zake. Hesabu inaonyesha kuwa, kila kete inaporushwa kuna uwezekano wa mara tano wa kupoteza pesa zetu zaidi ya uwezekano wa kushinda.

"Lakini kwa sababu rangi nyekundu inalipa mara nne basi tuna uwezekano wa kushinda mara nne. Kwa hiyo, kila siku mchezesha kamari anatarajia kuingiza moja ya tano ya pesa zote zilizochezwa.
"Je, mtu anaweza kutarajia kushinda mara nyingi ikiwa mchezo umepangwa ili apoteze moja katika kila michezo mitano?

"Lakini watu huwa wanashinda pesa nyingi," akasema msikilizaji mmoja.

"Ni kweli," akasema Arkad. "Lakini bado najiuliza kuwa pesa zinazopatikana kwa namna hiyo zinaweza leta mafanikio ya kudumu? Nina rafiki wengi ambao ni matajiri sana hapa Babiloni lakini hamna hata mmoja wao aliyepata utajiri wake kupitia kamari. "
"Nyinyi mliokusanyika hapa mnajua watu wengi zaidi. Ningependa kujua ni watu wangapi wamepata mafanikio kupitia kamari? Kila mmoja aseme anaowajua."

Baada ya kimya kirefu mtu mmoja mjanjamjanja akasema, 'swali lako linahusisha wachezesha kamari?"

"Kama hamna mnayemfahamu, vipi kuhusu ninyi, kuna mtu hapa huwa anashinda mara kwa mara kiasi kwamba anaweza kusema kuwa chanzo chake cha mapato ni kamari?"

Swali lake lilijibiwa kwa miguno na vicheko.
"Inaonekana hatuendi kutafuta bahati sehemu ambazo Mungu wa bahati hutembelea," akaendelea Arkad.
"Hebu na tuone maeneo mengine. Bahati haipo kwenye kuokota pochi. Haipo kwenye meza za kamari wala kwenye mashindano ya farasi. Kwenye mashindano ya farasi nakiri kupoteza pesa nyingi kuliko nilizowahi shinda.

"Sasa tuangalie kazi na biashara zetu. Je, si kawaida kuwa tukifabya biashara au kazi na kupata faida hatuoni kuwa ni bahati bali huona kuwa ni matokea ya jitihada zetu? Nafikiri inawezekana hatuoni baraka za Ashtar. Inawezekana anatusaidia lakini hatuthamini baraka zake. Ninyi hili mnalionaje?"

Hapo alisimama mfanyabiashara mmoja mzee na kuweka vazi lake sawa na kusema."Kwa ruhusa yako mheshimiwa na rafiki yangu Arkad, naomba kutoa mchango wangu. Kama umesema mafanikio yetu yanatokana na jitihada zetu, vipi kuhusu mafanikio tuliyoshindwa kuyafikia? Yale ambayo iwapo tungeyafikia tungepata faida kubwa. Si ingekuwa ni mfano mzuri wa bahati iwapo tungeyafikia? Kwa sababu hatukuyafikia hatuwezi kusema ni baraka tulizostahili. Watu wengi hapa wametokewa na jambo kama hilo.

"Tuliangalie hilo kwa mtazamo ufuatao," akasema Arkad. "Nani kati yenu alikuwa karibu kabisa kupata bahati lakini ikamponyoka?"
 
Hakika Kuna Elimu kubwa ndani yake.
IMG_20210409_084318.jpg
 
Mikono mingi ilinyooshwa, na wa yule mfanyabiashara mzee ukiwemo. Arkad akamuonyeshea ishara kuwa aongee. "Kwa sababu wewe ndiye umetoa wazo, tungependa kusikia kutoka kwako."

"Nitafurahi kuwasimulia hilo," akasema Arkad.
"Nitawasimulia hadithi inayoonyesha ni jinsi gani bahati inaweza mkimbia mtu na jinsi anavyoweza kuiacha iondoke bila kujua na kuishia kupata hasara au majuto."

"Miaka mingi iliyopita nilipokuwa kijana. Nilipokuwa nimetoka tu kuanza kazi na kuoa, baba yangu alinifuata na kunisihi sana kuhusu kuanza kuwekeza. Mtoto wa mmoja wa rafiki zake alikuwa ameona eneo moja kame nje ya kuta za mji. Lilikuwa lipo sehemu ya muinuko kutoka kwenye mfereji wa umwagiliaji hivyo maji hayakuweza kufika.

"Kijana yule aliandaa mpango wa kununua lile eneo na alitarajia kujenga mashine ya kupandisha maji iliyoendeshwa kwa ng'ombe. Akikamilisha hilo, alipanga kuligawa kwenye vishamba vidogovidogo na kuwauzia wakazi wa jiji kwaajili ya kulima bustani.

"Lakini kijana yule hakuwa na pesa za kutosha kufanya yote haya. Kama mimi tu, alikuwa ni kijana mwenye kipato cha kawaida. Baba yake alikuwa na familia kubwa na kipato cha kawaida kama baba yangu tu. Kwa hiyo aliamua kutafuta watu ambao wako tayari kushirikiana naye kwenye huo mradi. Walitakiwa watu kumi na mbili wenye kipato. Kila mmoja alitakiwa kuchangia moja ya kumi ya kipato chake mpaka pale eneo litakapokuwa tayari kwa kuuzwa. Baada ya kuuza kila mmoja atapata faida kulingana na alichowekeza.

'kijana wangu,' aliniambia baba yangu. 'ningependa uanze kuwekeza ungali bado kijana ili hapo baadaye uje kuwa mtu wa maana. Napenda kuona ukifaidika kwa kujifunza kutokana na makosa ya baba yako.'

'''Natamani sana kufanya hivyo baba yangu,' nikajibu.
'''Vema, nashauri ufanye kile nilichopaswa kufanya nilipokuwa na umri kama wako. Kwenye pato lako hakikisha moja ya kumi unawekeza kwenye mradi. Kwa kipato utakachopata kutokana na uwekezaji huo, utakuwa tajiri mkubwa kabla hata ya kufika umri kama wangu.

'''Hayo ni maneno ya hekima sana baba yangu. Natamani sana kuwa tajiri lakini kipato changu kina matumizi mengi. Sitaweza kufanya kama ulivyoshauri ila mimi bado ni kijana, muda bado upo.
'''Hata mimi nilipokuwa na umri kama wako nilifikiri hivyo lakini sasa miaka mingi imepita na sijafanya chochote.'

'''Nyakati zimebadilika mzee wangu, nitajitahidi kuepuka makosa yako.'
''' Mwanangu, fursa ipo mbele yako. Inakupa nafasi ya kuweza kuwa tajiri. Nakuomba usikawie kuitumia. Kesho nenda kamuone kijana wa rafiki yangu na kubaliana naye kuwekeza asilimia kumi ya pato lako kwenye mradi. Nenda kesho bila kuchelewa. Fursa haimsubiri mtu yeyote. Siku zinasonga haraka, usichelewe.

"Pamoja na ushauri mzuri wa baba yangu lakini sikuweza kuufuata. Kulikuwa na mavazi mazuri yaliyoletwa na wafanyabiashara kutoka mashariki. Zilikuwa nguo nzuri sana kwa hiyo nikanunua yangu na ya mke wangu.

"Ningetumia asilimia kumi ya pato langu kuwekeza kwenye ule mradi ningekosa vitu hivi vizuri na vingine vingi. Nilichelewa kufanya maamuzi hadi muda ukapita. Najutia sana jambo hili.

"Mradi ule ulikuja kuleta faida kuliko tulivyofikiria. Hiyo ni hadithi yangu ya jinsi nilivyoacha bahati ipite."

"Kwenye simulizi hii tumeona jinsi bahati inavyomfuata mtu ambaye anatumia fursa," alisema mtu mmoja mweusimweusi kutoka maeneo ya jangwani.
"Ili kujenga utajiri lazima kuwe na mwanzo. Mwanzo unaweza kuwa vipande vichache tu vya dhahabu au fedha ambavyo mtu anatoa toka kwenye pato lake na kuwekeza. Mimi mwenyewe ninamiliki mifugo mingi. Nilianza ufugaji nikiwa mvulana tu. Nilinunua ndama mmoja kwa kipande kimoja cha fedha. Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa utajiri wangu na ninauthamini sana.

"Kuanza hatua za kwanza za kujenga utajiri ndiyo bahati yenyewe. Hatua hiyo ndiyo huwabadili watu kutoka wale wanaotegemea kipato kutokana na kazi zao kuwa wale wanaopata kipato kutokana na uwekezaji wao.
Wengine kwa bahati nzuri huwekeza wangali bado vijana. Hawa huwaacha mbali wale wanaowekeza umri ukiwa umeenda au wale wasiowekeza kabisa kama baba wa huyu mfanyabiashara.

" Kama rafiki yetu mfanyabiashara angeanza kuwekeza angali kijana pale alipopata fursa leo angebarikiwa kwa utajiri mkubwa sana. Kama rafiki yetu mshona nguo naye akichukua hatua muda huu, utakuwa mwanzo wa mafaniko makubwa sana."

"Asanteni! Nami ningependa kusema." Akasema mtu mmoja kutoka nchi ya mbali. " Mimi ni msiria. Siongei vizuri lugha yenu. Napenda kumbatiza huyu mfanyabiashara jina. Pengine mtaona si vema lakini ningependa nimpe jina.
Sijui kwa lugha yenu mnamuitaje huyu mtu, nikimuita kwa kisiria hamtaelewa. Naomba mniambie, mnamuitaje mtu ambaye kila mara anachelewa na kusita kufanya mambo ambayo yanaweza kuwa na faida kwake?"
"Mhairishaji," ilijibu sauti moja.

"Huyo huyo," alisema muashuru kwa furaha.

"Akiona fursa haitumii, anasema, sasa nina mambo mengi, kwaheri tutaongea baadaye. Fursa hawezi kusubiri mtu goigoi hivyo. Anajua kuwa mtu anayetafuta bahati lazima atachangamkia fursa. Mtu yeyote ambaye hatumii fursa haraka mhairishaji mkubwa kama huyu rafiki yetu mfanyabiashara.

Yule mfanyabishara alisimama na kutoa ishara ya kuinamisha kichwa baada ya watu kulipuka kwa kicheko." Heshima yangu kwa mgeni wetu msiria ambaye hajasita kuongea ukweli'

"Sasa hebu tusikilize simulizi nyingine juu ta fursa iliyopotea. Nani ana simulizi nyingine?" Akauliza Arkad.
 
"Kama alivyokuwa amesema Algamishi, wafoenike walimtapeli Azmur. Walimuuzia vioo vilivyoonekana kama vito. Lakini kama Algamish alivyonihimiza, nikaanza kutunza tena kila sehemu ya kumi ya pato langu. Kwa vile nilikuwa nimeshazoea, haikuwa kazi ngumu.

"Baada ya miezi 12 Algamish alirudi tena, alinitafuta na kuniuliza, 'umefikia wapi toka tulipoonana?'
'''Nimejilipa kwa uaminifu', nilijibu, 'akiba yangu nimempatia Agger mtengeneza ngao, alienda kununua shaba na kila baada ya miezi minne ananilipa.
'''Vyema sana. Na hiyo pesa anayokulipa umeifanyia nini?'

'''Nimefanya karamu kubwa ikiwa na asali, divai na keki zenye viungo. Pia nimenunua kanzu ya rangi nyekundu-angavu na nina mpango wa kununua punda wa kutembelea.'

"Aliposikia hivyo Algamish alicheka, kisha akasema 'unakula watoto wa akiba yako. Sasa unategemea watakufanyiaje kazi? Na watawezaje kuwa na watoto ambao watatakiwa kukufanyia kazi?

Tengeneza kwanza jeshi la watumwa wa dhahabu na utafurahia karamu nyingi bila wasiwasi?
Baada ya kusema hayo aliondoka tena.
"Sikumuona tena kwa miaka miwili. Aliporudi alikuwa amezeeka sana, akaniambia, 'Arkad, umefanikiwa kupata utajiri ulioutaka?' "Sijafanikiwa lengo bado lakini nilicho nacho kinazalisha na kilichozalishwa nacho kinazalisha," nilijibu

'''Bado unachukua ushauri kutoka kwa wafyatua matofali?'
'''Labda kuhusu matofali, hapo wanatoa ushauri mzuri sana,' nikajibu.

'''Umejifunza somo hili vizuri sana Arkad. Kwanza ulijifunza kuishi chini ya kipato chako. Kisha ukajifunza kupata ushauri kwa wale wenye uzoefu na mwisho umejifunza kufanya fedha ikufanyie kazi.

'''Umejifunza jinsi ya kupata pesa, jinsi ya kuitunza na jinsi ya kuitumia. Sasa upo tayari kwa majukumu makubwa zaidi. Mimi sasa nimekuwa mzee na wana wangu wanafikiria kutumia pesa tu, hawawazi namna ya kujiongezea kipato. Miradi yangu ni mingi na nina wasiwasi sitaweza kuisimamia vizuri. Kama utaweza kwenda Nippur na kusimamia miradi yangu nitakufanya kuwa mshirika wangu na utakuwa na hisa kwenye mali zangu.'

"Kwahiyo nikaenda Nippur na kusimamia mali zake, alikuwa na mali nyingi sana. Kwa sababu nilikuwa ni mtu mwenye malengo na sasa nilikuwa nimejifunza zile sheria tatu za jinsi ya kusimamia utajiri niliweza kukuza sana mali zake.

Nilitajirika sana. Algamish alipokufa nilibaki na hisa zangu kwenye mali ile kama alivyoandaa kwenye mkataba." Hayo ndiyo aliyozungumza Arkad.
Sijaelewa kidogo hapo anaposema inatakiwa ujilipe 10% ya mapato yako. Je ansmaanisha ndani ya hiyohiyo 10% ndio uweze kumudu matumizi ya kila siku? Na nyingine uwekeze izalishe ndani ya hiyohiyo 10%?. Na vipi kuhusu 90% inayobaki?. Mlioelewa tafadhali mtueleweshe sisi wa Std 4.
 
"Mimi nina kisa kimoja," akasema mtu mmoja wa umri wa kati aliyekuwa amevaa vazi jekundu." Mimi nafanya biashara ya wanyama, hasa hasa ngamia na farasi na mara chache kondoo na mbuzi. Hadithi yangu itaonyesha jinsi ambavyo fursa hutokea bila kutegemewa. Pengine ndiyo maana niliacha ipite, mtajionea wenyewe.

"Siku moja jioni nilirudi jijini kutoka kwenye safari ya siku kumi ya kutafuta ngamia, safari ambayo sikupata ngamia wowote. Nilipofika Babiloni nilikasirika kukuta milango ya jiji imefungwa. Ikatubidi kulala nje ya jiji. Hatukuwa na maji wala chakula cha kutosha. Watumwa wangu walipokuwa wanatengeneza mahema kwaajili ya kulala nilifuatwa na mfugaji mmoja mzee. Naye pia alikuwa amechelewa na kukuta milango ya jiji imefungwa.

"'Mheshimiwa,' alianza kunisemesha. "'Kwa muonekano wako unaonekana kama ni mfanyabiashara. Kama ndivyo ningependa nikuuzie kondoo niliokuja nao, ni kondoo bora kabisa. Mke wangu yupo kitandani kwa kuumwa, ninatakiwa kurudi nyumbani haraka. Nunua kondoo wangu ili mimi na watumwa wangu turudi bila kuchelewa."

"Ilikuwa ni giza sana kiasi ambacho sikuweza kuona kondoo wake lakini kutokana na milio wao nilitambua kuwa walikuwa wengi sana. Baada ya kuhangaika siku kumi na kukosa ngamia nilifurahi kufanya naye biashara. Kwa sababu ya kuwa na haraka alinitajia biei nzuri sana. Nikakubali nikitarajia asubuhi tutawaingiza kondoo jijini na kuwauza kwa faida kubwa.

"Tukakubaliana kisha nikawaita watumwa wangu walete taa ili tuwahesabu wale kondoo. Yule mfugaji alisema ana kondoo mia tisa. Nisiwachoshe na maelezo ya jinsi ilivyo vigumu kuhesabu kundi kubwa la kondoo wenye njaa na kiu gizani. Lilikuwa zoezi gumu sana. Nikamwambia yule mfugaji kuwa nitawahesabu asubuhi kukicha na nitamlipa wakati huo.

'''Tafadhali mheshimiwa,' aliniomba. 'basi nilipe theluthi mbili ya pesa leo usiku ili niende zangu. Nitamuacha watumwa wangu wenye uelewa ili akusaidie kuhesabu ifikapo asubuhi. Yeye ni miaminifu na utampatia pesa iliyobaki.

"Nilikuwa mjeuri na nilikataa kulipa usiku ule. Asubuhi ilipofika, kabla sijaamka milango ya jiji ilifunguliwa na wanunuzi wanne walitoka wakitafuta kondoo. Walikuwa na mchecheto wa kununua, tena kwa bei kubwa sababu kulikuwa na uwezekano wa jiji kuzingirwa hivyo kulikuwa na uhaba wa chakula. Walinunua kondoo wale kwa bei mara tatu zaidi ya ile niliyoambiwa jana usiku. Hivyo ndivyo nilivoruhusu bahati adimu iniponyoke."

"Hiki ni kisa cha tofauti sana," akasema Arkad. "Kinatufundisha nini?"

"Kinatufundisha kuchukua hatua haraka iwapo tumeona biashara ni nzuri na haina tatizo," alisema mtu mmoja wa makamo ambaye kazi yake ilikuwa ni kutengeneza matandiko ya wanyama.

"Asanteni sana! Ningependa kuongea tena" akasema msiria akiwa amekwishasimama. "Hizi hadithi zinafanana. Katika zote, fursa ilipotea kwa njia ileile.

Kila mara fursa inawafuata wahairishaji ikiwa na mpango mzuri. Lakini mara zote wanasita, hawajiambii huu ndiyo muda muafaka nifanye haraka! Mtu unawezaje kufanikiwa kwa mwendo kama huo?"

"Maneno ya busara sana rafiki yangu" akasema mfanyabiashara ya mifugo. " Kwenye simulizi zote, bahati ilipotea kwa sababuan ya kusitasita na kuhairisha mambo. Tunatamani kuwa matajiri lakini mara zote fursa zinapotokea roho ya kuahirisha na kusitasita inatuambia ngoja kwanza. Kwa kuisikiliza tunakuwa maadui wetu wenyewe, tena adui mbaya.

"Wakati ningali kijana sikulijua hili kwa namna aliyoongelea rafiki yetu msiria. Mwanzo nilifikiri kwamba maamuzi yangu mabaya ndiyo yalisababisha nikose fursa nyingi zenye faida. Baadaye nikafikiri ni sababu ya ujeuri wangu. Mwisho ndipo nikagundua ni kitu gani-Tabia ya kusitasita na kuhairisha badala ya kutenda, kutenda kwa haraka na kwa akili. Baada ya kuijua nimeichukia sana. Kwa hasira za punda wa porini aliyefungwa kwenye gari la farasi nilijichomomoa kutoka kwa huyo adui wa mafanikio yangu."
"Asante! Ningependa kumuuliza mfanyabiashara swali," alisema msiria.

"Wewe unavaa mavazi bora, si kama wavaavyo maskini. Na hata ongea yako ni kama ya mtu aliyefanikiwa. Hebu tuambie, hadi sasa bado unaisikia sauti ya kuhairisha mambo ikikunong'oneza masikioni?"

"Kama tu rafiki yetu mfanyabiashara ya mifugo, mimi pia ilinibidi kuishinda tabia ya kuahirisha mambo" alisema mfanyabiashara. "Kwangu ilikuwa ni adui ambaye alitazama mafanikio yangu ili ayayeyushe. Kisa nilichosimulia ni kimoja tu ila vipo vingi vinavyoonyesha jinsi nilivyopoteza fursa. Ukiijua tabia hii ni rahisi kuishinda. Hakuna mtu anaweza kumruhusu mwizi aibe ghala yake ya nafaka kwa hiari. Wala hakuna mtu anaweza ruhusu adui akimbize wateja wake na faida yake kwa hiari.

Nilipogundua kuwa adui yangu anafanya matendo kama hayo nilidhamiria kumshinda. Hivyo, kila mtu anapaswa kuishinda roho ya kusitasita na kuahirisha mambo kabla hajatarajia kushiriki utajiri wa Babiloni.


Mungu wa bahati huwapendelea watu wa vitendo.

Mwisho wa sura ya nne.
 
Sijaelewa kidogo hapo anaposema inatakiwa ujilipe 10% ya mapato yako. Je ansmaanisha ndani ya hiyohiyo 10% ndio uweze kumudu matumizi ya kila siku? Na nyingine uwekeze izalishe ndani ya hiyohiyo 10%?. Na vipi kuhusu 90% inayobaki?. Mlioelewa tafadhali mtueleweshe sisi wa Std 4.
Kwa jinsi nilivyo elewa hio 10% unayojilipa ni kama Mbegu na 90% hio ni kwaajili ya kulipa bili mbalimbali
 
Watu kama nyinyi Red Giant mnabarikiwa sana. Hiki kitabu nilikipakua huku mwaka jana nikapitia tu list of content nikaacha leo nimekisoma kupitia kwako.

Nasema mnabarikiwa kwasababu kama mimi nashindwa tu kujisomea, je kweli ningeweza kusoma na kutafsiri niandike kwa ajili ya watu?

Shukrani. Big up
 
SHERIA TANO ZA PESA


"Ukiambiwa uchague kati ya mfuko uliojaa dhahabu na mabamba ya vigae yaliyoandikwa maneno ya hekima na busara, utachagua nini?"

Wasikilizaji walikuwa wamekaa jangwani wakiwa wamekusanyika kuzunguka moto. Walikuwa wakisikiliza kwa makini. Mwanga wa moto ulionyesha nyuso zao ambazo zilianza kuwa nyeusi sababu ya jua la jangwani.

"Dhahabu, dhahabu," walijibu wote ishirini na saba kwa pamoja.

Mzee Kalabab alitabasamu kama vile kuna siri anaifahamu yeye peke yake.
"Sikilizeni niwaambie," alisema huku akiinua mikono kuwanyamazisha. "Sikilizeni mbwa mwitu wanavyolia kwa kunung'unika sababu ya njaa. Ukisema uwapatie chakula ni nini kitatokea? Wataishia kupigana na wakisha kula wataishia kupigana na kuzurura wala hawatafikiria kesho yao itakuwaje.

Hivyo ndivyo walivyo binadamu. Waambie wachague kati ya hekima na dhahabu nao watafanya nini? Wataidharau hekima na kutapanya dhahabu. Kesho yake wanaanza kunung'unika sababu hawana dhahabu.
"Pesa ipo kwaajili ya wale wanaojua sheria zake na kuzifuata."
Kalabab akatengeneza kanzu yake na kujifunika hadi miguuni sababu upepo wa baridi wa usiku ulikuwa umeanza kuvuma, kisha akaendelea. "Mmekuwa waaminifu sana kwangu na katika safari yetu yote mmetunza vizuri ngamia wangu. Mmefanya kazi kwenye joto kali la jangwani bila malalamiko. Mmepambana kishujaa na vikundi vya waporaji waliotaka kupora mali yangu. Kwa sababu ya hayo nitawasimulia kisa kihusucho sheria tano zinazoongoza pesa. Sijawahi msimulia mtu yeyote kisa hiki.

"Nisikilizeni kwa makini sana mambo nitakayowaeleza, iwapo mtayaelewa vizuri na kuyafanyia kazi mtakuja kuwa matajiri wakubwa."

"Kalabab mpaka sasa umetusimulia visa vingi sana," aliongea msimamizi wa wa upakiaji. "Tunategemea hekima yako na busara zako zituongoze huko tuendako baada ya kesho kumaliza utumishi kwako."

"Mambo yote niliyokuwa nawasimulia yalikuwa ni visa vilivyonitokea katika safari zangu za mbali. Lakini leo nitawasimulia kuhusu hekima ya Arkad, mtu mwenye busara na tajiri mkubwa.

"Tumemsika sana huyo bwana," alisema kiingozi wa upakiaji. "Inasemwa kuwa ndiye mtu tajiri zaidi kuwahi kuishi Babiloni,"
"Alikuwa tajiri mkubwa kwa sababu alikuwa anajua jinsi ya kushughulika na pesa. Alikuwa na ujuzi mkubwa wa pesa kuliko mtu yeyote aliyepata kuishi kabla yake. Leo nitawasimulia kuhusu hekima yake kama nilivyosimuliwa na kijana wake Nomasir nilipokuwa bado kijana huko Ninawi.

"Siku moja mimi na bosi wangu tulikuwa kwenye jumba la Nomasir hadi usiku mwingi. Nilikuwa namsaidia bosi wangu kupeleka mazuria ili Nomasir ayakague na kuyajaribu kuona kama yanamfaa. Alipopata linalomfaa alitukaribisha kukaa na kunywa pamoja naye. Kilikuwa kinywaji bora na chenye harufu nzuri sana, sijawahi kunywa kinywaji kizuri namna ile.

"Tulipokuwa tunakunywa alitusimulia kisa cha baba yake, Arkad. Nitasimulia kama alivyosimulia.

'''Mwanangu, ninatamani urithi na kuendeleza utajiri wangu, lakini ni lazima kwanza uthibitishe kuwa unauwezo wa kuusimamia. Kwa hiyo ningependa uende na uonyeshe kwa vitendo iwapo una uwezo wa kupata pesa na kuwa mtu wa kuheshimika kati ya watu.

'''Kwa kuanzia nitakupatia vitu viwili ambavyo mimi mwenyewe sikuvipata nilipokuwa bado kijana maskini.
"'Kwanza nakupatia mfuko huu wa dhahabu. Iwapo utazitumia kwa busara basi ndiyo utakuwa msingi wa utajiri wako.
'''Pili nakupatia hili bamba ambalo juu yake kumeandikwa sheria tano zihusuzo pesa. Iwapo utazitumia kwa vitendo zitakuletea ufanisi na usalama.

'''Baada ya miaka kumi kutoka leo rudi hapa nyumbani na unionyeshe mambo uliyotimiza. Iwapo utathibitika kuwa unafaa nitakufanya kuwa mrithi wa mali zangu. Kinyume na hilo, nitatoa mali zangu na kuwapa makuhani, pengine zitanisaidia kuingia peponi.

"Kwa hiyo Nomasir akaondoka na kwenda kujitegemea. Akabeba pochi ya dhahabu aliyopewa na kufunga lile bamba vizuri kwenye kitambaa cha hariri. Akamchukua mtumwa wake, wakapanda farasi na kwenda zao.

"Baada ya miaka kumi kupita Nomasir alirudi kwa baba yake kama walivyokubaliana. Baba yake akamwandalia karamu kubwa sana na ndugu na marafiki wakaalikwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom