Umewahi kukutwa na hali kama hii??

LD

JF-Expert Member
Aug 19, 2010
3,014
574
Yani unaweza ukajikuta unakosa amani moyoni, ukifikiria ulicho kifanya hukioni!!! Lakini moyo umeinama, huna furaha, yani hujachangamka kwa ujumla.

Lakini ukiangalia umekosea wapi huoni, ukijiuliza sasa kwa nini unakuwa hivi hupatati jibu. Unaweza ukatamani hata kukaa tu mahali peke yako.....hutaki kuongea ongea ingawa wewe ni muongeaji sana. Yani dah unakuwa upo upo tu.......

Hebu nambieni hali kama hii imewahi kukupata, kama ndiyo unafanya nini ili iondoke.
 
Amani ya roho na moyo huletwa kwa kusali na kusubiri. Jaribu hilo.
 
Nitakuletea cd ya Mchungaji Mwakasege!

Kwa ufupi ukiona hali hiyo inakutokea, si ya kubahatisha hata kidogo...Ni mzigo wa maombi unakuwa unakukabili, lakini kwa akili za kawaida huwezi elewa..

Kwa habari ya rohoni, upatapo hali kama hiyo maana yake ni amri kuwa kimbia uingie kwa magoti uanze kuomba haraka sana, maana kuna jambo Mungu anataka kukuonyesha , au kukuonya , au kukuelekeza.

Kama ni msomaji wa bible, Yesu akikaribia kukamatwa na wayahudi aliwaambia wanafunzi wake,,"Nina huzuni kiasi cha kufa"...lakini hakupata kueleza ni huzuni ya namna gani...Lakini pia bible inaeleza juu ya 'kuugua rohoni isivyomithilika"..

Ni hali inayoweza kumpata mtu yeyote, lakini amini usiamini ina sababu zake kwa ulimwengu wa roho!
 
Yani unaweza ukajikuta unakosa amani moyoni, ukifikiria ulicho kifanya hukioni!!! Lakini moyo umeinama, huna furaha, yani hujachangamka kwa ujumla.

Lakini ukiangalia umekosea wapi huoni, ukijiuliza sasa kwa nini unakuwa hivi hupatati jibu. Unaweza ukatamani hata kukaa tu mahali peke yako.....hutaki kuongea ongea ingawa wewe ni muongeaji sana. Yani dah unakuwa upo upo tu.......

Hebu nambieni hali kama hii imewahi kukupata, kama ndiyo unafanya nini ili iondoke.

Ni kitu cha kawaida. Kila mtu kuna muda unahitaji uwe peke yako.
Jaribu kubadili mazingira -Have a change of scene. Take a walk ukutane na vitu vipya au watu wapya kabisa. Pia jishughulishe na mazoezi ya mwili. Imba nyimbo kwa nguvu na sauti kubwa, and remember to "confer to your God".
 
LD hiyo hali huwa inamtokea binadamu yoyote wakati fulani.Lakini haya yanaweza kusaidia kuvuka hapo

* To be very honest and look within yourself what kind of solitude is that suffering and what circumstances they should.
* Losing the fear to look within ourselves, and face the need to know how we are: our hopes and ambitions, limitations and fears, in addition to honestly assess the self-image.
* Take the initiative to develop new relationships, you can determine who interest us, and then develop a strategy to contact them.
* Consider that there is nothing to lose and that fear of rejection is a deterrent to making new friends or lovers.
* To put off the attitude of the victim, for although the world is sometimes cruel, materialistic, sure there are people who want to meet someone like us.
* Avoid closed in yourself when you have strong feeling of loneliness, which can cause more damage. It is better to have nobody to talk to whom and intimate love.
* Thinking we're not as rare as we think, to check that there is more depth and confidence to talk to someone. We have the ability to "fill" to more people than we think, and we may be enticing many people who have very close.
* Initiate or resume any sport or artistic activity also often helps to improve mood, in addition to providing the atmosphere between people who have similar hobbies.

The feeling of loneliness is a situation that could become temporary and that is not necessarily bad, since it is possible to transform it into a space for reflection to know thoroughly and sincerely find our own identity.
 
Nitakuletea cd ya Mchungaji Mwakasege!

Kwa ufupi ukiona hali hiyo inakutokea, si ya kubahatisha hata kidogo...Ni mzigo wa maombi unakuwa unakukabili, lakini kwa akili za kawaida huwezi elewa..

Kwa habari ya rohoni, upatapo hali kama hiyo maana yake ni amri kuwa kimbia uingie kwa mgoti uanze kuomba haraka sana, maana kuna jambo Mungu anataka kukuonyesha , au kukuonya , au kukuelekeza.

Kama ni msomaji wa bible, Yesu akikaribia kukamatwa na wayahudi aliwaambia wanafunzi wake,,"Nina huzuni kiasi cha kufa"...lakini hakupata kueleza ni huzuni ya namna gani...Lakini pia bible inaeleza juu ya 'kuugua rohoni isivyomithilika"..

Ni hali inayoweza kumpata mtu yeyote, lakini amini usiamini ina sababu zake kwa ulimwengu wa roho!

Asante sana PJ, umenikumbusha hili somo, hebu ngoja niingie chumba cha ndani haraka!!
Jaribu ni mtaji wa kuongeza Imani..........
 
LD my dear pole kama yamekutokea
Mie yalikuwa yananitokeaga sana
Na tiba yake mi nikawa na chukua gin an tonic
Usema ukweli nilijiingiza kwenye matatizo zaidi..
Naelewa kwamba ni tatizo kubwa sana kumweleza mtu
Lakini kutafuta msaada mapema na kuongea na mtu
unaye mwamini ..
Pole sana dear kama uko kwenye hiyo situation..
 
LD my dear pole kama yamekutokea
Mie yalikuwa yananitokeaga sana
Na tiba yake mi nikawa na chukua gin an tonic
Usema ukweli nilijiingiza kwenye matatizo zaidi..
Naelewa kwamba ni tatizo kubwa sana kumweleza mtu
Lakini kutafuta msaada mapema na kuongea na mtu
unaye mwamini ..
Pole sana dear kama uko kwenye hiyo situation..

Dah!! Asante AD
Naomba nikuulize kidogo, wewe ulikuwa unajisikia sikia je yani. Manake kuna ile unakosa amani lakini ukifikiria unaona labda kuna kitu unakifikiria sana...au kuna kitu unakihitaji kama pesa lakini hauna kwa wakati huo!!! Sasa hii ya unajikuta tu upo hivo inasababishwa na nini??
 
LD my dear pole kama yamekutokea
Mie yalikuwa yananitokeaga sana
Na tiba yake mi nikawa na chukua gin an tonic
Usema ukweli nilijiingiza kwenye matatizo zaidi..
Naelewa kwamba ni tatizo kubwa sana kumweleza mtu
Lakini kutafuta msaada mapema na kuongea na mtu
unaye mwamini ..
Pole sana dear kama uko kwenye hiyo situation..

Dah!!! Itabidi niache LONG ISLAND ICE TEA
 
Ni hali ambayo huwa inatokea PJ amezungumzia vizuri, ni vizuri zaidi kama utamshirikisha Mungu kwa maombi na sala inawezekana kuna kitu fulani kinataka kutokea au jambo fulani basi ni vizuri kujiweka mbele ya Mungu kwa maombi zaidi
 
Hiyo hali kutokea sana pole sana dada Muombe Mungu akusaidie uondokane na hiyo hali.

Mungu ni mwema na yupo kwa ajili ya wote atakusaidia. "sikuja kuwaita watu wema bali wenye dhambi ili wapate kutubu" na Wenye afya hawamuhitaji daktari, bali wanaomwitaji ni wale wagonjwa"

Kila la heri
 
Yani unaweza ukajikuta unakosa amani moyoni, ukifikiria ulicho kifanya hukioni!!! Lakini moyo umeinama, huna furaha, yani hujachangamka kwa ujumla.

Lakini ukiangalia umekosea wapi huoni, ukijiuliza sasa kwa nini unakuwa hivi hupatati jibu. Unaweza ukatamani hata kukaa tu mahali peke yako.....hutaki kuongea ongea ingawa wewe ni muongeaji sana. Yani dah unakuwa upo upo tu.......

Hebu nambieni hali kama hii imewahi kukupata, kama ndiyo unafanya nini ili iondoke.

Mi huwa inanipata na kuwa kama nimegutushwa na kujiuliza mimi ni nani na kujisiskia moyo unawasiwasi, but huwa inalast within 2-5 minutes, mimi ikinipata huwa nasema maneno machache tu "Mungu naomba amani" basi within muda mfupi narudi normal. Kwa sababu huwa ni hali ambayo haidumu na haitokei mara kwa mara huwa sijawahi kudhani kama ni tatizo.
 
pole sana LD.
ukipatwa na hali hiyo kama ni mtu usiemwamini mungu wanasema utapata habari mbaya sana ndo mana inaanza kukutesa mapema.
ila kwa upande wa waliokombolewa basi kusali na kukaribia uwepo wa mungu,sikiliza kwaya au imba nyimbo za kuabudu mda mrefu sana ikiwezekana zikupitie na usingizi.

mimi hali hii ishawahi ntokea lakini niligundua shida ilikua ni msongo wa mawazo.nilikua na mipango mikubwa mingi na kila nikiangalia njia za kutimiza zinaniumiza kichwa. na kila ukijiuliza hupati jibu na unakua hujielewi elewi.
kwa upande wangu nilisikiliza nyimbo sana za kutia moyo na kufariji na kuamsha akili upya.(pia fanya mazoezi na kunywa maji kwa wingi)
 
Dah, LD hata mimi huwa inanitokea hiyo hali na sa zingine hadi machozi yananitoka na ikitokea nimekumbuka tukio baya naweza nikalia kabisa.
Mara nyingi hutokea hivyo ninapokuwa mwenyewe kwahiyo nikihisi kupooza pooza natafuta watu wa kuongea nao au hata simu nipige ilimradi nisihisi upweke.
 
Pole sana LD hiyo hali ilishawahi nitokea na mimi kipindi fulani nimuuliza mtu mkubwa aliekuwa jirani na mimi akaniambia inatokana na kuwaza sana halafu vitu vyenyewe unavyowaza haujui ufumbuzi wake mfano unawaza kupata pesa lakini hujui utapataje kwa kifupi unawaza vitu ambavyo haviwezekani kwa wakati huo na akaniamia solution ni kwamba ukiona unawaza kitu ambacho unajua huwezi kukipatia muafaka kwa wakati unaotaka kifukuze kabisa moyoni mwako na ndio hapo unatakiwa uingie katika maombi, mimi nilifanya hivyo na nikafanikiwa
 
Dah, LD hata mimi huwa inanitokea hiyo hali na sa zingine hadi machozi yananitoka na ikitokea nimekumbuka tukio baya naweza nikalia kabisa.
Mara nyingi hutokea hivyo ninapokuwa mwenyewe kwahiyo nikihisi kupooza pooza natafuta watu wa kuongea nao au hata simu nipige ilimradi nisihisi upweke.

Kweli Husninyo kuna wakati unatamani kulia kabisa yani, halafu naona kama najisikia kunyamaza na kufanya mambo yangu kimya kimya vile....mtu akikusemesha semesha unaona kama nini sijui.....dah
 
Pole sana LD hiyo hali ilishawahi nitokea na mimi kipindi fulani nimuuliza mtu mkubwa aliekuwa jirani na mimi akaniambia inatokana na kuwaza sana halafu vitu vyenyewe unavyowaza haujui ufumbuzi wake mfano unawaza kupata pesa lakini hujui utapataje kwa kifupi unawaza vitu ambavyo haviwezekani kwa wakati huo na akaniamia solution ni kwamba ukiona unawaza kitu ambacho unajua huwezi kukipatia muafaka kwa wakati unaotaka kifukuze kabisa moyoni mwako na ndio hapo unatakiwa uingie katika maombi, mimi nilifanya hivyo na nikafanikiwa

Asante Maty, hebu ngoja niache kuwaza kujenga ghorofa angani lol!!!
 
Back
Top Bottom