Nitakuletea cd ya Mchungaji Mwakasege!
Kwa ufupi ukiona hali hiyo inakutokea, si ya kubahatisha hata kidogo...Ni mzigo wa maombi unakuwa unakukabili, lakini kwa akili za kawaida huwezi elewa..
Kwa habari ya rohoni, upatapo hali kama hiyo maana yake ni amri kuwa kimbia uingie kwa magoti uanze kuomba haraka sana, maana kuna jambo Mungu anataka kukuonyesha , au kukuonya , au kukuelekeza.
Kama ni msomaji wa bible, Yesu akikaribia kukamatwa na wayahudi aliwaambia wanafunzi wake,,"Nina huzuni kiasi cha kufa"...lakini hakupata kueleza ni huzuni ya namna gani...Lakini pia bible inaeleza juu ya 'kuugua rohoni isivyomithilika"..
Ni hali inayoweza kumpata mtu yeyote, lakini amini usiamini ina sababu zake kwa ulimwengu wa roho!