Umewahi kujiuliza kwanini upo hapa?

Umewahi kujiuliza kwanini upo hapa?

Dunia yakoo

Senior Member
Joined
Nov 23, 2019
Posts
139
Reaction score
214
Mabadiliko mbalimbali yaliyoikumba sayari yetu yangetosha kutengeneza mabuku makubwa jiographia na historia na kutoa elimu sahihi wapi tumetoka na wapi tunaelekea.

Na juu ya yote kwanini tuko hapa tulipo hapa sasa. Kinyume chake uongo, uzushi vimekuwa muhimili wa elimu yetu ya zama zote.
 
Hata kama yakaletwa mabuku makubwa yakutandaza mita mia,bado tunaamini kuinuka kiuchumi na kuinuka huko kunaleta madhara ktk dunia yetu! Mpaka yatupate ndo tutajua nini ni nini.. tupo hapa kwasababu tupo hapa na hapa ndipo tupo panafaa tuwepo kwasababu tupo.
 
Kwa nini unaita uongo na uzushi? Wote wanajaribu kuelezea wasichokifahamu kama wewe tu, sasa iweje uwaite waongo na wazushi?
 
Mabadiliko mbalimbali yaliyoikumba sayari yetu yangetosha kutengeneza mabuku makubwa jiographia na historia na kutoa elimu sahihi wapi tumetoka na wapi tunaelekea.

Na juu ya yote kwanini tuko hapa tulipo hapa sasa. Kinyume chake uongo, uzushi vimekuwa muhimili wa elimu yetu ya zama zote.

Mimi najua kwanini niko hapa.

Vipi wewe unajua kwanini uko hapa au ushawahi kujua majibu ya maswali yako unayapataje ?

Akili salama lazima ijue ya kuwa duniani tunaishi kwa malengo na si kwa bahati mbaya,sababu hiyo bahati mbaya hakuna anae weza kuithibitisha.
 
. tupo hapa kwasababu tupo hapa na hapa ndipo tupo panafaa tuwepo kwasababu tupo.

Kwanini hii kauli umeifanya kama sababu ? Maana ya sababu ni kuelezea chanzo au kujibu swali la kwanini baada ya la kwanza kuwepo,lakini kauli yako haija kidhi sifa hiyo,sasa kwanini uipe sifa ya sababu ? Hali ya kuwa haija jibu swali husika ?
 
Kwanini hii kauli umeifanya kama sababu ? Maana ya sababu ni kuelezea chanzo au kujibu swali la kwanini baada ya la kwanza kuwepo,lakini kauli yako haija kidhi sifa hiyo,sasa kwanini uipe sifa ya sababu ? Hali ya kuwa haija jibu swali husika ?
Kwa jibu jepesi Ni kuwa sijui ila tupo hapa kwasababu tupo hapa na panafaa tuwepo kwani tupo na panakizi mahitaji yetu ya sisi kuwepo.
 
Kwa jibu jepesi Ni kuwa sijui ila tupo hapa kwasababu tupo hapa na panafaa tuwepo kwani tupo na panakizi mahitaji yetu ya sisi kuwepo.

Japo umekiri ila umerudia kile nilichokihoji hapo kabla.

Sababu umekiri hujui basi hata hiyo sababu hauko nayo yaani lazima ukosee.
 
Japo umekiri ila umerudia kile nilichokihoji hapo kabla.

Sababu umekiri hujui basi hata hiyo sababu hauko nayo yaani lazima ukosee.
He he! Umenielewa sehemu moja ila bado hujaelewa kitu kidogo Sana Soma tena.
 
He he! Umenielewa sehemu moja ila bado hujaelewa kitu kidogo Sana Soma tena.

Bila shaka utakuwa unafahamu japo kidogo Kiswahili cha waswahili,yaani wewe ni mswahili. Kauli inapingana na maana bali mjengeko wa sentensi yako kiuchambuzi,yaani "Unasadikisha kwa upande wa kwanza ila unakanusha kwa upande wa unaofata".

Ulipokiri ya kuwa hujui,basi jibu hili lilifunga na kuonyesha hiko cha mbele hutapatia,yaani hutoki katika makosa na uongo,kauli yako ni sawa sawa na mtu yule asemaye/asemae "Mimi sijui lakini kitu lakini hunidanganyi" kauli haisemi isipokuwa mjinga,sababu amekiri kwanza na akakanusha kwa kujitoa katika kauli yake mwenyewe. Kwa maana hajui na kudanganywa atadanganywa tu sababu hajui,kwahiyo kauli yako hiyo iko kama hii na hii inaishia au inakuwa kama kinogesho au kipashio tu katila mazungumzo na kuchangamsha soga ili muda uende,ila kiuhalisia haina maana yoyote.
 
Bila shaka utakuwa unafahamu japo kidogo Kiswahili cha waswahili,yaani wewe ni mswahili. Kauli inapingana na maana bali mjengeko wa sentensi yako kiuchambuzi,yaani "Unasadikisha kwa upande wa kwanza ila unakanusha kwa upande wa unaofata".

Ulipokiri ya kuwa hujui,basi jibu hili lilifunga na kuonyesha hiko cha mbele hutapatia,yaani hutoki katika makosa na uongo,kauli yako ni sawa sawa na mtu yule asemaye/asemae "Mimi sijui lakini kitu lakini hunidanganyi" kauli haisemi isipokuwa mjinga,sababu amekiri kwanza na akakanusha kwa kujitoa katika kauli yake mwenyewe. Kwa maana hajui na kudanganywa atadanganywa tu sababu hajui,kwahiyo kauli yako hiyo iko kama hii na hii inaishia au inakuwa kama kinogesho au kipashio tu katila mazungumzo na kuchangamsha soga ili muda uende,ila kiuhalisia haina maana yoyote.
ieleweke hivi tupo hapa kwasababu Kuna mazingira yanayotufanya/kutuwezesha sisi kuwepo hapa ila sijui kwanini tupo hapa kwasababu sijui lengo la alietuweka hapa au kilichotuweka hapa!

Napo haujaelewa..?
 
Mabadiliko mbalimbali yaliyoikumba sayari yetu yangetosha kutengeneza mabuku makubwa jiographia na historia na kutoa elimu sahihi wapi tumetoka na wapi tunaelekea.

Na juu ya yote kwanini tuko hapa tulipo hapa sasa. Kinyume chake uongo, uzushi vimekuwa muhimili wa elimu yetu ya zama zote.
Uongo, uzushi wa elimu ni upi?

Na ukweli je ni upi?

Na unapatikanaje?
 
ieleweke hivi tupo hapa kwasababu Kuna mazingira yanayotufanya/kutuwezesha sisi kuwepo hapa ila sijui kwanini tupo hapa kwasababu sijui lengo la alietuweka hapa au kilichotuweka hapa!

Napo haujaelewa..?

Safi kabisa,je hudhani kama chanzo cha sisi kuwepo hapa kinatakiwa kijulikane na ndio kitakuwa na majibu ya kwanini sisi tupo hapa na kwanini vilivyomo hapa duniani vina uhusiano kati ya kimoja na kingine ?
 
Back
Top Bottom