contask
JF-Expert Member
- Jan 3, 2021
- 965
- 1,972
Habari wakuu.
Leo natamani tujadili mapinduzi ya mifumo ya malipo kwenye sekta yetu ya usafiri wa umma, hasa hapa mjini ambapo kero ya chenji imekuwa ya kudumu. Kila siku tunashuhudia mabishano yasiyo na tija kati ya abiria na makondakta, jambo ambalo linaweza kuisha kabisa tukiamua kubadilisha namna tunavyolipa nauli zetu.
Chukulia mfano unaotokea kila siku, Nauli ni mia Saba, unatoa buku. Kondakta anakuuliza papo hapo "Masta, una mia mbili hapo nikupe jero?" Ukimwambia huna, anakwambia subiri mbele nitakupa. Unasafiri hadi unafika kituo chako cha kushuka, chenji huna na gari linaondoka, mwisho wa siku unaamua tu kumuachia ile mia mbili yako kwa unyonge kwa sababu ya haraka. Piga hesabu abiria ishirini wakiacha mia mbili zao kwa siku, huu unakuwa wizi wa kistaarabu kwa kisingizio cha uhaba wa chenji mtaani.
Sasa tuko kwenye karne ya uchumi wa kidijitali na sasa hivi huduma za Lipa Namba na Selcom Pay zimekuwa sehemu ya maisha yetu, kuanzia kwa mama ntilie hadi kwa wauza mshikaki.
Swali langu la msingi ni kwanini tunashindwa kuleta huu mbadala wa malipo kwenye daladala, bajaji na bodaboda? Inashindikana vipi kila chombo kuwa na sticker yake ya Lipa Namba ili abiria akipanda anahamisha nauli kamili ya mia sita au mia saba bila kuhitaji kubeba fedha taslimu?
Mbadala huu wa kidijitali una faida kubwa sana kiuchumi maana utaondoa kabisa migogoro ya chenji, na utawasaidia wamiliki wa magari kupokea mapato yao moja kwa moja kwenye akaunti zao bila usumbufu.
Zaidi ya hayo, utaratibu huu utarahisisha mzunguko wa fedha na kuokoa muda mwingi unaopotea vituoni wakati wa kuhesabu sarafu na noti zilizochakaa.
Je, kikwazo kikubwa cha sekta hii kutofanya mabadiliko ya malipo kiko wapi? Ni gharama za miamala? uvivu wa jamii kubadilika, au kuna watu wanaona mifumo hii itabana mianya yao ya kupiga hela ya juu?
Wadau na wataalamu wa mifumo ya kifedha humu ndani, hebu tushushe hoja hapa ni mbinu gani zikitumika tutafanikiwa kuachana na malipo ya mkononi kwenye usafiri wa umma.
Leo natamani tujadili mapinduzi ya mifumo ya malipo kwenye sekta yetu ya usafiri wa umma, hasa hapa mjini ambapo kero ya chenji imekuwa ya kudumu. Kila siku tunashuhudia mabishano yasiyo na tija kati ya abiria na makondakta, jambo ambalo linaweza kuisha kabisa tukiamua kubadilisha namna tunavyolipa nauli zetu.
Chukulia mfano unaotokea kila siku, Nauli ni mia Saba, unatoa buku. Kondakta anakuuliza papo hapo "Masta, una mia mbili hapo nikupe jero?" Ukimwambia huna, anakwambia subiri mbele nitakupa. Unasafiri hadi unafika kituo chako cha kushuka, chenji huna na gari linaondoka, mwisho wa siku unaamua tu kumuachia ile mia mbili yako kwa unyonge kwa sababu ya haraka. Piga hesabu abiria ishirini wakiacha mia mbili zao kwa siku, huu unakuwa wizi wa kistaarabu kwa kisingizio cha uhaba wa chenji mtaani.
Sasa tuko kwenye karne ya uchumi wa kidijitali na sasa hivi huduma za Lipa Namba na Selcom Pay zimekuwa sehemu ya maisha yetu, kuanzia kwa mama ntilie hadi kwa wauza mshikaki.
Swali langu la msingi ni kwanini tunashindwa kuleta huu mbadala wa malipo kwenye daladala, bajaji na bodaboda? Inashindikana vipi kila chombo kuwa na sticker yake ya Lipa Namba ili abiria akipanda anahamisha nauli kamili ya mia sita au mia saba bila kuhitaji kubeba fedha taslimu?
Mbadala huu wa kidijitali una faida kubwa sana kiuchumi maana utaondoa kabisa migogoro ya chenji, na utawasaidia wamiliki wa magari kupokea mapato yao moja kwa moja kwenye akaunti zao bila usumbufu.
Zaidi ya hayo, utaratibu huu utarahisisha mzunguko wa fedha na kuokoa muda mwingi unaopotea vituoni wakati wa kuhesabu sarafu na noti zilizochakaa.
Je, kikwazo kikubwa cha sekta hii kutofanya mabadiliko ya malipo kiko wapi? Ni gharama za miamala? uvivu wa jamii kubadilika, au kuna watu wanaona mifumo hii itabana mianya yao ya kupiga hela ya juu?
Wadau na wataalamu wa mifumo ya kifedha humu ndani, hebu tushushe hoja hapa ni mbinu gani zikitumika tutafanikiwa kuachana na malipo ya mkononi kwenye usafiri wa umma.