Umesoma shule ya bweni wewe?

Umesoma shule ya bweni wewe?

kakuruvi

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2009
Posts
770
Reaction score
259
Kama umesoma shule ya bweni ya serikali basi hili ni jambo la kawaida sana utazoea na kupiga shule kwa furaha. Pale Tosamaganga tulikuwa tunaita Bondo, kuna jamaa aliapa kwamba akijapata ajira atapiga marufuku ugali na maharage nyumbani kwake eti kwa kuwa tulikuwa tunakula mchana na jioni chakula hicho hicho kwa mwaka mzima.

Asikudanganye mtu kikipikwa chakula hicho kwake sasa hivi anakula!!
 

Attachments

  • bondo.jpg
    bondo.jpg
    33.7 KB · Views: 4,520
Nguna kwenye. Mustin na wale wadudu wa kwenye mbaazi na Maharage tukiita njuka, utando wa mafuta ya mboga yakiitwa ufusi
 
Mara secondary kulikuwa na watoto tunawaita busima dar umenikumbusha mbali sana na badae mazengo dodoma kulikuwa na raha yake sana.
 
Duuh maisha ya shule ni ya shule tu never compered na mahali kwingine
 
Daah umenikumbusha mbali sana Iambi Sec.School-Singida
 
Mara secondary kulikuwa na watoto tunawaita busima dar umenikumbusha mbali sana na badae mazengo dodoma kulikuwa na raha yake sana.

Pale Mazengo ilikuwa inahitaji ubaunsa kuipata hyo kitu mapema, wale watoto tulikuwa tunawaita Kikuyu!
 
nakumbia SHYCOM enzi za baba karo na mzee mwerangi....
 
Kama umesoma shule ya bweni ya serikali basi hili ni jambo la kawaida sana utazoea na kupiga shule kwa furaha. Pale Tosamaganga tulikuwa tunaita Bondo, kuna jamaa aliapa kwamba akijapata ajira atapiga marufuku ugali na maharage nyumbani kwake eti kwa kuwa tulikuwa tunakula mchana na jioni chakula hicho hicho kwa mwaka mzima.

Asikudanganye mtu kikipikwa chakula hicho kwake sasa hivi anakula!!

Nilisoma hapo enzi za Dudu(R.I.P). Wali ulikuwa unaitwa nyali(wingi wa wali), uji ulikuwa unaitwa sifongo(haukuwa na sukari). Kama unahela ulikuwa unaenda Kontolengo kupiga chai na maandazi(mabanzi).Jioni unaenda Nsukanzi au Ipamba kutembea.
 
Uji ni Pora,..
Ugali ni Gaa,..
Wali ni Nyali,..
..R.I.P Kwao..
 
Kuna rafiki yangu Mbelgiji aliwahi kuniambia kitu nikacheka nusura nife kwa kupaliwa mate 'ukisoma shule ya bweni Tanzania basi una uwezo wa kukaa jela yeyote ulaya' na kisa cha kusema hivyo ni yale aliyoyaona tulipoenda kumtembelea mdogo wangu Forest Hill Sec
 
Kama umesoma shule ya bweni ya serikali basi hili ni jambo la kawaida sana utazoea na kupiga shule kwa furaha. Pale Tosamaganga tulikuwa tunaita Bondo, kuna jamaa aliapa kwamba akijapata ajira atapiga marufuku ugali na maharage nyumbani kwake eti kwa kuwa tulikuwa tunakula mchana na jioni chakula hicho hicho kwa mwaka mzima.

Asikudanganye mtu kikipikwa chakula hicho kwake sasa hivi anakula!!

Mi napenda mpangilo wa hayo mabakuli na rangi zake,yaani yamependeza. Ni kazi ya sanaa hiyo imefanyika hapo.
 
Kama umesoma shule ya bweni ya serikali basi hili ni jambo la kawaida sana utazoea na kupiga shule kwa furaha. Pale Tosamaganga tulikuwa tunaita Bondo, kuna jamaa aliapa kwamba akijapata ajira atapiga marufuku ugali na maharage nyumbani kwake eti kwa kuwa tulikuwa tunakula mchana na jioni chakula hicho hicho kwa mwaka mzima.

Asikudanganye mtu kikipikwa chakula hicho kwake sasa hivi anakula!!

dah kitu cha Malata hicho,dah Tosamaganga daima,,huyu mpishi wa shule 2shamdaka na ndoo ya nyama wanfunz anatulisha michuz duh!
 
songea boys au sobosea enzi za kusirawe said.tumekua tukiita nguna na wazee wa soft
 
Hapo ukiwa form one lazima uwe dreva wa kiranja kumbebea msosi ili uweze kushiba
 
Back
Top Bottom