Umeondoka tukiwa bado tunakuhitaji mno!

Umeondoka tukiwa bado tunakuhitaji mno!

banalunda

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2012
Posts
231
Reaction score
67
Leo jioni majira ya saa moja, maeneo ya mapinga Bagamoyo ilitokea ajali ya pikipiki kugongwa na daladala na kusababisha vifo vya watu watatu, akiwemo Baba yangu mdogo na amefariki palepale, kiukweli it is very sad for us, na tupo kwenye kipindi kigumu sana
 
Mkuu pole sana,

Ni kweli utakuwa kwenye kipindi kigumu ila yakupasa umuombe Mungu akupe moyo wa uvumilivu.

Pia ni wakati wa wafiwa wote kushikamana kwa pamoja na kufarijiana kwa kuondokewa na baba mdogo.

Mungu amlaze mahali pema baba mdogo.
 
Poleni na Mungu awape moyo wa subira wafiwa wote, tuko pamoja kwa kila hali katika wakati huu mgumu wa majonzi. RIP.
 
Pole mkuu mungu ni mwema muombe utapata faraja ya kweli,
pole sana.
 
Poleni sana mkuu. Mungu awatie nguvu katika hiki kipindi kigumu. Kazi ya Mungu haina makosa. Mia
 
Poleni sana kwa msiba huu. Mungu akupeni ujasiri na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu.
Marehemu apumzike kwa amani. Amina.
 
Leo jioni majira ya saa
moja, maeneo ya mapinga Bagamoyo ilitokea ajali ya pikipiki kugongwa na
daladala na kusababisha vifo vya watu watatu, akiwemo Baba yangu mdogo
na amefariki palepale, kiukweli it is very sad for us, na tupo kwenye
kipindi kigumu sana

niko bunju nipe maelekezo nije kukufariji
 
Dah so sad, pole sana Mungu akupe faraja mkuu, dunia tunapita
 
Poleni sana kwa msiba mkubwa uliowafika. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na awape nguvu na faraja katika kipindi hiki kigumu kwenu~AMEN
 
Back
Top Bottom