Umeme vijijini: futuhi wametoa point ya msingi

Umeme vijijini: futuhi wametoa point ya msingi

Naibili

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2011
Posts
1,878
Reaction score
1,060
Habari wadau,
Mdau nilikuwa nnaangalia kipindi cha futuhi, kinachorushwa na Star Tv , wamezungumzia swala la umeme vijijini ingawa ni kwa vichekesho lakini nnamimi ujumbe umefika. Wamesema umeme vijijini, nyumba zenyewe za nyasi je watakuwa na sifa za kuwekewa umeme?

Wameongezea kuwa ni bora wapewe kwanza mifuko ya sementi ili waboreshe kwanza makazi yao.
wadau hapa kuna mambo yakujadili
1) makazi duni
2) kumudu gharama za umeme. e.t.c
Je wakazi wa vijijini wameandaliwa kupokea huo umeme ambao serikali inaupigia chapuo
 
Labda wapeleke Msoga huo umeme!!!! maudhui yao ni mazuri ukitaka meza ukitaka acha!!!
 
yaani hiyo ni sawa na kilimo kwanza bila ya elimu kwa mkulima, au maisha bora wakati kodi kwa maskini zinaongezeka!
 
Swala ni umeme ufike kwenye eneo husika, sijui nyumba a nyasi au ya udongo ni vya baadae.
Tunataka umeme vijijiniiiiiiiiiii
 
Umeme vijijin ni ndoto ya mchana kwa kuwa na yenyeww ni kama ahadi zingine zilizotolewa na serikali hiihi ambazo hazijatekalezwa tangu 2010. Hapo tu nikufunika kombe ili mwanahalam apite.
 
Ni kituko kingine kutoka Tanzania ambapo serikali inaweka kipaumbele cha umeme bila msukumo wa makazi bora.Bei ya bidhaa na vifaa vya ujenzi iko juu sana hivyo tuanzie huko kwanza.Ni upuuzi kuamini mwananchi anayemiliki kitembe ambacho thamani yake ni 80,000tsh eti atavuta umeme na kumudu gharama.Sera iwe ubora wa makazi kwanza, umeme baadae!
 
Liganga na mchuchuma tangu utoto mpaka uzee wangu...sasa wameongeza na hili.....
Nenda vijijini kajionee hao wanaotaka kuletewa umeme ndio utajua kama wanahitaji umeme kwanza au huduma ya maji safi na salama....
 
Hapo futuhi wamechemka! Wao wamelenga karibu wakati serikali inalenga mbali miaka 10 na kuendelea. Sasa hivi vijijini kuna mabadiliko makubwa sana kuhusu makazi, jaribu kulinganisha kijijini kwenu miaka 10 iliyopita uone tofauti iliyopo na sasa. Serikali inafanya vizuri sana katika hili, siyo halali kubweteka eti mpaka makazi yawe bora ndo tuwapelekee umeme!! GO GO GO Muhongo. Jamani wakati mwingine mnyonge tumnyonge lakini haki yake tumpe! Umeme ni kichocheo kingine kinachowafanya raia kubadili makazi yao, chunguzeni kote kulikowekwa umeme vijijini mwone jinsi raia wanavyoshughulika! Sikutegemea kama usukumani nao wangezinduka kuhusu ujenzi wa nyumba bora!
 
Sina tatizo na umeme kwenda vijijini ila swali kwa Serikali. Je iwapo mjini watu wanalalamikia bili hizi zinazopanda kila siku Je vijijini wataweza kumudu gharama?
 
Ni siasa tu, utaona kama umeme utapelekwa huko. Wanatafuta pesa za kampeni tu!!!!!
 
Hapo futuhi wamechemka! Wao wamelenga karibu wakati serikali inalenga mbali miaka 10 na kuendelea. Sasa hivi vijijini kuna mabadiliko makubwa sana kuhusu makazi, jaribu kulinganisha kijijini kwenu miaka 10 iliyopita uone tofauti iliyopo na sasa. Serikali inafanya vizuri sana katika hili, siyo halali kubweteka eti mpaka makazi yawe bora ndo tuwapelekee umeme!! GO GO GO Muhongo. Jamani wakati mwingine mnyonge tumnyonge lakini haki yake tumpe! Umeme ni kichocheo kingine kinachowafanya raia kubadili makazi yao, chunguzeni kote kulikowekwa umeme vijijini mwone jinsi raia wanavyoshughulika! Sikutegemea kama usukumani nao wangezinduka kuhusu ujenzi wa nyumba bora!

Unafikiri miaka kumi mingi? Watu kama hawajawezeshwa hata miaka 50 hali itabaki vivo hivyo,ukizingatia vijana wote wakikua tu wanakimbilia mjini,na huko vijijini wanabaki wazee tu,je huo umeme wenu utafidisha nini? Sera ya cdm 2010 ilikua nzuri sana ya kushusha bei za building material basically cement na bati,elimu bure na kuboresha shule,mi nafikiri hili lingesaidia,sasa hv kupeleka umeme vijijini ni sawa na kumpa kibogoyo mfupa,atautamani lakini hawez fanya lolote.
 
Ni kituko kingine kutoka Tanzania ambapo serikali inaweka kipaumbele cha umeme bila msukumo wa makazi bora.Bei ya bidhaa na vifaa vya ujenzi iko juu sana hivyo tuanzie huko kwanza.Ni upuuzi kuamini mwananchi anayemiliki kitembe ambacho thamani yake ni 80,000tsh eti atavuta umeme na kumudu gharama.Sera iwe ubora wa makazi kwanza, umeme baadae!

Mkuu issue ya msingi umeme ufike vijijin. Mambo kuingiza kwny nyumba z another issue
 
Swala ni umeme ufike kwenye eneo husika, sijui nyumba a nyasi au ya udongo ni vya baadae.
Tunataka umeme vijijiniiiiiiiiiii

ukipeleka umeme alafu hakuna watumiaji hiyo ni wastage of resouces.
vijijini wanahitaji huduma bora za afya, miundombino bora ya barabara, maji safi na salama
 
Serikali iko sahihi kupeleka umeme vijijini. Suala la makazi litakuwa motivated na maendeleo makubwa kama haya ya umeme. Na huwezi kusubiri raia eti wajenge nyumba ndiyo upeleke umeme, hiyo itakuwa ni akili ndogo. Umeme vijijini unafika nimeshuhudia sehemu kama Mdabulo, Rungemba, Ulete, umeme unapelekwa kuna maeneo kama Malangali kazi imeanza. So, nadhani serikali imedhamiria. Go go go Serikali. Wasioitakia mema nchi hii na wapinzani wa Serikali ndiyo wanapinga mkakati huu.
 
Back
Top Bottom