Umeme vijijini: futuhi wametoa point ya msingi

Umeme vijijini: futuhi wametoa point ya msingi

Umeme vijijin ni ndoto ya mchana kwa kuwa na yenyeww ni kama ahadi zingine zilizotolewa na serikali hiihi ambazo hazijatekalezwa tangu 2010. Hapo tu nikufunika kombe ili mwanahalam apite.

kwanza wanajichanganya waziri mkuu anasema kodi ya simu ni umeme vijijini, waziri kwenye bajet amesema kodi mpya kwenye mafuta ni ajili ya umeme vijijini
 
Hapo futuhi wamechemka! Wao wamelenga karibu wakati serikali inalenga mbali miaka 10 na kuendelea. Sasa hivi vijijini kuna mabadiliko makubwa sana kuhusu makazi, jaribu kulinganisha kijijini kwenu miaka 10 iliyopita uone tofauti iliyopo na sasa. Serikali inafanya vizuri sana katika hili, siyo halali kubweteka eti mpaka makazi yawe bora ndo tuwapelekee umeme!! GO GO GO Muhongo. Jamani wakati mwingine mnyonge tumnyonge lakini haki yake tumpe! Umeme ni kichocheo kingine kinachowafanya raia kubadili makazi yao, chunguzeni kote kulikowekwa umeme vijijini mwone jinsi raia wanavyoshughulika! Sikutegemea kama usukumani nao wangezinduka kuhusu ujenzi wa nyumba bora!

una maana umeme utawaletea huduma za afya, maji, bara bara
 
Hizo zote siasa, Tatizo la midanganyika miradi au sera zinapoanzishwa serikali hitangaza sana lakini hutasikia taarifa za hatua za utekelezaji wake, aidha kama imefanikiwa au imefeli. Tena kama imefeli ndo kimya kabisaaa! Maisha bora kwa kila mtanzania iko wapi? Kilimo kwanza imefanikiwa? vipi kuhusu MKUKUTA, MKURABITA etc? Ok, umeme vijijini, pamoja na bei kuwa juu je mijini umetoshereza na watu wako happy?
Chukua chako mapema!
 
hapo futuhi wamechemka! Wao wamelenga karibu wakati serikali inalenga mbali miaka 10 na kuendelea. Sasa hivi vijijini kuna mabadiliko makubwa sana kuhusu makazi, jaribu kulinganisha kijijini kwenu miaka 10 iliyopita uone tofauti iliyopo na sasa. Serikali inafanya vizuri sana katika hili, siyo halali kubweteka eti mpaka makazi yawe bora ndo tuwapelekee umeme!! Go go go muhongo. Jamani wakati mwingine mnyonge tumnyonge lakini haki yake tumpe! Umeme ni kichocheo kingine kinachowafanya raia kubadili makazi yao, chunguzeni kote kulikowekwa umeme vijijini mwone jinsi raia wanavyoshughulika! Sikutegemea kama usukumani nao wangezinduka kuhusu ujenzi wa nyumba bora!

we utakua unaongelea vijiji vya pugu,kitunda na kivule
 
Mkuu issue ya msingi umeme ufike vijijin. Mambo kuingiza kwny nyumba z another issue

Dah! Sijuhi Akili ya wapi hii?
Ni sawa na Kujenga Viwanja vya ndege wakati mwenye ndege ni raisi tu na Huko kwenye viwanja hakuna hata Barabara.

Pia Kumbuka una peleka umeme wakati watu hata Maji safi/Machafu hakuna, Zahanati hakuna, Shule hakuna kama ipo ni gofu tu, hakuna walimu wala wanafunzi hawahudhurii.
 
Swala ni umeme ufike kwenye eneo husika, sijui nyumba a nyasi au ya udongo ni vya baadae.
Tunataka umeme vijijiniiiiiiiiiii

Big Results Now! Hao ndiyo viongozi wetu bwana, wanataka kujenga Rome kwa siku moja! Dah
 
Futuhi hapa wamejaribu kutuonesha picha kubwa ya nani anapanga vipaumbele vya mahali husika, ni wanannchi wenyewe au wasomi wachache wanaokutana mahotelini na kuamua kuhusu maeneo wanayoyajulia kwenye 'ripoti'. Vipo vijiji vingi tu ambavyo umeme si hitaji lao la msingi, kwao maji ndo hitaji la msingi, hawa hawahitaji umeme, wanahitaji MAJI safi na salama.

Hakuna dhambi mbaya kama ya kudhani unajua nataka nini kabla ya kuniuliza, hivi dhana ya kupeleka maamuzi kwa wananchi iko wapi linapokuja suala la kuamua 'tunataka nini kwanza au kwa wakati mmoja? Hata kama serikali ina 'nia' kweli ni wakati wa kukaa na wananchi na kuuliza vipaumbele vinginevyo ile sense ya ownership itapotea na hujuma ya huo umeme itakuwa ni kubwa kuliko.

Wamechekesha, ndiyo, ujumbe ufike na huu si wakati wa kunipangia nataka nini bila kuniuliza, BTW misingi ya utawala bora na ugatuzi wa madaraka unasema kuhusu ushiriki wa wananchi na hata wachache lazima haki zao ziheshimike (politics of limited objectives)
 
Hivi kati ya umeme na maji vijijini, kipi kitangulie?
 
Ni kituko kingine kutoka Tanzania ambapo serikali inaweka kipaumbele cha umeme bila msukumo wa makazi bora.Bei ya bidhaa na vifaa vya ujenzi iko juu sana hivyo tuanzie huko kwanza.Ni upuuzi kuamini mwananchi anayemiliki kitembe ambacho thamani yake ni 80,000tsh eti atavuta umeme na kumudu gharama.Sera iwe ubora wa makazi kwanza, umeme baadae!

Hili suala la kodi kwenye vifaa vya ujenzi ccm na Serikali yake walitangaza kulifanyia kazi sijui limeishia wapi.!!!
 
Swala ni umeme ufike kwenye eneo husika, sijui nyumba a nyasi au ya udongo ni vya baadae.
Tunataka umeme vijijiniiiiiiiiiii


kabla ya kulilia kuletewa Umeme vijijini; nilitarajia mtataka kuletewa na kuboreshewa huduma za jamii mfano Afya, madawa, mbolea, mbegu bora, uhakika wamasoko kwa mazao yenu, barabara, vituo vya polisi nk.


Waangalie hawa huko vijijini mlivyo ambako mnataka umeme jinsi mnavyoishi:-

Akina+mama+wakibeba+mizigo+na+watoto,+kijiji+cha+Kagera+Nkanda+wilaya+ya+Kasulu+-+Kigoma.jpg


Na hizi ndizo nyumba zeu mnazotaka kuweka umeme:-

View attachment 104152

Makuti.jpg

Hapa huenda ni kwa Mwenyekiti wa Kijiji au Diwani - yeye kaweka DISH.

Mbavu za mbwa.jpg

Hii ni ofisi ya CCM ya Kijiji:-

Ofisi ya CCM 01.JPG

Hizi ndizo Shule wanakosoma watoto wenu:-

wanafunzi-mkapa-school.jpg

View attachment 104157


Hii ni Hospitali yenu mnayotibiwa mnataka kuwekewa Umeme hapa:-

WAGONJWA_ZAHANATI_KISAKI[1]_.JPG


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI......

ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CCM......

CCM OYEEEEEEEEEEEEE........

......WAJINGA NDIO WALIWAO.......



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!​
 
yaani hiyo ni sawa na kilimo kwanza bila ya elimu kwa mkulima, au maisha bora wakati kodi kwa maskini zinaongezeka!

Umenena mkuu. Watu wanapelekewa huduma kabla ya kuandaa mazingira ya huduma yenyewe hehe. It's only in Tanzania.
 
idawa; Tangu lini serikali ya CCM ikasema tunalifanyia kazi jambo na likafanikiwa? Vifaa vya ujenzi bado gharama yake iko juu!
 
Last edited by a moderator:
Umeme ni chachu ya maendeleo kwa maana umeme ukiwepo vijijini;
1.Maji safi na salama yatapatika kwakua mitambo itatumia umeme
kusukuma maji maeneo yaliyo na maji kwenda maeneo yasiyo na maji.

2.Wananchi wataboresha makazi yao either kwa kushirikiana kijamaa au
kwa msaada wa ndugu zao walioko mijini,kizuri zaidi badala ya kufuja
pesa zitokanazo na mifugo na mazao ya kilimo watazitumia katika maboresho
ya makazi yao.
3.Ajira kwa vijana katika viwanda vidogo vidogo zitapatikana kwa urahisi.
4.Rular to urban migration itapungua kwa kasi.
5.Umaskini wa kipato utapungua hasa maeneo ya mijini ambapo wimbi la vijana wanaohamia
kila siku mijini kujikita katika ajira moja utapungua.
6.Ni wazi kabisa jamii na viongozi wa jamii husika watahakikisha kuwa nguvukazi yao
haipotei bure kusikojulikana na wataamua kwa dhati kupanga mikakati ya kuwasaidia
vijana hasa wale wanaomaliza elimu zao kama dhana za kazi vijijini.

Si vibaya kama kila kijiji kitaweka vipaumbele vyao ili fedha na misaada mingine itakapokuja
viweze kuanza na vipaumbele vyao.
 
Ni kituko kingine kutoka Tanzania ambapo serikali inaweka kipaumbele cha umeme bila msukumo wa makazi bora.Bei ya bidhaa na vifaa vya ujenzi iko juu sana hivyo tuanzie huko kwanza.Ni upuuzi kuamini mwananchi anayemiliki kitembe ambacho thamani yake ni 80,000tsh eti atavuta umeme na kumudu gharama.Sera iwe ubora wa makazi kwanza, umeme baadae!

ambao hawaja sapoti hoja yako jua wanachuki binafi
saluti Jr
 
Mimi nafikiri nia ya Serikali kupeleka umeme vijijini ni pamoja na kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na matumizi makubwa ya kuni na mkaa kama nishati kwa ajili ya kupikia.

Kwa sasa, gharama za umeme ziko juu sana na sidhani kama wananchi wa vijijini wataweza kuzimudu. Hata mjini watu wengi hawatumii umeme kupikia kutokana na gharama kubwa.

Ni muhimu serikali ikaangalia jinsi ya kupunguza gharama za umeme ili watu wengi waweze kuzimudu.Tofauti na hivyo, watu hawatamudu na wale wachache watakaomudu watakuwa wanatumia umeme kwa ajili ya mwanga tu vifaa ambavyo havitumii umeme mwingi kama radio.
 
Swala ni umeme ufike kwenye eneo husika, sijui nyumba a nyasi au ya udongo ni vya baadae.
Tunataka umeme vijijiniiiiiiiiiii

Kama mnataka umeme vijijini pelekeni kwa fedha zenu.
 
Hakuna umeme vijijini hapo suala ni kwamba ccm wanatafuta pesa za uchaguzi 2015 maana vyanzo vingine vinaonekana kustukiwa na raia. walianza na kutenga fedha nyingi za ukaguzi wa miradi ya maendeleo wakati kila mradi unaosimamiwa na serikali una bajeti yake ya ukaguzi. Mnyika akawastukia akawaumbua mchana kweupe sasa wakaona watoke kwa namna hii ya kutoza kodi kwenye simcard!!!!!!! ila naona nayo watu wameanza kuitolea macho sasa sijui itakuwaje??!!!
 
Back
Top Bottom