Umeme vijijini: futuhi wametoa point ya msingi

Umeme vijijini: futuhi wametoa point ya msingi

kwanza wanajichanganya waziri mkuu anasema kodi ya simu ni umeme vijijini, waziri kwenye bajet amesema kodi mpya kwenye mafuta ni ajili ya umeme vijijini

Hakuna kilichoharibika, kubwa umeme ufike kijijini kwetu.
 
Hizo zote siasa, Tatizo la midanganyika miradi au sera zinapoanzishwa serikali hitangaza sana lakini hutasikia taarifa za hatua za utekelezaji wake, aidha kama imefanikiwa au imefeli. Tena kama imefeli ndo kimya kabisaaa! Maisha bora kwa kila mtanzania iko wapi? Kilimo kwanza imefanikiwa? vipi kuhusu MKUKUTA, MKURABITA etc? Ok, umeme vijijini, pamoja na bei kuwa juu je mijini umetoshereza na watu wako happy?
Chukua chako mapema!

Vp umeazimisha akili yako.
 
Dah! Sijuhi Akili ya wapi hii?
Ni sawa na Kujenga Viwanja vya ndege wakati mwenye ndege ni raisi tu na Huko kwenye viwanja hakuna hata Barabara.

Pia Kumbuka una peleka umeme wakati watu hata Maji safi/Machafu hakuna, Zahanati hakuna, Shule hakuna kama ipo ni gofu tu, hakuna walimu wala wanafunzi hawahudhurii.

Nahisi hujitambui unataka serikali ikujengee nyumba. Uwepo wa kimoja husaidia katika sekta nyingine na wakazi wengi siku hizi wanainua nyumba za bati labda kama huko kwenu bado kuna vijana mnaoezeka makuti, Mkimsubiri dr awaletee bati...
 
][/B]Hapo futuhi wamechemka! Wao wamelenga karibu wakati serikali inalenga mbali miaka 10 na kuendelea. Sasa hivi vijijini kuna mabadiliko makubwa sana kuhusu makazi, jaribu kulinganisha kijijini kwenu miaka 10 iliyopita uone tofauti iliyopo na sasa. Serikali inafanya vizuri sana katika hili, siyo halali kubweteka eti mpaka makazi yawe bora ndo tuwapelekee umeme!! GO GO GO Muhongo. Jamani wakati mwingine mnyonge tumnyonge lakini haki yake tumpe! Umeme ni kichocheo kingine kinachowafanya raia kubadili makazi yao, chunguzeni kote kulikowekwa umeme vijijini mwone jinsi raia wanavyoshughulika! Sikutegemea kama usukumani nao wangezinduka kuhusu ujenzi wa nyumba bora!

Kimsingi hawajachemka ila wamefungua mjadala mpya kwamba wakati umeme unapelekwa kuna haja ya serikali kuangalia hali ya makazi kama yana vigezo vya kupelekewa umeme maana mwisho wa siku umeme unapelekwa na linawekwa transformer watumiaji wanakuwa 6, nilichojifunza mie kutokana na huu uzi pia na point yako hapo nilipo-bold kwamba kuna mazingira wananchi wanaweza kujenga nyumba nzuri kama watapata elimu ya ujenzi wa technolojia rahisi hivyo kupitia huduma hii ya umeme inaweza ikawa fursa nzuri kwa serikali na wadau wengine kutoa elimu kwa wananchi wake kwa kuwa kila kitu kinakuwa kinaonekana kwa macho
 
Futuhi hapa wamejaribu kutuonesha picha kubwa ya nani anapanga vipaumbele vya mahali husika, ni wanannchi wenyewe au wasomi wachache wanaokutana mahotelini na kuamua kuhusu maeneo wanayoyajulia kwenye 'ripoti'. Vipo vijiji vingi tu ambavyo umeme si hitaji lao la msingi, kwao maji ndo hitaji la msingi, hawa hawahitaji umeme, wanahitaji MAJI safi na salama.

Hakuna dhambi mbaya kama ya kudhani unajua nataka nini kabla ya kuniuliza, hivi dhana ya kupeleka maamuzi kwa wananchi iko wapi linapokuja suala la kuamua 'tunataka nini kwanza au kwa wakati mmoja? Hata kama serikali ina 'nia' kweli ni wakati wa kukaa na wananchi na kuuliza vipaumbele vinginevyo ile sense ya ownership itapotea na hujuma ya huo umeme itakuwa ni kubwa kuliko.

Wamechekesha, ndiyo, ujumbe ufike na huu si wakati wa kunipangia nataka nini bila kuniuliza, BTW misingi ya utawala bora na ugatuzi wa madaraka unasema kuhusu ushiriki wa wananchi na hata wachache lazima haki zao ziheshimike (politics of limited objectives)

Issue ya maendeleo ni pana sana. Ukitaka wananchi wakupe wanayoyahitaji utakesha. Mwingine atakwambia barabara mwingine ukumbi wa dsco mwingine viwanja. Kwa hiyo lazima itazame ni vp vya msingi na vitstimulate maendeleo. Tatizo lenu nyie mnaokaa kwenye umeme na wapinzani ndiyo mnaopinga hii issue ya umeme. Tuoneeni huruma tumechoka kukaa gizani. Tena ngoja nijenge kanyumba ka bati kwa sbb umeme unakuja huku Malangali.
 
Dr.Slaa akumbukwe kwa sera yake 2010 ya makazi bora.Wananchi waliielewa ndo mana wakampa urais
 
Serikali iko sahihi kupeleka umeme vijijini. Suala la makazi litakuwa motivated na maendeleo makubwa kama haya ya umeme. Na huwezi kusubiri raia eti wajenge nyumba ndiyo upeleke umeme, hiyo itakuwa ni akili ndogo. Umeme vijijini unafika nimeshuhudia sehemu kama Mdabulo, Rungemba, Ulete, umeme unapelekwa kuna maeneo kama Malangali kazi imeanza. So, nadhani serikali imedhamiria. Go go go Serikali. Wasioitakia mema nchi hii na wapinzani wa Serikali ndiyo wanapinga mkakati huu.

Hivyo vijiji unavyosema ni vya kiwango gani kimaendeleo?na umeme umefikishwa hapo kwa utaratibu upi?au nyee wenzetu mulianza kulipia kodi za laini tangu zamani ndiyo maana mukaletewa umeme.Maana yake kuna vijiji vingi sana hapa Tz ambavyo nyumba za bati ni za kuhesabu tena kwa mbali zilizo bakia zote ni nyasi na makuti ukiingia humo ndani amejitahidi sana ni chumba sebule tajiri wa kijiji ndiyo utakuta ana chumba sebule chumba.Malazi ndiyo usiseme mifugo humo humo watoto wote humo humo kupata sh100 kwake ni tabu mpaka auze mazao ndiyoaipate na ni kwa ajili ya chumvi tu.Sasa ndiyo umwambie kuwa alipie na umeme ataweza wapi labda kama watapelekewa bila kutoa gharama zozote na wawe wanatumia bure.
 
Issue ya maendeleo ni pana sana. Ukitaka wananchi wakupe wanayoyahitaji utakesha. Mwingine atakwambia barabara mwingine ukumbi wa dsco mwingine viwanja. Kwa hiyo lazima itazame ni vp vya msingi na vitstimulate maendeleo. Tatizo lenu nyie mnaokaa kwenye umeme na wapinzani ndiyo mnaopinga hii issue ya umeme. Tuoneeni huruma tumechoka kukaa gizani. Tena ngoja nijenge kanyumba ka bati kwa sbb umeme unakuja huku Malangali.
Habari za Isimikinyi? Hapo malangali mbona ni candidate wazuri tu wa umeme lakini can we afford?
 
  • Thanks
Reactions: Obe
...wakiongeza juhudi kidogo tu watanunuliwa na Manji na yule jamaa wa Home Shopping center kama akina Masanja. Akina Masanja walipokuwa EATV waliwaigiza sana akina Manji na wizi wa EPA, leo hii ukimuuliza Masanja kuhusu EPA atakuuliza "what do you mean?" --halafu anajidai kaokoka anaimba gospel -unafiki mtupu.
 
sisi tunaotembea vijijini tumeona haswa mikoa ya kusini umeme umepita lakini wananchi hawawezi kuweka.Serikali ifanye kazi moja ya kuongeza kipato cha kaya na ukitaka hvyo ni kuongeza kodi kwa matajiri na kuratibu masoko ya mazao vizuri kwa kutafuta soko la uhakika na kuboresha miundombinu vijijini. Kuongeza kodi nyingi kwa daraja la chini litaathiri daraja hili kujikwamua na kuingia daraja la kati na hili litafanya malengo ya millenia kutofikiwa. Siku zote purchasing power ikiwa kubwa kwenye nchi , uchumi unakuwa mzuri hata foreign market ikitetereka haitaathiri sana uchumi wa nchi. Mfano wa CHINA domestic market si nzuri kwa kuwa haikuwezesha pato la kaya vizuri na hii walifanya kwa kutoongeza mshahara kwa wafanyakazi wake na riba ya kutunza fedha benki kuwa ndogo na imewaletea shida sasa kwa kuwa foreign market imeyumba sasa. Tanzania inataka kuharibu domestic market kwa kutoza kodi nyingi kwa mlalahoi hvyo kutoweza kupiga hatua kwenda daraja la kati , maana daraja la kati ndilo lenye purchasing power kubwa
 
Hapo futuhi wamechemka! Wao wamelenga karibu wakati serikali inalenga mbali miaka 10 na kuendelea. Sasa hivi vijijini kuna mabadiliko makubwa sana kuhusu makazi, jaribu kulinganisha kijijini kwenu miaka 10 iliyopita uone tofauti iliyopo na sasa. Serikali inafanya vizuri sana katika hili, siyo halali kubweteka eti mpaka makazi yawe bora ndo tuwapelekee umeme!! GO GO GO Muhongo. Jamani wakati mwingine mnyonge tumnyonge lakini haki yake tumpe! Umeme ni kichocheo kingine kinachowafanya raia kubadili makazi yao, chunguzeni kote kulikowekwa umeme vijijini mwone jinsi raia wanavyoshughulika! Sikutegemea kama usukumani nao wangezinduka kuhusu ujenzi wa nyumba bora!


"Ni upumbavu kushabikia ujinga"
 
sisi tunaotembea vijijini tumeona haswa mikoa ya kusini umeme umepita lakini wananchi hawawezi kuweka.Serikali ifanye kazi moja ya kuongeza kipato cha kaya na ukitaka hvyo ni kuongeza kodi kwa matajiri na kuratibu masoko ya mazao vizuri kwa kutafuta soko la uhakika na kuboresha miundombinu vijijini. Kuongeza kodi nyingi kwa daraja la chini litaathiri daraja hili kujikwamua na kuingia daraja la kati na hili litafanya malengo ya millenia kutofikiwa. Siku zote purchasing power ikiwa kubwa kwenye nchi , uchumi unakuwa mzuri hata foreign market ikitetereka haitaathiri sana uchumi wa nchi. Mfano wa CHINA domestic market si nzuri kwa kuwa haikuwezesha pato la kaya vizuri na hii walifanya kwa kutoongeza mshahara kwa wafanyakazi wake na riba ya kutunza fedha benki kuwa ndogo na imewaletea shida sasa kwa kuwa foreign market imeyumba sasa. Tanzania inataka kuharibu domestic market kwa kutoza kodi nyingi kwa mlalahoi hvyo kutoweza kupiga hatua kwenda daraja la kati , maana daraja la kati ndilo lenye purchasing power kubwa

asante mkuu, hapo unadhihirisha serikali haifanyi utafiti kabla ya kupanga vupaumbele vyao.
 
Serikali iko sahihi kupeleka umeme vijijini. Suala la makazi litakuwa motivated na maendeleo makubwa kama haya ya umeme. Na huwezi kusubiri raia eti wajenge nyumba ndiyo upeleke umeme, hiyo itakuwa ni akili ndogo. Umeme vijijini unafika nimeshuhudia sehemu kama Mdabulo, Rungemba, Ulete, umeme unapelekwa kuna maeneo kama Malangali kazi imeanza. So, nadhani serikali imedhamiria. Go go go Serikali. Wasioitakia mema nchi hii na wapinzani wa Serikali ndiyo wanapinga mkakati huu.

Acha kuandika bila kufikiri, ss hapa mpinzani gani asiyetaka maendeleo?
Wakati unaona kila siku watu wanapiga makelele kwa ajili ya maendeleo?
 
Kwetu ushaletwa mkuu. Hamna siasa
Kwa tozo la 1000 kila line ya simu kwa mwezi na huu ni mwezi wa saba ndo kwanza tarehe moja mwezi huu ule mswada umepita? Na umefika kijijini kwenu muda huu? Sidhani na si kutendwa na serikali hii ya Chama Cha Mapinduzi ya Mdomoni!!!!!
 
Hakuna umeme vijijini hapo suala ni kwamba ccm wanatafuta pesa za uchaguzi 2015 maana vyanzo vingine vinaonekana kustukiwa na raia. walianza na kutenga fedha nyingi za ukaguzi wa miradi ya maendeleo wakati kila mradi unaosimamiwa na serikali una bajeti yake ya ukaguzi. Mnyika akawastukia akawaumbua mchana kweupe sasa wakaona watoke kwa namna hii ya kutoza kodi kwenye simcard!!!!!!! ila naona nayo watu wameanza kuitolea macho sasa sijui itakuwaje??!!!


Hawa watu wa vijijini hawajui jinsi Wajanja wanavyokula hapa TZ.


Mfano katika bajeti Serikali imetangaza kuwa wana mpango wa kuanzisha Benk ya Wakulima;

Wabunge kwa umbumbumbu wakashangilia na kupiga makofi eti mkombozi wa wakulima atapatikana!!!!

Janja yao binafsi nimeishitukia kutafuta fedha tu!!!!!!


KUNA BENK YA "CRDB" (Cooperative and Rural Development Bank)Benki ya Ushirika na maendeleo Vijini.

Malengo ya hii benki miaka ilipoanzishwa ni kama jina lake linavyojieleza lakini hivi sasa hii benki imekuwa kwa ajili ya mafisadi na wafanyabiashara wakubwa. Haimnufaishi mkulima wala vyama vya ushirika.

Hii Benki ipo maeneo ya mijini tu huko vijijini kwanza hata hawajui kama kuna benki ya maendeleo vijijini. Enzi zile za utawala wa awamu ya kwanza kweli nakubali hii benki ilifanya kazi iliyokusudiwa, nakumbuka vijiji walikuwa wanakopeshwa magari ya kijiji na matrekta ya kijiji toka katika benki hii.

Leo hii Serikali wanakuja na ndoto za kuanzisha kitu ambacho kipo tayari. Kwa nini wasielekeze nguvu za CRDB katika malengo ya kuanzishwa kwake???? Au wabadirishe jina hii benki isiwe CRDB tena atafute jina lingine tujue moja.

Sas mnasema mnataka kupeleka umeme vijijini na ikiwa watu wapo katika enzio za UJIMA kutumia jembe la mkono!!!!!!!

Huduma za afya ni mbovu!!!!!!

nk nk nk nk


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Habari wadau,
Mdau nilikuwa nnaangalia kipindi cha futuhi, kinachorushwa na Star Tv , wamezungumzia swala la umeme vijijini ingawa ni kwa vichekesho lakini nnamimi ujumbe umefika. Wamesema umeme vijijini, nyumba zenyewe za nyasi je watakuwa na sifa za kuwekewa umeme?

Wameongezea kuwa ni bora wapewe kwanza mifuko ya sementi ili waboreshe kwanza makazi yao.
wadau hapa kuna mambo yakujadili
1) makazi duni
2) kumudu gharama za umeme. e.t.c
Je wakazi wa vijijini wameandaliwa kupokea huo umeme ambao serikali inaupigia chapuo

Wanapoongelea vijijini ni makao makuu ya kata kule usukumani wanaita sentani
 
Back
Top Bottom