A
Anonymous
Guest
Kero yangu ni kukatika-katika kwa umeme mara kwa mara katika eneo la MATIKA, Kata ya Lugarawa, Wilaya ya LUDEWA, Mkoa wa Njombe huku wahusika wakikaa kimya bila kufanyia ufumbuzi suala hili, tunaomba TANESCO Wilaya ya LUDEWA watueleze ni lini tatizo hili litakwisha maana imekuwa ni kero kubwa hasa nyakati za jioni.
Umeme huwa unakatika mara kwa mara hasa nyakati za jioni kuanzia Saa 12 mpaka Saa tano usiku na hakuna taarifa zozote za kufanyia ufumbuzi ni kero sana.
Ni mwezi mzima na tunashindwa kuangalia hata taarifa za habari usiku maana umeme unakatika kila muda, kwakifupi hatuna furaha na umeme wao ni kama tunapewa msaada.
Umeme huwa unakatika mara kwa mara hasa nyakati za jioni kuanzia Saa 12 mpaka Saa tano usiku na hakuna taarifa zozote za kufanyia ufumbuzi ni kero sana.
Ni mwezi mzima na tunashindwa kuangalia hata taarifa za habari usiku maana umeme unakatika kila muda, kwakifupi hatuna furaha na umeme wao ni kama tunapewa msaada.