Manyanza
Platinum Member
- Nov 4, 2010
- 19,940
- 45,557
wana Jamvi
nilipokuwa napata dinner jioni hii, ghafla Umeme ukakatika.
nikakumbuka miaka 11 iliyopita.
ilikuwa jioni moja tumekaa mkekani tunajiandaa kula ilikuwa ni ugali na samaki na mchicha ghafla umeme ukakatika,nikainuka kwenda kutafuta Taa ya Chemli nikavaa Kandambili zangu wakati nakatisha katika ya chakula mguu ukatua ndani ya bakuli la mboga yaani samaki! haraka haraka nikautoa na sikusema kitu nikaenda kunawa nikaleta taa nikawasha tukaendelea na kupiga Menu kama kawaida lakini sikula samaki wala mchuzi mpaka mwisho nilikula mchicha tu.
nimeikumbuka hii jioni hii mara baada ya umeme kukatika wakati nakula
haya ni baadhi ya madhala ya kukatika bila taarifa.
KAMA NA WEWE UNALO LAKO UNAWEZA KUTUJUZA
nilipokuwa napata dinner jioni hii, ghafla Umeme ukakatika.
nikakumbuka miaka 11 iliyopita.
ilikuwa jioni moja tumekaa mkekani tunajiandaa kula ilikuwa ni ugali na samaki na mchicha ghafla umeme ukakatika,nikainuka kwenda kutafuta Taa ya Chemli nikavaa Kandambili zangu wakati nakatisha katika ya chakula mguu ukatua ndani ya bakuli la mboga yaani samaki! haraka haraka nikautoa na sikusema kitu nikaenda kunawa nikaleta taa nikawasha tukaendelea na kupiga Menu kama kawaida lakini sikula samaki wala mchuzi mpaka mwisho nilikula mchicha tu.
nimeikumbuka hii jioni hii mara baada ya umeme kukatika wakati nakula
haya ni baadhi ya madhala ya kukatika bila taarifa.
KAMA NA WEWE UNALO LAKO UNAWEZA KUTUJUZA