daxy Jr

Member
Apr 15, 2020
88
304
KIMJONG.jpg

(1) Kalenda ya Korea Kaskazini inategemea mwaka wa kuzaliwa wa mwanzilishi wa nchi hiyo, Kim Il-Sung. Mwaka huu 2023, Korea Kaskazini itaadhimisha mwaka wa 112, kwa vile Kim Il-Sung alizaliwa mwaka 1912.

(2) Korea Kaskazini ina mfumo wake (operating system) kwenye upande wa computers zao, unaoitwa Red Star OS. Ni toleo lililorekebishwa la Linux na limeundwa ili kuwaweka watumiaji wote ndani ya nchi chini ya uangalizi.

(3) Korea Kaskazini ina time zone yake, inayojulikana kama ''Pyongyang Time'', ambayo iko dakika 30 nyuma ya Korea Kusini na Japan.

(4) Serikali nchini Korea Kaskazini imepiga marufuku mitindo fulani ya nywele, zikiwemo nywele ndefu za wanaume na mitindo fulani ya wanawake. Inasemekana kuna mitindo 28 pekee ya nywele iliyoidhinishwa na serikali kwa wanawake na 10 kwa wanaume.

(5) Nchini Korea Kaskazini, ni lazima kuvaa beji yenye picha ya mwanzilishi wa nchi hiyo, Kim Il-Sung, na mwanawe, Kim Jong-Il. Kukosa kufanya hivyo kunaweza kusababisha adhabu.

(6) Korea Kaskazini ina jeshi la watu milioni 1.2, ambayo ni ya nne kwa ukubwa duniani. Hata hivyo, nchi hiyo pia inajulikana kwa kuwa na vifaa vya kijeshi vilivyopitwa na wakati na visivyotunzwa vizuri.

(7) Korea Kaskazini ndio nchi pekee duniani kuwa na udikteta wa kikomunisti wa kurithi. Nchi hiyo imetawaliwa na familia ya Kim kwa vizazi vitatu, huku kiongozi wa sasa akiwa Kim Jong-Un.

(8) Korea Kaskazini ni moja ya nchi maskini zaidi duniani, wastani wa Pato la Taifa kwa kila mtu ni karibu $1,800 pekee. Licha ya hayo, serikali inaripotiwa kutumia sehemu kubwa ya bajeti yake katika mpango wake wa kijeshi na silaha za nyuklia.
 
Kama ni kweli, siku moja wananchi watachoka hayo maisha, wajifunze kwa USSR na baadhi ya nchi zilizokuwa na misimamo hio, kwa kawaida asili ya mwanadamu hapendi kubanwa mpaka kupangiwq mitindo ya uvaaji na unyoaji wa nywele.

Raia wengi wanatamani kwenda Korea Kusini, waendelee na misimamo yao lakini wafanye namna wananchi wapate uhuru flani.

USSR kulikuwa kuna scientist vichwa kweli kweli, hawakuthaminiwa kwao na kazi zao lakini huko magharibi waliahidiwa kuishi maisha ya kifahari na kuheshimiwa. Mtu kahangaika kufanya tafiti na gunduzi mwishoni wanasema ni mali ya serikali, wengi walitoroka na hio ni moja ya sababu kubwa ya anguko la ukomunisti.
 
(10) Unapotaka kupiga picha sanamu au picha ya "viongozi wapendwa" wa nchi hiyo Kim Jong Il, Kim Il Sung na Kim Jong Un ni lazima upige picha sanamu zima au picha nzima, ni marufuku kupiga kipande au nusu picha. Ni marufuku pia kuchora katuni za viongozi hao.
Ukienda kwenye eneo la ujenzi ni marufuku kuwapiga picha wafanyakazi wanaoendelea na ujenzi wala kupiga picha jengo lisilokamilika, ni lazima upige picha jengo lililokamilika na lenye kupendeza.
Ni marufuku kupiga picha wanajeshi au kambi ya jeshi, hili ni sharti gumu kidogo kwasababu asilimia 25 ya raia ni wanajeshi.
Ni marufuku kutembea peke yako na kupiga picha maeneo yaliyoharibika kama vile barabara mbovu au maduka ambayo hayajajaa bidhaa. Serikali ya Korea Kaskazini inajitahidi ulimwengu upate picha ya kupendeza kuhusu nchi hiyo.
 

(1) Kalenda ya Korea Kaskazini inategemea mwaka wa kuzaliwa wa mwanzilishi wa nchi hiyo, Kim Il-Sung. Mwaka huu 2023, Korea Kaskazini itaadhimisha mwaka wa 112, kwa vile Kim Il-Sung alizaliwa mwaka 1912.

(2) Korea Kaskazini ina mfumo wake (operating system) kwenye upande wa computers zao, unaoitwa Red Star OS. Ni toleo lililorekebishwa la Linux na limeundwa ili kuwaweka watumiaji wote ndani ya nchi chini ya uangalizi.

(3) Korea Kaskazini ina time zone yake, inayojulikana kama ''Pyongyang Time'', ambayo iko dakika 30 nyuma ya Korea Kusini na Japan.

(4) Serikali nchini Korea Kaskazini imepiga marufuku mitindo fulani ya nywele, zikiwemo nywele ndefu za wanaume na mitindo fulani ya wanawake. Inasemekana kuna mitindo 28 pekee ya nywele iliyoidhinishwa na serikali kwa wanawake na 10 kwa wanaume.

(5) Nchini Korea Kaskazini, ni lazima kuvaa beji yenye picha ya mwanzilishi wa nchi hiyo, Kim Il-Sung, na mwanawe, Kim Jong-Il. Kukosa kufanya hivyo kunaweza kusababisha adhabu.

(6) Korea Kaskazini ina jeshi la watu milioni 1.2, ambayo ni ya nne kwa ukubwa duniani. Hata hivyo, nchi hiyo pia inajulikana kwa kuwa na vifaa vya kijeshi vilivyopitwa na wakati na visivyotunzwa vizuri.

(7) Korea Kaskazini ndio nchi pekee duniani kuwa na udikteta wa kikomunisti wa kurithi. Nchi hiyo imetawaliwa na familia ya Kim kwa vizazi vitatu, huku kiongozi wa sasa akiwa Kim Jong-Un.

(8) Korea Kaskazini ni moja ya nchi maskini zaidi duniani, wastani wa Pato la Taifa kwa kila mtu ni karibu $1,800 pekee. Licha ya hayo, serikali inaripotiwa kutumia sehemu kubwa ya bajeti yake katika mpango wake wa kijeshi na silaha za nyuklia.
(9)
JamiiForums1434033461.jpg
 
Kama ni kweli, siku moja wananchi watachoka hayo maisha, wajifunze kwa USSR na baadhi ya nchi zilizokuwa na misimamo hio, kwa kawaida asili ya mwanadamu hapendi kubanwa mpaka kupangiwq mitindo ya uvaaji na unyoaji wa nywele.

Raia wengi wanatamani kwenda Korea Kusini, waendelee na misimamo yao lakini wafanye namna wananchi wapate uhuru flani.

USSR kulikuwa kuna scientist vichwa kweli kweli, hawakuthaminiwa kwao na kazi zao lakini huko magharibi waliahidiwa kuishi maisha ya kifahari na kuheshimiwa. Mtu kahangaika kufanya tafiti na gunduzi mwishoni wanasema ni mali ya serikali, wengi walitoroka na hio ni moja ya sababu kubwa ya anguko la ukomunisti.
Mbona wewe umepangiwa kuvaa nguo nanumekubali?
 
Back
Top Bottom