Umefanya nini toka Januari 2015 hadi Disemba?

Umefanya nini toka Januari 2015 hadi Disemba?

nimemnyanganya power bank dada Niliemhonga, nimeacha rasmi kumfatilia mtoto wa Mwenye nyumba, nimebakiza somo moja CPA, Nimefanya pepa ya IFRS
 
Nakumbuka siku ya tarehe ya mwisho na dakika ya 59 kabla ya kuingia mwaka mpya wa 2015, nilisha kata tamaa tangu awali. Niliupokea mwaka nikiwa mwingi wa mawazo na huzuni, hii ni zaidi ya kumbukumbu kwangu, nilikuwa mtu asie kubalika na watu, mpweke na mnyonge, nikiwa na matumaini ya kuuanza mwaka mwingine ovyo ovyo tu kama mingine mingi tu iliyopita, aah la hasha,2015 ni mwaka bora sana katika historia yangu, mwezi wa kwanza tu niliteuliwa nafasi za uongozi mara kumi, yaani kazini, mtaani, kwenye vyama, sijui kanisani, mara kwenye maproject makubwa, muda mwingine usimamizi, watu wamenikubali na kuniamia kupita kiasi. nimepata kazi ambayo ni moja ya ndoto zangu, Ofisi binafsi, ujenzi tena ambao ulishindikana kwa miaka kumi sasa, sasa umekamilika, certificate safi kabisa katika course nilizokua nafeli miaka yote,kufanya kazi na makampuni makubwa niliokuwa nayasikia redion tu, kuweka ahadi kubwa kubwa na viapo vizito, nimenunua set 2 computer new model, kumiliki card nying za benk, Kutimiza ndoto yangu ya kuwa na libraly binafsi ya vitabu, kujua mambo maelfu kuusu watu na ulimwengu wote huu katika app bomba na kivutio kikubwa kwangu JAMIIFORUMS.
all in GOD i truth
 
Namshukuru Mungu kanipigania nmemaliza mwaka wa kwanza chuo salama ingawa nilikumbana na changamoto nyingi mwanzon mwa mwaka
 
God has been good kwangu kwa mwaka 2015..tangu nizaliwe sijawahi kuwa na furaha na matumaini kama mwaka huu. Kwa miaka 27 tu mshahara wangu umepanda mpaka kufikia milioni moja, nina plan ya kukopa pesa ambayo sijawahi ishika maishani mwangu, nyumba imeisha bila msada wa mkopo, nina amani, nina likizo ya masomo kazini nikiisaka shahada ya uzamili,

Lucky and happiness are smilling at me...mwaka huu ndio nimeamini Mungu anatuona na anatujua mahitaji yetu...he gave me underserving favour.

Ushukuriwe sana MUNGU uliyezitanda mbingu na nchi. The most high, lord of lords and king of kings.

Hallelujah!!
 
Daah kwangu haukua mwaka mzuri sana lkn cna jinsi yote mema mpangaji ni mola!!, nlitaman sana kufunga ndoa lkn haikua najpanga tena 2016 nioe
 
Sijafanya lolote mimi sababu desemba bd sana
 
Back
Top Bottom