Umeelewa nini hapa? Usiogope funguka

MstahikiMeya

JF-Expert Member
Jan 8, 2014
1,633
559
Tofauti ya BIASHARA na SIASA
ikila hasara inaweza buma
wakati SIASA kila mara ukiwa
unang’ara ujue kuna
kinara anayeunda msafara wa
wanaojituma na
kuchuma kwa kukufanya uwe
imara hapo hasara hakuna

KIDUMU CHAMA CHA MASELA…
Ukoloni mambo leo umetupa
uhuru wa bendera
tuone kufuru za wenye hela

TANZANIA ni ‘ demu wa mtungo ‘
wanamuiita CHA WOOTE’’
HANGOVER .. ‘’anaikimbia kwa
kupiga ‘ “ mtungi “ saa zote

Mkubwa anazuga atasolve…
matatizo ya nchi yake
‘’na gari bovu..’’ halisukumwi kwa
kukaa ndani yake

MAENDELEO ni ile
ndoto..MWEZEKAJI ashaipuuza
je Kukaa karibu na moto ni kuuota
au kujiunguza

hakuna UHURU wa kweli (Africa)
msidanganywe na illusion
na daily tunafeli sababu ya
POLITICAL institutions
CIVILIZATION imeadvance sasa
wanatuua economically

hakuna utumwa mbaya kama ule
wa kujiona uko free
Kuusaka ukweli ni sawa na
kumenya kitunguu
kila ganda litakutoa machozi na
utabaki macho juu
Ukishafika kwenye kiini niambie
nini utagundua
zaidi ya mafaili yaliyounganika
utaghairi kuyafunua

Wamejivisha U-NOAH.. SAFINA zao
zikatoboka
Wakajivisha U-MUSSA.. FIMBO zao
hazikugeuka NYOKA
sasa wanaujaribu Umungu mtu
kuamua leo nani atatoka
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom