Ulivyokuwa na Miaka 14 ulikuwa wapi? Mjue Kairan Quazi, Genius wa SpaceX

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,026
1,621
1686555816213.png



Ulivyokuwa na Miaka 14 ulikuwa wapi? Mjue Kairan Quazi, Mfanyakazi wa Elon mwenye Umri mdogo
zaidi

Genius huyu ameteka vichwa vingi vya Habari baada ya kupost kwenye ukurasa wake wa Linkedin kuwa ameajiriwa kwenye kampuni hiyo ambayo haikujali umri wake

Kairan Quazi, mvumbuzi wa programu (software developer) mwenye umri wa miaka 14, amekuwa mfanyakazi mdogo zaidi katika kampuni ya anga ya Elon Musk, SpaceX

Kairan Quazi ni nani??? Kwa ufupi kabisa

Akiwa na umri wa miaka miwili tu, alikuwa akizungumza kwa sentensi kamili. Kadiri alivyosonga mbele katika shule, walimu wake na wenzake waligundua haraka uwezo wake wa kushangaza wa kusimulia habari alizosikia kwenye Redio, hata akiwa bado anasoma darasa la awali.

Wakitambua kwamba Kairan anahitaji masomo ya juu zaidi ili kupata changamoto za kutosha, wazazi wake, mwalimu, na daktari wa watoto waliamua kutafakari uwezekano wa kuvushwa darasa

Hata hivyo, kupata chuo kikuu ambacho kingekubali kumchukua kilikuwa changamoto. Hatimaye, alipata mahali katika Chuo cha Las Positas huko Livermore, California, ambapo alianza safari yake ya elimu.

Kuhitimu shahada kutoka Shule ya Uhandisi ya Chuo Kikuu cha Santa Clara na kujiunga na SpaceX kama muhandisi wa programu akiwa na umri mdogo kama huo ni ushahidi wa kipaji chake cha kipekee

Mara nyingi watu huhitaji ufafanuzi kuhusu jinsi mtu mchanga kama Kairan anavyoweza kumudu majukumu na matarajio ya kufanya kazi katika kampuni yenye hadhi kubwa kama SpaceX.

Hata hivyo, umri wake haupaswi kuonekana kama kikwazo, bali kama chachu kwa wengine. Hadithi ya Kairan inaonyesha kwamba umri haupaswi kuwa kikwazo katika kufuatilia na kutumiza ndoto zako katika kuleta mabadiliko chanya katika Jamii
 
14 years ndo wengi tulikuwa darasa la 6 au la 7 na wachache form 1. Inatokea mara chache duniani, labda 1 kwa laki moja kuwa na vipaji vya namna hiyo. Wanasema Mungu aliwapenda zaidi average people kama wewe na mimi ndo maana akatuumba kwa wingi.
 
View attachment 2654815


Ulivyokuwa na Miaka 14 ulikuwa wapi? Mjue Kairan Quazi, Mfanyakazi wa Elon mwenye Umri mdogo
zaidi

Genius huyu ameteka vichwa vingi vya Habari baada ya kupost kwenye ukurasa wake wa Linkedin kuwa ameajiriwa kwenye kampuni hiyo ambayo haikujali umri wake

Kairan Quazi, mvumbuzi wa programu (software developer) mwenye umri wa miaka 14, amekuwa mfanyakazi mdogo zaidi katika kampuni ya anga ya Elon Musk, SpaceX

Kairan Quazi ni nani??? Kwa ufupi kabisa

Akiwa na umri wa miaka miwili tu, alikuwa akizungumza kwa sentensi kamili. Kadiri alivyosonga mbele katika shule, walimu wake na wenzake waligundua haraka uwezo wake wa kushangaza wa kusimulia habari alizosikia kwenye Redio, hata akiwa bado anasoma darasa la awali.

Wakitambua kwamba Kairan anahitaji masomo ya juu zaidi ili kupata changamoto za kutosha, wazazi wake, mwalimu, na daktari wa watoto waliamua kutafakari uwezekano wa kuvushwa darasa

Hata hivyo, kupata chuo kikuu ambacho kingekubali kumchukua kilikuwa changamoto. Hatimaye, alipata mahali katika Chuo cha Las Positas huko Livermore, California, ambapo alianza safari yake ya elimu.

Kuhitimu shahada kutoka Shule ya Uhandisi ya Chuo Kikuu cha Santa Clara na kujiunga na SpaceX kama muhandisi wa programu akiwa na umri mdogo kama huo ni ushahidi wa kipaji chake cha kipekee

Mara nyingi watu huhitaji ufafanuzi kuhusu jinsi mtu mchanga kama Kairan anavyoweza kumudu majukumu na matarajio ya kufanya kazi katika kampuni yenye hadhi kubwa kama SpaceX.

Hata hivyo, umri wake haupaswi kuonekana kama kikwazo, bali kama chachu kwa wengine. Hadithi ya Kairan inaonyesha kwamba umri haupaswi kuwa kikwazo katika kufuatilia na kutumiza ndoto zako katika kuleta mabadiliko chanya katika Jamii
Yaani mimi nina shida kichwani. Nikipata mtoto wa miaka miwili na ana uwezo kama alivyokuwa huyu pindi alipokuwa na umri huo, kuna uwezekano hata nikamharibu akili yake; maana nitampenda kupitiliza
Mungu ambariki sana huyu mtoto
 
14yrs 2012 nilikuwa kidato cha pili, natoroka shule naenda kucheza playStation.
 
Back
Top Bottom