Aisee niliwahi pata kisa kama chako, nafika tu form 5 moyo ukadondokea kwa binti mmoja wa shule ya jirani! Yeye alikuwa form 2..
Nilifanya jitihada zote nimpate, hakuonesha interest yeyote na mimi, kidume nakomaa lakini wapi (story yake naweza andika kitabu), mengi nilipitia na mengine ya aibu hata kusimulia, ningefanyeje na moyo ushapenda, miaka miwili yote mpka naondoka ule mji mambo yalikuwa bila bila ila atleast nilikuwa na namba yake!
Baada ya kuondoka kule akaja akanikubalia, nadhan ile kutaka kuniridhisha tu maana nilikuwa mbali na sina madhara, kuna kipindi nikiwa nshaanza chuo nikamfunga safari kumfuata, dah yan alinikana hadharan akadai hata kusema ananipenda huwa anajilazimisha tu, nilijibebesha mwenyewe maua na kadi, ikabidi nimpe tu, pengine aliyatupa huko mbele ya safari.
Nilipiga moyo konde, nikaamua kusonga mbele..sikupanga kumtafuta tena na yeye alijua hilo, na akabaki kimya. Miaka ikaenda nikamaliza chuo, nikawa nshaanza kazi na maisha yanaendelea.
Basi siku moja napokea simu akajitambulisha kwamba ni yeye, story zikawa nyingi kama huyo prisca wako, akauliza kama nshaoa na akadai eti ananipenda

Nikaona isiwe kesi, nikamuuliza nitaamini vipi sasa, akadai anakofanya kazi ana likizo tayari hivyo kabla hajaenda kwao atasafiri kuja kwangu atakaa wiki.
Sikuwa na kipingamizi, alisafiri na akapika na kupakua wiki nzima, kiukweli nilikuwa bado nampenda ila target yake kuu niliiona ni kuolewa maana ndan ya hiyo wiki akataka anitambulishe kwa baba ake, niliwaza sana na nilichokuja kugundua ni kwamba mambo yake hayakwenda vile alivyopanga hasa baada ya kufeli form 4,hivyo akaona mimi ndo option ya mwisho kwake.
Baada ya wiki aliondoka na ndo ukawa mwisho wa story, miaka 8 sasa imepita bado sijapata mbadala wake, bado najuta kwanini sikujenga naye maisha, hasira ziliniponza maana kuna ajabu gani mtoto wa o level kukukataa!
Mkuu fuata moyo wako, kama unampenda mchukue tu.. mimi nataman siku zirudi nyuma ila ndo hivyo haiwezekani!