Ulishawahi kuwa na marafiki wa aina hii?

Dejane

JF-Expert Member
Jan 1, 2014
49,661
68,636
Ushawahi kuwa na rafiki kila siku ana shida yeye, analalamika yeye tu akiwa na shida haraka kwenda.

Rafiki anataka kukugeuza kama chawa wake hivi. Kukopa sasa pesa ndio usiseme
Ulifanyaje ulivyokuwa na rafiki wa hivi muda wote analalamika anaona humtendei vyema tu.
 
Kwa maisha ya Kitanzania ni wengi wanapitia hali hiyo kutokana na ugumu wa maisha.

Hali kama hiyo pia huwa inawakuta mabinti wale walioolewa kisha hawasaidiwi mahitaji yao na waume zao.

Wengine ni hulka zao tu kuwa hivyo. Nimeshawahi kufanyakazi na watu wenye tabia hizi. Unatakiwa usiwachukie ila unatakiwa uwasaidie kuondokana na hii Sonona ya kimaisha
 
Huo ni mzigo, ubebe uone kama ni size yako, ukiona mzito utue chini haraka sana
 
Njia rahisi ya mtu anayekukwaza ni kumchana tu ukweli wa pale anapozingua, akinuna akakaa kimya ndiyo anakuwa amekusaidia..!

Mkiendelea, kuna namna naamini atakuwa kajifunza hii itamsaidia kupunguza speed...!
 
Sisi wanaume huwa 'tunawatema' washikaji wa namna hiyo...

Maana kuna raia utadhani watoto yatima, na wana tarehe zao hizo utaanza tu kuona stori zinabadilika badilika malalamiko ya kifedha yanaongezeka...

Ukiacha washikaji pia kuna ndugu wale wa "niazime laki, 50k n.k nitakurejeshea mambo yangu yakikaa sawa"
 
Mimi sihitaji marafiki wa hivyo. Binafsi nina marafiki wachache sana na ni wa muda mrefu sana.

Kwanza hata mtu akitaka kuwa na urafiki na mimi, lifestyles yangu itamshinda atajitoa tu mwenyewe.

Maana:

  • Situmii pombe
  • Situmii sigara
  • Situmii ugoro
  • Sibet
  • Si mshabiki sana wa mpira
  • Sivuti bangi
  • Siyo mtu sana wa parties ( Birthdays, night clubs n.k )
  • Siyo movie enthusiasist
  • Kanisani nina muda sana sijaenda

Sasa kwa hali hiyo, utakuwa na urafiki na mimi utaweza ?
 
Waswahili wengi hamjui rafiki ni nani..
Kuna washkaji.
Kuna majirani.
Kuna Ndugu na jamaa
Kuna workmates..

Halafu kuna Rafiki..

Sasa unatakiwa mtu kabla hajatoka huko..
Kwenye jirani au Ndugu na jamaa au workmates uwe ushamjua kabla ya kumfanya rafiki....

Kwa wanawake rafiki kama huyo usikute keshakuuza sana bila wewe kujua..
Kama ana njaa kutwa na mtu anakutaka
Atashindwa kupokea hela kutoa namba yako?
Au kupokea hela na kukupelela sehemu.?
Anajifanya nisindikize Tu mara moja kumbe
Kapewa hela anakufikisha sehemu anapotea..

Mnakuwaje na marafiki kama hao??
 
Rafiki ni watu walioshbana wenye kupendana na kusaidiana kwenye kila hali unayemzungumzia siyo rafiki ni mpigaji
 

Tatzo lake kukopa sana na yeye ndio ana shida muda wote
Nimeshindwa aisee nimemchana tumeachana
 

Heheheh ukikopwa je?
 

Ukiwa rafiki na mtu inatakiwa kubalance mambo na kutokuwa negative sana
 

Unawasaidiaje wakati nawe una na shida kibao
Kupokea simu yake unaogopa unajua tu ni lawama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…