Dah,
Ahsante Utumishi.
Nimeenda kupiga pepa Dodoma, intavyuu ya TRA tuko mtu nyomi. Kusema ukweli hili nyomi nililitabiri tu, hivyo nikakata kabisa gari ya kwenda na kurudi, na kuna binamu yangu mmoja anaishi Dodoma nikamuomba anifanyie booking ya room. Ingawa alitaka nilale kwake.
Niliingia Dodoma ijumaa saa kumi na moja jioni nkamkuta binamu stand ananisubir. Alimaindi why sikutaka kulala kwake nkamwambia niko poa tu, gharama asijali, alinichukua mpaka lodge aliyonifanyia booking nkapumzika hapo nimechoka hoi. Lodge iko nyuma ya Pub ya Platnum pale opposite ghorofa za NHC.
Saa moja usiku nkasema ntoke nkatafute mlo ili nirud nije nisome "possibles" za pepa ya kesho yake. Wakati natoka mapokezi nkakutana na mdada anashuka kwenye bodaboda, yule dereva anamwambia wajaribu pale labda watapata. Yule dada akaanza kulalamika why Utumishi wameamua kuleta pepa huku Dom, hapo nkajua kumbe yule dada ni "mwenzangu".
Nlimwambia Mimi pia ni mpiga pepa mwenzie, hivyo kama hatojali basi aniamini tu tuwe kampani asiendelee kuzunguka, mji umejaa. Alinielewa, nikarud nae ndani kuweka begi lake kisha nikatoka nae. Pale lodge ni karibu na Chako ni Chako ambako tulienda kupata menu tukarud kujadili pepa la kesho. Tulionyeshana vitambulisho ili tutambuane na kuaminiana zaidi, aliniambia katokea Tanga.
Pepa tumejadili weeee, mpaka saa saba usiku tukaamua inatosha. Tulikua free tu kujadili kana kwamba ni watu tunaojuana kitambo. Tulipeana uzoefu mbalimbali juu ya pepa za TRA zinavyokua. Dodoma wakuu ni barid sana usiku, yaani utadhani umeweka AC mpaka ile lowest temperature 15°. Kwakua ilikua usiku sana tuliamua tulale tu Sasa tusubir hiyo asubuhi. Kwenye kuoga kila mtu alioga kivyake, kuvaa unajitanda shuka kisha unageukia ukutani ndo unavaa. Kulala ilikua ni Mzungu wa Nne.
Sintoeleza ya kwenye pepa maana yapo humu, ila jioni tulikutana tena pale lodge. Hapa sasa hatukua na obligation yoyote zaidi ya kujiandaa kwa kesho kurud makwetu. Tulisema tuzunguke tuone mji ulivyo tukaingia viwanja kadhaa. Vinjwaji pia havikukoseka huko viwanjani. Tulirud kwenye saa nane hivi usiku, Pombe hazina adabu na Dodoma ni baridi hivyo kimasihara masihara tunda likamegwa. Sikumtongoza, hakunitongoza bali automatically tu tukajikuta tunajiliwaza kwa kumaliza pepa.
Zilipigwa game kadhaa usiku huo ili kujaribu kushindana na baridi, lakini mwishowe tuliamua tupumzike tu, maana ni ngumu kushindana na nature. Mtoto alikua "fundi" Sana nkasema nitaenda tu Tanga one day kwa ajili ya Mechi ya marudiano. Gari yangu ilikua saa tisa mchana, yeye saba mchana. Hivyo tulipata wasaa wa kupiga story hiyo asubuhi.
Ahsanteni Tena Utumishi.