Ulishawahi kukutana na mtu aliyevaa nguo zinazofanana na zako? How did you react to it?

Nilishawahi onana na watu wawili kwa wakati tofauti wamevaa gauni za kitenge kama zangu yaani Hadi mshono.

Nilishawahi kuonana na mtu amevaa gauni ya mtumba kama yangu vilevile

Nishawahi onana na mtu amevaa blauzi ya mtumba Kama yangu

I was so excited
 
Nilikua natoka zangu hostel naenda class nimepiga suruali nyeusi na shati fulani hivi za njano (ya duka), wakati nikiwa njian nikakutana na jamaa kavaa vile vile, nikapuuza baada ya hatua chache nikakutana na watu wengi wakiwa wamevaa vilevile dah nilistuka sana.kumbe walikua wanakwaya aisee na ilikua ni siku ya jumapili. nilikosa amani kutwa nzima. nilivyorudi kitaa(likizo) nikampa dogo na nikaapa kutokuja vaa nguo za duka tena.
 
Kuna rafiki yangu mmoja iliwahi kumkuta hii, ilikuwa back in 2005 alikwenda kupiga picha, kipindi Photo studio dili sana. Alipiga picha akiwa amevaa T.shirt yake flani hivi, made in Malaysia na hakuweka pozi lolote zaidi ya kukaa tu juu ya stuli. Kumbe kuna jamaa mwengine nae alishawahi kufika pale na kupiga picha tena ikiwa hata mavazi walivaa sare. Kwa bahati mbaya siku ya pili tulikwenda wote kufata picha zake Picha zilikuwa hazikutoka fresh ziliungua!! Muda si muda na yule jamaa mwingine nae alifika na kuziona zile picha, basi hapo ukawa ugomvi mkubwa sana, kila mmoja akisema zile picha ni zake
Busara za mpiga picha ndio zilimaliza ugomvi baada ya kuwataka wote wapige picha upya ila kiukweli pia walikuwa wanamfanano isipokuwa rafiki yangu nywele zake zilikuwa fupi sana.
 
Kuna jamaa alinipa kaunda suti yake bure anayotokelezea ofisini akasema inambana. Siku mbili badae nikasikia kwa mshikaji eti jamaa kanipa suti baada ya kuniona eti nimevaa suti kama yake halafu nimekaa chini nasuka mkeka (nabeti). Jamaa hajui kama kazi yangu ni sawa tu na yake tofauti yeye anatumia elimu. Kwa hasira na mimi nikaigawa bure suti yake kwa muuza juice ya miwa. GG ikawa imetoa tayari.
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Sio kila muda tunapaswa kusoma na kujadili makala zinazohusiana na masuala ya Cold War, jeshi na ujasusi wa KGB. Leo ngoja tujadili kidogo changamoto za maisha katika jamii tunamoishi.

Eti ndugu zangu Watanzania;

HUMAN BEHAVIORAL PSYCHOLOGY.
============
Ulishawahi kukutana na mtu ghafla (kwenye sherehe, daladala au njiani) aliyevaa nguo zinazofanana na za kwako? How did you react to it? mlipungia mkono, mlipeana tabasamu, mlimfuata kumsalimia au ulikwepesha macho?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

BIASHARA: Ninauza Vitabu Vya Kujifunzia Lugha Ya Kijerumani. Ich komme aus der Stadt Dar Es Salaam und verkaufe diese Deutsch-Lernbücher
Hua nachukia sana ndomaana napenda kuvaa mtumba
 
Mimi haikuwa nguo bali magari..zote zilikuwa
Make: Toyota Cresta
Model: GX 90
Color: Silver
Registration: T800ABJ , T800ADJ
nilikuwa wa kwanza kupaki nikaingia duka la spare...akaja jamaa akapaki sawa sawa na mimi naye akaja dukani
Sikuwa makini kuhusu gari yake hivyo nilipanda yangu na kutaka kuondoka ...ghafla nikamuona jamaa keshajaa mlango wa dereva anapiga kioo..alidhani nimeiba gari yake
Nikapaki nikashuka ..kwa dakika nzima wote tulichanganyikiwa mpaka tulipokuja kuona tofauti ya number
Mpaka rims zilifanana...
Hi ilinitokea pale kituo cha garage External mwaka 2009

Yeye aliikuta gari yako iko pale tayari. Ina maana hakuiona? Wakati wewe unaanza kuondoka alikuwa haoni kama kulikuwa na Toyota Cresta nyingine maeneo alipoacha gari yake?
 
Nafananishwa sana, nilienda polisi pale kariakoo yaani niliitwa jina afande ...... na nilihudumiwa haraka mno.

Polisi tena hapo loliondo niliitwa jina la mama fulani na kuulizwa habari za dodoma, nilihudumiwa na nauli walinipa, mmh nilivyoondoka nakasema wasije shituka duuu,

Nafananishwa siyo kawaida.
 
Nimewahi kukutana nae, cha ajabu zilikuwa za mtumba. Tulipungiana huku tunacheka
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Sio kila muda tunapaswa kusoma na kujadili makala zinazohusiana na masuala ya Cold War, jeshi na ujasusi wa KGB. Leo ngoja tujadili kidogo changamoto za maisha katika jamii tunamoishi.

Eti ndugu zangu Watanzania;

HUMAN BEHAVIORAL PSYCHOLOGY.
============
Ulishawahi kukutana na mtu ghafla (kwenye sherehe, daladala au njiani) aliyevaa nguo zinazofanana na za kwako? How did you react to it? mlipungia mkono, mlipeana tabasamu, mlimfuata kumsalimia au ulikwepesha macho?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

BIASHARA: Ninauza Vitabu Vya Kujifunzia Lugha Ya Kijerumani. Ich komme aus der Stadt Dar Es Salaam und verkaufe diese Deutsch-Lernbücher
Hata mm syo nguo... Ila Nishawahi kubananishwa
Border ya TNDMA, siku 2 pale nilifafanishwa na mtu ambaye kumbe ni mtu wa msalaa
Majina tu tofauti.... Kilichonisaidia vitambulisho
Dunia wawili wawili
Nkirudi kwenye uzi wako Sasa, unaweza ukafanya jambo kumbe Kuna mwanadam Mwenzako kwengine
Anafanya hivyo hivyo

Ova
 
mimi nikikutaga mtu ana drive gari kama yangu kwasababu ni unique huwa nampiga taa ile ya salam wengi huwa wanaelewa wana reply
Hii kawaida,hata kama unataka kuingiza gari kwenye foreni wewe ukiona gari model sawa na yako mpige taa...anakupisha
 
Mimi nilikutana na mtu tunafana sura,urefu ,skin color, hadi jina la mwanzo hadi leo tumekua brothers japo ni koo mbali mbali kabisa
Nilipoingia form one nilimkuta mkaka wa form three anafanana na kaka yangu vibaya mno, yaani kila kitu kasoro rangi ye alikuwa maji ya kunde. Yaani kila nikimuona ilikuwa lazima nizubae kumuangalia. Nikajua labda macho yangu siku moja nimeingia staff walimu wakaniuliza J ni kaka yako?? Nikasema hapana. Wakasema kama sio kaka yako ni nani yako? Maana haiwezekani muwe hamhusiani kabisa
 
mimi nikikutaga mtu ana drive gari kama yangu kwasababu ni unique huwa nampiga taa ile ya salam wengi huwa wanaelewa wana reply
Yaani wanaelewa kuwa ni salamu ya kufanana kwa model ya gari, sijui na rangi (check kwenye red)?
 
Back
Top Bottom