Gustavo Gaviria
JF-Expert Member
- Nov 19, 2018
- 630
- 1,109
Wakuu tupo pamoja.
Mimi hapa nina mwanamke mmoja bwana ana mtoto mmoja ila sio wangu nataka kumuoa, nimeridhia kabisa na nimempenda mwanamke licha ya kuwa na mtoto, ila kipengele kinakuja kwenye familia sidhani kama watanielewa! na hata kama watanielewa sidhani kama watatoa ushirikiano ipasavyo...navyoona wataniona bwege la kutupwa kulingana na uchaguzi wangu...yaani naona uchumba hapo ndio kizingiti kilipo na utafia hapo! hapa nawaza tu nimwambie mchumba aendelee na maisha yake nisimpotezee muda au nikaushe tu, tatizo ninampenda sitaki kabisa kuachana naye.
Nikimwambia ugumu utakaokuwepo nahisi ndio itakuwa mwisho wa mahusiano na mimi bado namhitaji...haya nikisema kumwambia baadae nitakuwa nimempotezea muda, yaani ni kizunguzungu, ninachojua familia yangu haitopendezwa kabisa mimi kuoa mwanamke aliye na mtoto wa mtu mwingine, ila mimi ndio nimeshampenda.
haya endapo nikimwambia kuwa hilo suala la yeye kuwa na mtoto tulifiche, itakuwa sio rahisi maana kutakuwa na muingiliano wa familia na itajulikana tu.
Je Mwanamke au Mwanaume ni changamoto gani ulipitia katika kumtambulisha Mwenza wako katika familia yako yaani baba mama na ndugu zako?
Tiririka kisa chako tupate uzoefu, naamini sio mimi tu niliyepo katika hili.
Mimi hapa nina mwanamke mmoja bwana ana mtoto mmoja ila sio wangu nataka kumuoa, nimeridhia kabisa na nimempenda mwanamke licha ya kuwa na mtoto, ila kipengele kinakuja kwenye familia sidhani kama watanielewa! na hata kama watanielewa sidhani kama watatoa ushirikiano ipasavyo...navyoona wataniona bwege la kutupwa kulingana na uchaguzi wangu...yaani naona uchumba hapo ndio kizingiti kilipo na utafia hapo! hapa nawaza tu nimwambie mchumba aendelee na maisha yake nisimpotezee muda au nikaushe tu, tatizo ninampenda sitaki kabisa kuachana naye.
Nikimwambia ugumu utakaokuwepo nahisi ndio itakuwa mwisho wa mahusiano na mimi bado namhitaji...haya nikisema kumwambia baadae nitakuwa nimempotezea muda, yaani ni kizunguzungu, ninachojua familia yangu haitopendezwa kabisa mimi kuoa mwanamke aliye na mtoto wa mtu mwingine, ila mimi ndio nimeshampenda.
haya endapo nikimwambia kuwa hilo suala la yeye kuwa na mtoto tulifiche, itakuwa sio rahisi maana kutakuwa na muingiliano wa familia na itajulikana tu.
Je Mwanamke au Mwanaume ni changamoto gani ulipitia katika kumtambulisha Mwenza wako katika familia yako yaani baba mama na ndugu zako?
Tiririka kisa chako tupate uzoefu, naamini sio mimi tu niliyepo katika hili.