Ulinzi wa Faragha ya Taarifa Binafsi ni Haki ya Msingi ya Binadamu

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938

1674453071578.png

Siku ya Ulinzi wa Faragha ya Taarifa Binafsi (Data Privacy Day) inaadhimishwa kila Januari 28

Haki ya Faragha inawezesha Raia kufurahia Haki nyingine kama:

- Uhuru wa Mawazo

- Uhuru wa Kujieleza

- Uhuru wa Kukusanyika

Ni Msingi wa Jamii ya Kidemokrasia

Katika Nchi nyingi, Faragha inatambulika kama Haki ya Msingi ya Binadamu, na Sheria za Kulinda Taarifa Binafsi zipo ili kuilinda

Ibara ya 16 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema, "Kila Mtu anastahili kuheshimiwa na kupata Hifadhi kwa Nafsi yake, Maisha yake Binafsi na Familia yake na Unyumba wake, na pia Heshima na Hifadhi ya Maskani yake na Mawasiliano yake ya Binafsi"

Ili Watu washiriki kikamilifu Mitandaoni, wanahitaji kuamini Taarifa zao Binafsi zipo salama

Bila Kulinda Faragha, tunaweza kuwa hatarini kutengeneza Jamii isiyoweza Kujieleza kwa Uhuru, suala ambalo ni Ukiukwaji wa Haki za Binadamu

FARAGHA YA TAARIFA BINAFSI NI NINI?
Ni Haki ya Msingi ya Binadamu kwa Mujibu wa Ibara ya 12 ya Tamko la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa la Mwaka 1948

Inahusisha Wananchi kuwa na Udhibiti wa jinsi Taarifa zao Binafsi zinavyokusanywa, kuhifadhiwa na kutumika. Taarifa hizo ni pamoja na Jina, Jinsia, Namba ya Simu, Baruapepe, Makazi, Taarifa za Kiafya na Kifedha

Haki hii ambayo ipo Kikatiba pia inalindwa na Mikataba mbalimbali ya Kikanda ambayo Tanzania imeridhia

1674453174385.png

KWANINI HAKI YA FARAGHA NI MUHIMU?

Taarifa Binafsi zinaweza kutumika vibaya ikiwa hakuna Kanuni na Taratibu za kuziweka salama

Faragha inapotambulika kama Haki ya Msingi ya Binadamu, wale wasioiheshimu huwajibishwa

Mtu anayekosa Ulinzi wa Faragha ya Taarifa zake anaweza kushindwa kufurahia Haki nyingine kama Kutoa Maoni kwa Uhuru

FANYA HAYA KULINDA TAARIFA ZAKO BINAFSI

1) Kumbuka Mlinzi wa kwanza wa Taarifa zako ni Wewe. Unapotoa Taarifa zako Mtandaoni au nje ya Mtandao, unajiweka katika hatari zaidi ikiwa zitatumiwa vibaya

2) Epuka kubonyeza 'Link' usizozifahamu kwani Wahalifu wengi kwenye Mitandao hutumia mbinu hiyo kujaribu kuingilia Faragha yako

3) Sasisha (Update) Programu zako ili kuboresha Usalama wa Vifaa vyako vya Kidigitali na kujilinda dhidi ya mianya inayoweza kuathiri Faragha ya Taarifa zako

ZINGATIA YAFUATAYO KUIMARISHA ULINZI WA TAARIFA ZAKO
  • Funga Akaunti zisizo na Matumizi: Akaunti zisizotumika na kusimamiwa ipasavyo Mitandaoni bado zinaweza kuwa na Taarifa Binafsi ambazo zinaweza kutumiwa vibaya
  • Weka Nywila (Password): Fanya hivi katika Vifaa vyako vya Kidigitali na Akaunti zako za Mitandao ya Kijamii. Kumbuka kuwa na Nywila Imara na jitahidi kuhakikisha hazifanani
  • Epuka 'WiFi' za Umma: Wahalifu wanaweza kuitumia kuingilia Kifaa chako kupitia 'WiFi' zisizo salama na kuingilia Faragha ya Taarifa zako
FARAGHA MTANDAONI: JENGA TABIA HIZI KUWA SALAMA

(i) Epuka Programu au 'App' ambazo hazieleweki: Asilimia kubwa zinachukua Taarifa zako bila ridhaa hivyo kuingilia Faragha yako

(ii) Tumia 'Two-Factor Authentification' pale unapoweza ili kujenga Usalama zaidi unapoingia kwenye Akaunti mbalimbali Mitandaoni

(iii) Weka Mikakati ya endapo utapoteza Simu au Kifaa chako cha Kidigitali ili Taarifa zako zibaki Salama

MUHIMU:

UKUSANYAJI TAARIFA BINAFSI:
Ni muhimu kuwepo kipimo/kiwango cha Taarifa zinazochukuliwa

KWANINI TAARIFA ZAKO BINAFSI ZINACHUKULIWA?: Ili kulinda Faragha yako, usisite kuuliza Matumizi ya Taarifa zako pale unapohitaji kufanya hivyo. Ni HAKI yao kufahamu!

MATUMIZI SAHIHI YA TAARIFA: Taarifa zetu Binafsi hazitakiwi kutumika kwa Masuala mengine tofauti na lengo husika

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI: Ni muhimu kuwepo na Miongozo kuhakikisha Taarifa zipo salama

UWAZI: Ukusanyaji wa Taarifa Binafsi usifanyike kisiri. Wananchi wafahamiwe kuhusu Michakato inayohusisha Taarifa zao

UWAJIBIKAJI: Yeyote anayehusika na Ukusanyaji wa Taarifa awajibishwe ikiwa Misingi ya Faragha haitazingatiwa

SOMA VIGEZO NA MASHARTI: Kabla hujakubali kutumia App au Tovuti husika, ni muhimu kusoma Vigezo vyake ili kujihakikishia usalama
 
Back
Top Bottom