Ulimwengu wa 3D na 4D

Ulimwengu wa 3D na 4D

Imeharibu hata ladha ya JF

ni kweli kabisa
Jukwaa siku hizi limeharibika, hakuna cha kujifunza ila ni ubishi tu
mtu kapata smartphone kajiunga JF basi atataka anachookota huko barabarani akilete humu na asipingwe atabishaa mpaka saver ijae.
hata kuchangia au kuelimishana elimu tulizozipata tunashindwa maan hujui unayewboshana naye ni kichaa au gwiji aliyebobea
sasa 4D na YOGA au NDOTO na Medidation ni wapi na wapi
 
Tukubali tusikubali ... watu wengi ni wavivu wa kufuatilia mambo. Kikundi kidogo tu cha watu ndo wanafuatilia mambo na hao wanajua mengi zaidi na zaidi .. waliobaki wanakuwa bendera fuata upepo tu.
Hata wewe unayesoma hapa uliwahi kujiuliza swali hili ... "mkono kwa ajili ya kulia chakula ni mkono wa kulia" nani aliweka utaratibu huo?
 
Kila kitu kimegota na kusimama kwenye hiyo meyiiiiii meyiiiii.kw hiyo hata km utafuata hayo maelekezo mengine lkn ukakosea kwenye hiyo meyiiiii meyiiiii.hutafanya lolote.hivyo meyiii meyiiii ndio kila kitu.
Sometimes huwa nikisoma post nyingine nacheka hata nikiwa peke yangu .... ebu ijaribu hiyo Meyiiiiiii uone kama ina madhara yoyote.
 
Chochote kile unachokijua ni kwa sababu ulijifunza, hii inamaanisha kuwa ulichozaliwa nacho ni uwezo wa kujifunza tu. Tatizo uwezo huo unaendelea kupungua pale unapoendelea kuwa na umri mkubwa.
Mtoto mdogo uwezo wake wa kujifunza ni mkubwa sana kwa sababu kichwani kwake hana mrundikano wa mambo mengi. Wewe hapo kutokana na mrundikano wa mambo mengi ndiyo maana unakomaa na kubishia vitu vya ukweli eti mpaka upate evidence ... evidence ipi kwa vitu visivyoonekana kwa macho ya kimwili lakini vipo?
Wewe unayebishia hii kitu nakufananisha na mshamba mmoja anayeamini kuwa kwenye computer mambo yote ni keyboard tu eti kwa sababu ndo inayotumika saidi kwenye kuingiza data.
 
Hiyo Hollywood wanatengeneza picha zilizopo katika ulimwengu unaoonekana kwa macho na usioonekana kwa macho.
 
Hapa kila Mkristo anaamini kabisa kwamba Yesu alifunga siku 40 usiku na mchana pasipo kula kitu chochote. Ukimuuliza iliwezekanaje? anasema huyo alikuwa mwana wa Mungu; binadamu wa kawaida hawezi.

Huyo huyo utamsikia akiimba pambio eti ..
"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wana"
 
Sometimes huwa nikisoma post nyingine nacheka hata nikiwa peke yangu .... ebu ijaribu hiyo Meyiiiiiii uone kama ina madhara yoyote.
Sisemi kuwa ina madhara yoyote.ila nataka nijue huyoo meyiii meyiii ni nani ktk umimwengu huuu?,!! Na ana mamlaka yapi ktk ulimwengu huu mpk jina lake litumike kufungua mlango wa jicho la tatu?!!
 
Kwanza nianze kwa kumshukuru Mshana Jr amekuwa msaada mkubwa kwangu kwenye kujifunza mambo mengi. Nami sasa naona nianze sasa kuwafundisha wengine ..

ULIMWENGU WA 3D NA 4D

Unajua kila mtu anaishi katika sehemu mbili; katika ulimwengu wa 3D na katika ulimwengu wa 4D. D= Dimension. / mwonekano

Katika ulimwengu wa 3D ndio huu unaoniwezesha sasa naandika haya kwenye kompyuta na nikiangalia ninaona jua magari na tunaenda shule kusoma nk. Ni ulimwengu huu ambao umeuzoea siku zote tuna kula na kunywa. Katika ulimwengu huu tunatumia macho mawili na huku tunashangaa kwanini watu wengine wanafanya miujiza wakati sisi wengine hatuwezi? Au kwanini watu wengine wanatabiri wakati sisi hatuwezi?.
Hawa watu wanaweza wakafanya hivyo kwa sababu wanaweza wakatumia jicho la tatu ambalo mtu akiwa mtoto mdogo au mchanga huwa lipo very active. Na kadri anavyozidi kuwa mkubwa jicho hilo hufumbwa na kufanya asiweze kuona tena vitu vilivyo kwenye 4D.

Watu wanafanya mambo hayo ni kwa sababu wanauwezo wa kufumbua jicho la tatu na kuona vitu vilivyo kwenye 4D. Huo uwezo wa kufumbua hilo jicho ndio unaosababisha watu wanafanya miujiza wanatabiri na wanafanya vitu vingi ambavyo havionekani.

Kwa sababu mtu amefumba jicho hilo kwa mda mrefu huwa inamchukua mda kuwa na uwezo wa kulifumbua jicho hilo. Lakini kwa maelekezo maalumu jicho hilo linaweza likafumbuka. Jicho la tatu linakufanya uone ulimwengu mwingine tunaoishi sisi ambao ni mzuri sana. Tofauti na huu ambao umeharibiwa na watu wachache. Mantiki ya sisi kuwepo ni kuufanya ulimwengu huu ufanane na ulimwengu ulio kwenye 4D. Uoga na kuogopeshwa kumewafanya watu wasiweze kabisa kuingia katika ulimwengu huo.

Nitajaribu kueleze jinsi ya kuingia katika ulimwengu huo hatua kwa hatua na ndipo sasa utaanza kujielewa wewe mtu ni wa namna gani? Je! ni nguvu gani uliyo nayo ambayo umefungwa na watu wachache walioweka kanuni zao ili wewe upumbazike.

*Jicho la tatu ndilo linalotufanya tuone vitu kwenye ulimwengu wa 4D*

Kwa sababu ni mda mrefu sana haujawahi kulitumia jicho hilo ni vyema kuanza kufanya mazoezi jinsi ya kulitumia. Tafuta sehemu iliyotulia. ambayo hakuna kelele kelele. Au ikiwezekana jifungie chumbani na uzime taa. Hatua utakazo fanya ni unakaa vizuri mikono yako weka kwenye magoti.

Fumba macho yako haya mawili. Kaa kimya kwa mda wa dakika kama 6 - 10 hivi. Vuta hewa kwa kutumia pua na itoe kwa kutumia mdomo. Fanya hivyo taratibu taratibu. wakati mwingine ukiwa unaanza utasikia kichwa kinauma. Usihofu hiyo ni kawaida.

Anza kutoa sauti kwa taratibu ukisema MEYIIIIIIIIIIIIII, MEYIIIIIIIIIII. Bada ya mda jicho la tatu litaanza kufunguka taratibu. Kwa sababu mda mrefu hujawahi kulifumbua utaona giza giza vitu vitu usivyo vielewa. Fanya hivyo kwa mda wa wiki mbili tayari utakuwa umezoea utaanza kuwa na uwezo sana.

Utaanza kujua vitu vingi sana na kuanza kujielewa sasa wewe ni nani na una nguvu gani. Nitakueleza siri hiyo wanatumia akina nani na inaleta matokeo gani. Hakuna uchawi hapa mtu asikudanganye. Ni wewe tu jinsi ya kujielewa.

Karibu tuujifunze kwa pamoja (theory na practical)
Kwanza bro ungeyataja hayo mambo unayosema una anza kuyaona ili tuyajadili moja baada ya jingine tujue ukweli wake.

Pili,nini maana ya MEYIIIII na kwanini MEYIIIII ?

Ukishajibu nitakuja kukupa faida kubwa sana juu ya mambo hayo.

Kwa ufupi huo ni USHIRIKINA na unakupelekea katika upotevu.........

Narudi bro...... Elimu sahihi ni nuru na Ujinga ni giza.
 
Hata nikikueleza nimejuaje hutakubali kwa sababu hujafunguliwa ...
Binadamu ana milango 8 ya fahamu ... lakini mitatu ya mwisho (isiyofundishwa) ndo inategemewa sana katika elimu ya vitu visivyoonekana.
Macho yatakuonesha kitu fulani lakini kuna sehemu yanapeleka hizo data.
Masikio yakisikia kitu fulani yanapeleka data sehemu fulani; hivyo hivyo pua, ngozi, ulimi ... pale ambapo data hizo zinafanyiwa processing ndo panapofungua hilo jicho la tatu ambalo linafungua ile milango mitatu isiyofundishwa madarasani.
Unapenda ku jibu nusu nusu ili uulizwe au...si ueleze kitu umalize
 
Kwanza bro ungeyataja hayo mambo unayosema una anza kuyaona ili tuyajadili moja baada ya jingine tujue ukweli wake.

Pili,nini maana ya MEYIIIII na kwanini MEYIIIII ?

Ukishajibu nitakuja kukupa faida kubwa sana juu ya mambo hayo.

Kwa ufupi huo ni USHIRIKINA na unakupelekea katika upotevu.........

Narudi bro...... Elimu sahihi ni nuru na Ujinga ni giza.
Asante Zurri kwa kuja nadhani tutajua mengi kuhusu huu Uzi
 
Jaribu kwanza ..
Unajua nashangaa kwa nini usijiulize kwa nini A inaitwa hivyo na wala sio Z
Hujajibu swali langu mkuu, ni bora utuambie maana ya maneno hayo kwanza kabla ya kuyatumia. Mimi naamini hayo maneno yana maana, siyo bure tu, na kama hayana maana basi inawezekana kabisa hilo likawa "jina" la kitu fulani au kiumbe fulani. Kama hujui maana yake basi usiwaambie watu wayatumie, inaweza kuwa hatari zaidi kuliko unavyofikiri wewe.

Fahamu kwamba ulimwengu wa "roho" umegawanyika mara mbili, kuna "Roho njema", na roho "wachafu", hizi roho chafu ni kama sumu, na sumu haijaribiwi kwa kuionja, utakufa. Itakuwa vipi kama hayo maneno(MEYIII) ni jina la roho mchafu na huyo roho akawaingia hao watakaomuita???
 
Aisee kweli nilitaka kujaribu labda ningeweza kuuambia mbuyu hama ukajipande baharini na ingekuwa kumbe fix wamarekani duh
hakuna kitu kama hii Bro. hizi ni ndoto ambazo Holywood wamezipandikiza ktk vichwa vya watu.
asilimia 99 ya maneno ya watabiri wote na waganga wote NI UONGO.
Nimefanya Research miaka chungu mbovu.

Usipoteze muda wako kuzigeuza hizi fictions kuwa Reality. Hizi habari za 4 Dimension ziwache kwenye movie's tu. kinyume cha hapo utapoteza muda wako huenda ukadhurika kwa kulishwa UCHAFU na sumu na waganga wa kienyeji.
 
Hujajibu swali langu mkuu, ni bora utuambie maana ya maneno hayo kwanza kabla ya kuyatumia. Mimi naamini hayo maneno yana maana, siyo bure tu, na kama hayana maana basi inawezekana kabisa hilo likawa "jina" la kitu fulani au kiumbe fulani. Kama hujui maana yake basi usiwaambie watu wayatumie, inaweza kuwa hatari zaidi kuliko unavyofikiri wewe.

Fahamu kwamba ulimwengu wa "roho" umegawanyika mara mbili, kuna "Roho njema", na roho "wachafu", hizi roho chafu ni kama sumu, na sumu haijaribiwi kwa kuionja, utakufa. Itakuwa vipi kama hayo maneno(MEYIII) ni jina la roho mchafu na huyo roho akawaingia hao watakaomuita???
kiongozi hakuna kitu kama hii.
sema "Meyiii" all day long hakuna kitakacho kukuta.
Hizi ni imani potofu. Na imani husababisha Brain ku react. ukiamini Nazi iliotupwa njia panda inadhuru na ukaikanyaga au kuiruka huenda ukadhurika Psychologically lkn kama huamini hii kitu hata wakikuwekea nazi Lori zima hakuna kitakachokukuta.

Imani ina athari kubwa sana ktk Ubongo.
na Ubongo ndio inayo control mwili wako wote. ukiathirika basi kila kiungo kinaathirika.

kuna watu through imani tu wanaweza kupona maradhi mengi kwa kunywa maji ya kawaida tu. kikubwa waaminishwe kuwa yale maji ni dawa KUU yenye kuponyesha hicho wanacho ugua.
 
Hayo madudu ya ajabu ajabu utakayoyaona nn faida yake mkuu
mkuu naona kama aujamuelewa mtoa mada vizuri kutokana na yeye kajichanganya kidogo alivyoanza na mambo ya 3D na 4D za kisayansi zaidi lakini mwisho wa uzii ameenda kwenye point yake mambo ya kumeditate na mjicho wa tatu sijui

Dunia ina mambo mkuu kwa habari ya jicho la tatu alilo lizungumzia mtoa mada ni kweli kabisa inawezekana na ukiwa na nia ya kulifungua ilo jicho litafunguka tu na utaona madudu ya ajabu ajabu
 
Sijapungukiwa akili kiasi cha kwenda kwa mganga wa kienyeji kutafuta solution ya issue zangu.
labda hufahamu maana ya Research.
nani aliwahi kukaa peke yake dakika kadhaa akaita hio research?

nakupa Homework
manake nadhani na wewe ni ktk wale wavaa hirizi kwa kujilinda na TRA.

Nenda kwa mganga yyt hali ya kuwa una mke na watoto kisha kamwambie unatafuta watoto miaka mingi sana unataka akutazamie tatizo ni nini kama atagundua wewe una watoto.!

au mpeleke asie na mke wala mtoto kisha mwambie mganga mke wa jamaa anatembea na MTU na unataka kujua ni mtu gani kama hakukutajia jirani yako au mjomba wako .

halafu fuata hizo Fictions za huyu jamaa uone km utaiona hio 4 Dimension.

Elimu ni kitu muhimu sana.
someni bandugu au mtaendelea kuibiwa mpk Siku ya kufa.
Kama mtu anapata kuwa na jicho la jini au la mzimu haumdanganyi kwa lolote labda wale matapeli tu.
 
Yote sawa! hata mimi nilikuwa mbishi kama wewe!
Hehehe alafu sasa hivi una third eye?
Nakushauri ukamuone daktari wa magonjwa ya akili aliyekaribu na eneo lako.
 
Kama mtu anapata kuwa na jicho la jini au la mzimu haumdanganyi kwa lolote labda wale matapeli tu.
hakuna kitu kama hii.
nani mwenye Jicho la tatu? nitajie mmoja tu.
manake Serikali yetu inahitaji watu kama hawa wakatuonyeshe majambazi wote na wizi wote mahala walipo tuwaondoe kabisa nchini ili askari nao wapumzike kidogo na sisi tupate kuishi bila wsws.

Hizo ni Holywood Movies my good friend.
hakuna mwenye uwezo wa kuona kinachokuja wala kilicho jificha. Na akidai ana uwezo huo huyo ni Tapeli tu.
 
Back
Top Bottom