Ulijisikiaje pale ulipoambiwa kuwa mpendwa wako hawezi kupona tena.Ugonjwa umeshambulia sana mwili?

Nominee

JF-Expert Member
Sep 5, 2017
459
1,240
Nakumbuka Baba yangu mzazi alikuwa anasumbuliwa na saratani ya ngozi.Tulifanya jitihada za kila namna kuokoa maisha ya baba yetu mpendwa,tulizunguka hospitali mbalimbali ila mwisho wa siku tukaelekezwa tuelekee hospitali ya Ocean Road Dar-es-salaam.

Ndugu walipambana kuchangishana hela ili mzee atoke mkoani aende Dar kwa matibabu.Tulifanikiwa kufika Ocean Road na matibabu ya mionzi(Radiotherapy na Chemotherapy) yalianza.Ila mwisho wa siku tuliambiwa kuwa kwa hali aliyonayo mzee hawezi kupona tena.Kwahiyo akawa anapatiwa tu dawa za kutuliza maumivu huku akikisubiri kifo chake.Ni nyakati mbaya sana za maisha ya mzee wangu.Hatimae baada ya miezi takribani nane baadae mzee akaaga Dunia.

Nililia sana,ila hakuna namna zaidi ya kumuachia Mungu.Vijana tujitahidi kufanya check-up za mwili mara kwa mara,magonjwa mengine huwa yanaibuka tu ghafla yakiwa katika terminal stage na hautoweza kujitibu.
 
Mimi niliambiwa pole sana, tumejitahidi kumpambania mama tumeshinda kwani fuvu limepasuka vipande vipande na damu imevuja nyingi mno.
Nikasema sawa nashukuru. Mungu nipe Kicheko nimalizie hii
Mama alipata ajali au?
 
Mkuu, ukisikia mpendwa wako hawezi kupona tena, unafikiri utajisikiaje? Furaha? Mbona umeuliza very obvious question? Hapo kwenye neno mpendwa andika "adui yako" ita make sense zaidi.
Labda itakuwa nimekosa msamiati sahihi wa kuweka hapo ili mada yangu ieleweke.
 
Kama huyo mpendwa ni mwanandoa hapo ni mtihani mgumu, kama ni lapulapu la shoo tu unaweza kulikimbia. Yapo matukio ya kweli kwa wapendwa kukimbiana inapotokea shida kwa mmojawapo, tena wengine ni wanandoa. Shida zenyewe ni ugonjwa usio na matumaini ya kupona na hali mbaya ya uchumi isiyo na matumaini ya kupanda
 
Wiki 2 zilizopita, simu ikaita.
Yeye (Her ) "Kizibo uko wapi?"
Mimi "Kazini"
Yeye "Wahi njoo unione, mimi nakufa"

Nilipofika, aisee, mdada (rafiki na mteja wangu sana) amenyong'onyea halafu amekuwa mweusi (rangi ya ngozi ya usoni imebadirika)

Yeye "Kizibo, umekuja kuniona? Mungu akusaidie sana. Mimi siwezi kuendelea rafiki yangu. Kizibo nakupenda sana rafiki yangu."

Mimi "Dah! A, amini nakwambia utapona"

Yeye "Kwa hapa nilipofika, siwezi kuendelea. Siwezi."

Mimi "A, huyo alieko hapo nje ndo mama yako?"

Yeye "Ndiyo"

Mimi nikatoka nikamfata mama, aliekuwa nje amebeba mtoto mgongoni usoni akilengwa lengwa na machozi kwa mbali na alionekana kudata
"Mama, kwa hali hii tunafanyaje??"
Tukadiscuss pale, nikawapa connection ya mtu fulani, nikamwambia mpigieni simu huyu mtu, gharama atakayowaambia kama akiweza kumponya nitawasaidia kulipa.


Nisiandike sana, hivi ninavyoandika mdada yuko kwenye hatua za mwisho za kurudi kwenye hali yake ya kawaida na leo wameenda kanisani.

Mama hadi muda huu anadai niwe mkwe wake na binti anatamani iwe hivyo ila mimi ( ).
 
Back
Top Bottom