Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Jumba alilonunua Ex wife wa Tiger Wood kwa $12 million
Jumba hilo amelibomoa na kusafisha kubaki uwanja mweupe kupisha ujenzi wa jumba analotaka
[h=3]Bofya hapa kupata kinagaubaga zaidi Tiger's ex destroys $12 million mansion[/h]
Twapata funzo gani hapa Wanajamii Forums?
Kwa wengi tunaweza kujifunza katika tukio hili, mali usiyoitokea jasho huna uchungu nayo. Kama angekuwa na akili kidogo kama yangu ambapo wengi wametoa comments za aina ya mtazamo wangu, ingekuwa na manufaa zaidi kama nyumaba hiyo ingebaki na kutafuta kiwanja kingine cha kujenga jumba la kiwango anachotaka. Lakini kwa kuwa ana akili zaidi yangu, hakuona umuhimu wa kuuza jumba hilo na kutafuta kiwanja kingine ili ajenge jumba analotaka kwa kuokoa $12 million.
Kwa uamuzi na utekelezaji aliofanya sijui kwa kushauriwa au kutoshauriwa ni sawa na kwamba ametumbukiza dampo $12 millioni kitu ambacho hata matajiri wakubwa hawathubutu kufanya hivyo.
Pesa aliyopata $100 millioni kutokana na talaka kwa Ex husband Tiger Wood imemchanganya akili kiasi cha mimi kumkumbuka yule tajiri wa Arusha aliyekuwa anauza madini ya Tanzanite alipokuwa anakaa chumba cha juu cha hoteli na kumwaga mapesa nje kupitia dirishani ili watu waokote wakati kuna taratibu ambazo kama ana uchungu na maskini angezifuata na zingefanya kazi vizuri zaidi.
Twapata funzo gani hapa Wanajamii Forums?
Kwa wengi tunaweza kujifunza katika tukio hili, mali usiyoitokea jasho huna uchungu nayo. Kama angekuwa na akili kidogo kama yangu ambapo wengi wametoa comments za aina ya mtazamo wangu, ingekuwa na manufaa zaidi kama nyumaba hiyo ingebaki na kutafuta kiwanja kingine cha kujenga jumba la kiwango anachotaka. Lakini kwa kuwa ana akili zaidi yangu, hakuona umuhimu wa kuuza jumba hilo na kutafuta kiwanja kingine ili ajenge jumba analotaka kwa kuokoa $12 million.
Kwa uamuzi na utekelezaji aliofanya sijui kwa kushauriwa au kutoshauriwa ni sawa na kwamba ametumbukiza dampo $12 millioni kitu ambacho hata matajiri wakubwa hawathubutu kufanya hivyo.
Pesa aliyopata $100 millioni kutokana na talaka kwa Ex husband Tiger Wood imemchanganya akili kiasi cha mimi kumkumbuka yule tajiri wa Arusha aliyekuwa anauza madini ya Tanzanite alipokuwa anakaa chumba cha juu cha hoteli na kumwaga mapesa nje kupitia dirishani ili watu waokote wakati kuna taratibu ambazo kama ana uchungu na maskini angezifuata na zingefanya kazi vizuri zaidi.