Ndugu Nyani Ngabu, Weweni mmojawapo wa wana JF ninaowafuatilia na kuheshimu sana post zenu. Sikujua Kabila lako hadi leo, na pia sikuwa na haja ya kujua kabila lako, kwani utanzania unanitosha.
Kuna usemi tembo haoni kilicho mgongoni mwake. Wasukuma ni kabila kubwa hapa nchini, na watu wenye imani, subira na upendo, tofauti na makabila mengi ya hapa Afrika Mashariki. Mimi ni ushahidi tosha, kwani nina watu wa jamii yangu ambao hawana asilia ya usukumani, lakini wanaishi na kufanya biashara sehemu nyingi za huku makwenu kwa zaidi ya miaka 70 , na hawakubaguliwa hata siku moja, Mwanza na Shinyanga ni mojawapo ya Miji yenye mchamganyiko mkubwa wa watu wa kila kabila.
Tusifumbie macho ukweli, kila kabila au umma lazima lina wachache walio tofauti na mwenendo wa wengi . Ukweli ni kuwa Hayati Raisi Magufuli alikuwa na mengi mazuri, lakini alikuwa Mkabila sana na Mdini, mimi nilikuwa mfuasi wake na nilimpigia kura mara zote mbili, lakini kwa haya ninauwezo wa kusema kuwa alikuwa MKABILA, MPENDELEAJI NA MDINI, Ukiangalia Baraza lake la Mawaziri ni ushahidi tosha, hata kwenye Udini alienda mbali sana , katika upendeleo wa kidini alielemea zaidi kwenye Madhehebu yake ya kikatoliki.
Wasukuma wengi hawakufurahia ukabila aliokuwa anaufanya, kwani hata hivyo hakuwa anawatendea haki wasukuma kwa ujumla, bali pale penye maslahi yake na wale wakaribu wake.
Wasukuma ni watu wenye mila nzuri na wapenda haki, ila kuna haka kakundi kinachotaka kulitumia taifa, kupitia ukabila, na wanufaika watakuwa ni wao wachache, ukabila unawanufaisha wachache, kupitia mgongo wa wengi.
Tunaihitaji TANZANIA isiyo ya kikabila,