Ulaya pamenishinda narudi bongo

Ulaya pamenishinda narudi bongo

Status
Not open for further replies.
Mbona mapema mno hata lugha umejua kweli,wenzio wanaoza miaka na hawakimbii mwisho wanatoka,wewe ungeomba wakaazi wa huko ulipo humu wakusaidie upate kazi hakuna mahali utapata kazi bila kushikwa mkono ila na hako kamji sasa utasanda

Atapata shida sana hako kamji, kamejaa wanafunzi balaa
 
Maisha kitu cha ajabu saana, wakati jamaa unahangaika huku na kule hapa bongo kuna mtu haijui hata Zambia ana uwezo wa kununua gari ya 80mil + humu humu... nahisi kuna tatizo kwa WaAfrica huku Africa kuzitafuta, kuzifikia na kuzitumia fursa...
 
Hujaishi ughaibuni, watu hawana makaratasi yoyote na kwa uzoefu ukimwangalia tu unajua ni mgeni kwa sura na rangi lakini wanapiga mzigo wa kufa-mtu bila wasiwasi wowote, tuulize sisi wenye uzoefu.
Wazungu wanaona mwarabu, mhindi mwafrika tunafanana, yaani inawachukua muda sana kutusoma...

Kuna watu wanatumia documents za mtu mmoja kufanya kazi...
Atafute wabongo, wanaija, wacongoman watakaompa michongo..mnakubaliana unawalipa.
Ahaso asisubirie kushikwa mkono.

Everyday is Saturday............................. 😎
 
Hope huyu mngoni kashadondoka bongo maana tangu mwezi march leo ni August ... Au corona ilimsave ? Kurudi nyumbani sio shida karibu sana home blaza ulaya unaweza kurudi ata miaka ya mbele usiwaze sanaa
 
Mkuu unafahamu kutengeneza Baiskeli? Kama ujuavyo Sweden na nchi nyingine nyingi za Ulaya, baiskeli ni usafiri wa kawaida na watu wengi hutumia. Nakushauri uanzishe sehemu ya kutengeneza.

Anza za majirani wanaokuzunguka badae wakishakujua utaanza kupokea za watu wengi. Jambo la msingi punguza tu bei maana garage za kutengeneza bike kwa Sweden ni very expensive. Unaweza ambulia hata 1000 kr kwa siku. Hiyo ni sawa na 260K za Bongo!

Kuna jamaa M-Kongo anapiga hiyo kazi pamoja na kunyoa watu nyumbani kwake tu kwa bei nafuu. Huwezi amini ana make pesa kimasikhra na maisha yanamwendea vizuri. Muhimu usichague tu kazi.

Mie kutokujua kutengeneza baiskeli na kutokujua kunyoa imenikosesha pesa za bure kabisa. Hapa kilichobaki ni kutafuta tu kazi ya kufanya delivery..
 
aaa mlongo vhangu unafeli wapi hao mabinti kwa nini wasi kuelewe kidume wa kingoniii?
ina onekana hujawapa mavitu ya ki namanditi dadii! komaa huko kota kubwelai kunyumba mlongo vhanguuuu!!!
 
Mkuu unafahamu kutengeneza Baiskeli? Kama ujuavyo Sweden na nchi nyingine nyingi za Ulaya, baiskeli ni usafiri wa kawaida na watu wengi hutumia. Nakushauri uanzishe sehemu ya kutengeneza.

Anza za majirani wanaokuzunguka badae wakishakujua utaanza kupokea za watu wengi. Jambo la msingi punguza tu bei maana garage za kutengeneza bike kwa Sweden ni very expensive. Unaweza ambulia hata 1000 kr kwa siku. Hiyo ni sawa na 260K za Bongo!

Kuna jamaa M-Kongo anapiga hiyo kazi pamoja na kunyoa watu nyumbani kwake tu kwa bei nafuu. Huwezi amini ana make pesa kimasikhra na maisha yanamwendea vizuri. Muhimu usichague tu kazi.

Mie kutokujua kutengeneza baiskeli na kutokujua kunyoa imenikosesha pesa za bure kabisa. Hapa kilichobaki ni kutafuta tu kazi ya kufanya delivery..
Kaka vip bado upo Sweden?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom