Ulaya pamenishinda narudi bongo

Ulaya pamenishinda narudi bongo

Status
Not open for further replies.
Title ya uzi pamoja na contents vinareflect hiki: "Ulaya pamenishinda narudi bongo".

Halafu wewe ambaye huwa unajitambulisha kuwa upo Uswisi ukacomment hivi:
View attachment 1447001

Hadi hapo huoni kwamba 'ushamchanganya' msomaji wa threads zako unazosimuliaga kwamba upo Uswisi? Just by common sense, huuoni kabisa huo utatanishi hapo?

Naona ushaanza kupanic .

-Kaveli-
Makaveliiiiiii fala sana wewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani niwe mbali na nyumbani kihasi hiko nishindwe nitauza hata makaratasi nitoboe.
 
Europe siku hizi hakuna ishu... Wakimbizi wa kiarabu wamejaa tele.. hakuna kazi yeyote. Canada, Australia, New Zealand, USA ndio place to be at least Kuna kazi za kusafisha na kuosha na box kwa ujumla ila ulaya labda UK kwa sababu wamejitoa kwenye umoja wa ulaya hivyo wamecut influx ya unqualified people na job zimespike.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Kwa UK hakuna kitu, kuna watu wanasoma PhD uku wanatafuta Part time jobs Ila kupata kazi za Part time ni ngumu mno wanaishia kufanya kazi za usafi
 
Mbona mapema mno hata lugha umejua kweli,wenzio wanaoza miaka na hawakimbii mwisho wanatoka,wewe ungeomba wakaazi wa huko ulipo humu wakusaidie upate kazi hakuna mahali utapata kazi bila kushikwa mkono ila na hako kamji sasa utasanda
 
Hujaishi ughaibuni, watu hawana makaratasi yoyote na kwa uzoefu ukimwangalia tu unajua ni mgeni kwa sura na rangi lakini wanapiga mzigo wa kufa-mtu bila wasiwasi wowote, tuulize sisi wenye uzoefu.
Ndo maana nasema atumie mtandao anaotumia kulialia aombe idea pa kuanzia.kama mwenyeji wake kalalia masikio anaweza asipate abc pa kuanzia.
 
Mkuu Kwa UK hakuna kitu, kuna watu wanasoma PhD uku wanatafuta Part time jobs Ila kupata kazi za Part time ni ngumu mno wanaishia kufanya kazi za usafi

Duuh!!
kwa vile mtu unasoma Phd , eti unataka upate kazi ya kuhusiana na usomi wa kibongo kwenye taaluma za ulaya .
kwa uzoefu gani wa kazi zao wakupe kazi?

ENI WEI , Fuatilia stori za wasomi duniani, waliokuwa wanaosha viombo mahotelini kupata hela ya kujikimu ili kuendelea na masomo yao.
 
Duuh!!
kwa vile mtu unasoma Phd , eti unataka upate kazi ya kuhusiana na usomi wa kibongo kwenye taaluma za ulaya .
kwa uzoefu gani wa kazi zao wakupe kazi?

ENI WEI , Fuatilia stori za wasomi duniani, waliokuwa wanaosha viombo mahotelini kupata hela ya kujikimu ili kuendelea na masomo yao.
Hujanielewa kabisa, wapo wengi wamemaliza Degree ya kwanza ad masters uku uku UK na sasa wanasoma PhD na kazi zimekua ngumu Kwa wao kupata ad wanadandia Part time job za Amazon na usafi.
Nikupe tu kitu kimoja kitakusaidia maishani waafrika wengi ambao wako vizuri wakifika Ulaya labda wanaenda kusoma mara nyingi wanafaulu kuliko hao wazungu unaowasifia. Wazungu wana elimu na mitaala Bora Ila usijidanganye eti Muafrika hawezi pata kazi nzuri Ulaya
 
Turudi kwa mtoa mada
sasa wewe una viza ya sweden inamaana ulikuwa na SHENGEN VIZA au?
kama ungeshajua zamani ulipofika hamna maslahi, kwanini usianze kuzurura ulaya nzima,
ungepata tu kibibi cha kukustiri
 
Uko ughaibuni upi mkuu wa bagamoyo?
Njiani katika njia za panya zilizobatizwa "Njia ya Kuzimu" kukwepa askari wa uhamiaji, kunaonekana utelezi utokanao na mvua zisizokoma za misitu minene ya tropiki, matope yafikayo ugokoni, makaburi yasiyo na jina wala alama za imani zao kwani hao wahamiaji waliopoteza maisha na sasa wamelala udongoni hata kaburini utambulisho wao haujulikani.

Nchi nyingi kama Colombia, Ecuador....

Soma zaidi: bofya linki hii chini:

Wahamiaji: Safari toka Congo kupitia Brazil mpaka Canada kwa miguu
 
Kuna mada kuhusu haya masuala ya kwenda majuu alileta mwenzetu aitwa Lusungo tukajadili sana na mimi nikiwepo.

Pole sana na yalokusibu lakini usikate tamaa, kwanini ukate tamaa na umefika Ulaya?

Mimi nimeishi hapo Sweden mji wa Sundsvall kwa muda kidogo kabla ya kuanza safari zingine katika nchi hizo za Ulaya.

Kwani Tanzania umesomea kozi gani?

Kwa kifupi kwa sasa hali ya soko la ajira ni ngumu kutokana na competition kubwa baada ya makampuni na biashara mbalimbali kufungwa na hivyo kutoa redundancies nyingi sana.

Ushauri wangu kwako ni kwamba utafute scholarships kama tayair unayo first degree na unatakiwa uombe ukiwa hukohuko eneo la tukio Sweden.

Pitia hapa angalia:

https://studyinsweden.se/Scholarships/

Na hapa

Scholarships in Sweden for International Students | 2020-2021 Scholarships

Mmalizie mbuzi huyo usibakize hata mkia.
Uko sahihi sana mkuu, kazi Ulaya Kwa sasa ni changamoto sana. Kazi za uku unafanya ambazo hazihusiani na elimu kama usafi kidogo afadhali. Kikubwa kinachoniumiza hasa Watanzania hatuna ushirikiano wa kuinuana tukiwa ughaibuni kama wenzetu wa Nigeria
 
Hujanielewa kabisa, wapo wengi wamemaliza Degree ya kwanza ad masters uku uku UK na sasa wanasoma PhD na kazi zimekua ngumu Kwa wao kupata ad wanadandia Part time job za Amazon na usafi.
Nikupe tu kitu kimoja kitakusaidia maishani waafrika wengi ambao wako vizuri wakifika Ulaya labda wanaenda kusoma mara nyingi wanafaulu kuliko hao wazungu unaowasifia. Wazungu wana elimu na mitaala Bora Ila usijidanganye eti Muafrika hawezi pata kazi nzuri Ulaya

Yaani nimekuelewa sana kimantiki lakini ni vigumu kama huna uzoefu na kazi hata kama unasoma au unayo Phd, utagonga mwamba tu,
hata kama ulikuja ukasoma ya kwanza na ya uzamili na Phd lakini kama huna uzoefu na kazi unayotaka, hivyo vyeti vyako si muhimu
kwa kiwango hiko cha elimu, mtoa kazi yeye anataka mtu atakaye anza kazi na mbio kwenye kazi, sio eti waanze kukufundisha kazi

Kupata kazi nzuri huku sio tatizo kabisa, mimi nishapiga shahada uhandisi na kujieleza vizuri niko Shirika la Afya, lakini nilipitia njia ndefu ya kazi ndogo ndogo tu kama hizo za Amazon, hizi ndio wanamaindi kujua work ethics ya mtu na iliyonipa uzoefu na kuweza kujipambanua kujieleza kiuzoefu
 
Uko sahihi sana mkuu, kazi Ulaya Kwa sasa ni changamoto sana. Kazi za uku unafanya ambazo hazihusiani na elimu kama usafi kidogo afadhali. Kikubwa kinachoniumiza hasa Watanzania hatuna ushirikiano wa kuinuana tukiwa ughaibuni kama wenzetu wa Nigeria

Ushirikiano ungestawi endapo kila huyo mtanzanai angekuwa hana makandokando alopitia huko Ulaya na Marekani.

Hata hao wanigeria si wote wanafanya hivyo unavyosema labda iwe ni wa familia moja.
 
Yaani nimekuelewa sana kimantiki lakini ni vigumu kama huna uzoefu na kazi hata kama unasoma au unayo Phd, utagonga mwamba tu,
hata kama ulikuja ukasoma ya kwanza na ya uzamili na Phd lakini kama huna uzoefu na kazi unayotaka, hivyo vyeti vyako si muhimu
kwa kiwango hiko cha elimu, mtoa kazi yeye anataka mtu atakaye anza kazi na mbio kwenye kazi, sio eti waanze kukufundisha kazi

Kupata kazi nzuri huku sio tatizo kabisa, mimi nishapiga shahada uhandisi na kujieleza vizuri niko Shirika la Afya, lakini nilipitia njia ndefu ya kazi ndogo ndogo tu kama hizo za Amazon, hizi ndio wanamaindi kujua work ethics ya mtu na iliyonipa uzoefu na kuweza kujipambanua kujieleza kiuzoefu
Naomba tumalize hoja mkuu Ila umenifurahisha sentence yako ya nimepiga Uhandisi hahaha kusoma Uhandisi ni kawaida sana kwa ulaya kuliko Tanzania. Elimu ya Tanzania ni ngumu mno kuliko ya Ulaya japo hauwezi kufikia ubora wa Ulaya. Ata Uhandisi niliosemea Mimi ni tofauti sana na Tanzania bado hatujaanza kufikiria kutoa iyo course.
Umeona kazi ulizopitia mwanzoni sababu ukikosa kazi sahihi kulingana na taaluma yako
 
Naomba tumalize hoja mkuu Ila umenifurahisha sentence yako ya nimepiga Uhandisi hahaha kusoma Uhandisi ni kawaida sana kwa ulaya kuliko Tanzania. Elimu ya Tanzania ni ngumu mno kuliko ya Ulaya japo hauwezi kufikia ubora wa Ulaya. Ata Uhandisi niliosemea Mimi ni tofauti sana na Tanzania bado hatujaanza kufikiria kutoa iyo course.
Umeona kazi ulizopitia mwanzoni sababu ukikosa kazi sahihi kulingana na taaluma yako

Ok tumalize hoja mkku
na uhandisi wa huku ni kichwa kufikiria ili kuleta mabadiliko halisi kwa hizo hizo simple kanuni za uhandisi sio kujaza mahesabu ubaoni ambayo hayaleti tija
 
Ushirikiano ungestawi endapo kila huyo mtanzanai angekuwa hana makandokando alopitia huko Ulaya na Marekani.

Hata hao wanigeria si wote wanafanya hivyo unavyosema labda iwe ni wa familia moja.
Ila Ulaya bora hata uwe na marafiki wazungu. Watu wa Africa full usintich wengi hawana ustaarabu,full wivu ,kufuatana fuatana n.k
 
Ok tumalize hoja mkku
na uhandisi wa huku ni kichwa kufikiria ili kuleta mabadiliko halisi kwa hizo hizo simple kanuni za uhandisi sio kujaza mahesabu ubaoni ambayo hayaleti tija
Mahesabu kwenye Uhandisi lazima yawepo mkuu tena mengine magumu sema walimu wengi wa Tanzania hawawezi kubadili ayo mahesabu kwenda kwenye practical application apo ndo tatizo kubwa. Tunajua kufanya mahesabu magumu bila kujua practical application zake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom