Ukweli utakuweka huru: CHADEMA mbioni kufa?

Ukweli utakuweka huru: CHADEMA mbioni kufa?

Ktk pitapita zangu kule ktk Jamhuri hii tukufu ya Danganyanaland, kule Sikonge kuna kata inaitwa Kiwele cjui uwele. Its very funny kama wale watu they are event knowledgeable of their own existence, sasa mtu akija na ID ya Sikonge naapata shaka sana kama anajitambua!
 
Last edited by a moderator:
Mbona unajihami sana na scud zangu? Heheheheeeee.... Wewe nimeshakumaliza na sihitaji tena kukushambulia.

Huwa sipendi mtu anilishe maneno na siyo kwamba nimepanic. Nipanic nini? Kwani kuna sehemu nimedanganya?

Kuhusu Padre wako, kamwambie kuwa kama yeye ni Mwanahabari basi ajifunze kuwa mtafiti.

Kama yeye kasikia Malalamiko ya mgawano wa viti maalumu, alitakiwa kufanya utafiti walau kidogo kwa kwenda mtaa wa Ufipa au kuwapigia simu wampe huo utaratibu ili ajuwe anaandika na ukweli ukoje.

Sasa yeye kasikia kitu tu anakuja na mihemko yake ya kuhukumu. Ila sisi tukimpa dozi kidogo, Wateja wake mnakuja macho yamewatoka utafikiri Machoman anamfokea Hogan.

Vipi mechi unaangalia lakini? Wewe ni City au wale mashoga waliofungishwa ndoa wakaambiwa MAN UNITED? Heheheee
Naona tupo katika viwango tofauti. Sikujua kama tupo hapa kushambuliana. Kwani siku hizi hatuwezi tu kujadili jambo kwa hoja, heshima na staha bila kushambuliana kwa maneno ya kejeli na kuitana mashoga? Au ni kwa vile tunatumia majina ya bandia?

Anyway - Mimi siyo mshabiki wa mpira na hayo mambo ya City sijui na mashoga wa MAN UNITED siyajui wala hayanihusu. Inashangaza kidogo kwani naona uko fixated sana na mambo ya ushoga. Kulikoni? Yaani huwezi kuongea kitu na wala kutukana mtu bila kurejelea ushoga? Sorry but wewe ni shoga? Na una uhakika kuwa huyo Padri Mapunda wako ni shoga (mwenzio)? Hata ukiitwa mahakamani unaweza kudhibitisha? Yeah! Ukikuta mtu yuko obsessed na kitu na kukitaja taja sana hata pasipostahili basi wanasaikolojia wanasema kuwa kuna uwezekano mkubwa mtu huyo kitu hicho kinamhusu au anahusika nacho moja kwa moja. Siko hapa kukuhukumu hata kama ni shoga hiyo ni haki yako na uko huru kuishi maisha uyatako hapa duniani ali mradi tu huvunji sheria. Lakini inakera unapojaribu kuburuza watu wengine katika hii obsession yako na mambo ya ushoga.

Hata mimi sitakushambulia hata urudi na povu na matusi kiasi gani. Hakuna tusi ambalo limeshawahi kumdhuru mtu tena la mtu anayetumia jina la bandia mtandaoni. Jaribu sana kujifunza kujadiliana na watu kwa ukawaida tu hata kama kuwa peke yako na keyboard kunakupa ujasiri, anonymity na nguvu za ajabu za kuporomosha matusi na kudharau watu.

NB: Hao mashoga wako wa MAN UNITED wameshinda au wameshindwa? Time to celebrate ama?
 
Ukweli una tabia ya kulipiza kisasi kama utapuuzwa
 
Hujui hata utani? Mtu mgumu. Kafie mbele na ugumu wako.

Naona tupo katika viwango tofauti. Sikujua kama tupo hapa kushambuliana. Kwani siku hizi hatuwezi tu kujadili jambo kwa hoja, heshima na staha bila kushambuliana kwa maneno ya kejeli na kuitana mashoga? Au ni kwa vile tunatumia majina ya bandia?

Anyway - Mimi siyo mshabiki wa mpira na hayo mambo ya City sijui na mashoga wa MAN UNITED siyajui wala hayanihusu. Inashangaza kidogo kwani naona uko fixated sana na mambo ya ushoga. Kulikoni? Yaani huwezi kuongea kitu na wala kutukana mtu bila kurejelea ushoga? Sorry but wewe ni shoga? Na una uhakika kuwa huyo Padri Mapunda wako ni shoga (mwenzio)? Hata ukiitwa mahakamani unaweza kudhibitisha? Yeah! Ukikuta mtu yuko obsessed na kitu na kukitaja taja sana hata pasipostahili basi wanasaikolojia wanasema kuwa kuna uwezekano mkubwa mtu huyo kitu hicho kinamhusu au anahusika nacho moja kwa moja. Siko hapa kukuhukumu hata kama ni shoga hiyo ni haki yako na uko huru kuishi maisha uyatako hapa duniani ali mradi tu huvunji sheria. Lakini inakera unapojaribu kuburuza watu wengine katika hii obsession yako na mambo ya ushoga.

Hata mimi sitakushambulia hata urudi na povu na matusi kiasi gani. Hakuna tusi ambalo limeshawahi kumdhuru mtu tena la mtu anayetumia jina la bandia mtandaoni. Jaribu sana kujifunza kujadiliana na watu kwa ukawaida tu hata kama kuwa peke yako na keyboard kunakupa ujasiri, anonymity na nguvu za ajabu za kuporomosha matusi na kudharau watu.

NB: Hao mashoga wako wa MAN UNITED wameshinda au wameshindwa? Time to celebrate ama?
 
Great Thinkres wanajua fika kuwa CCM ndiyo inayoyoma Tanzania. Mwangalieni Magufuli amefanya mangapi ambayo yameasisiwa na CCM tangu amepokea madaraka? Kama huniamini msikiliza kweye ile speech. Anatekeleza yale yote CDM waliyoyapigania kila siku bungeni. Chadema kwa watu waelewa imeshinda, inakuwa, na inastawi Tanzania vizuri sana. Hatimae watanzania wameanza kupata haki yao japo kidogo na kwa mbali kwa sababu ya kazi kubwa ambayo inafanywa na upinzani Tanzania. Mbowe ni mmoja wa viongozi imara na ambayo wanaimpact kubwa sana kwenye siasa za Tanzania. Mnaohangaika kumchafua mtaangukia pua kama Kikwete alivyotandikwa pale Dodoma juzi na Magufuli.
 
Siktir lan.....

Naona bado unahangaika na mambo yako ya kishoga. Haki ya nani kazi unayo. Mpaka unajua na mambo ya ku.fi.rwa katika Kituruki. Mungu mwenye rehema na Akurehemu. May the Lord have peace on your soul!

NB: Lengo la kumtukana mtu ni kumuumiza kihisia. Sasa unapoporomosha haya matusi yako ya kishoga tena kwa lugha isiyoeleweka kwa mlengwa, hapo si unakuwa unajitukana mwenyewe tu? Fag illogical logic eeeh?
 
Last edited by a moderator:
Ushauri wa kipumbavu huu! Hivi kuna yeyote anayelalamia hili kwa kufanya uchunguzi? Inamaana kama mtu anaonekana ni mpiganaji wa kweli aachwe kwa ajili ya kuogopa vijineno vya propaganda za kijinga kisa ni mtu wa kaskazini? Kama mtu alishinda kura za maoni aachwe tu kisa tu ana vinasaba vya kaskazini? Huu wote ni kipumbavu wa mtu asiyejua namna siasa inavyoendeshwa! Tujiulize kati ya wabunge wote wa Chadema kupitia viti maalum ni wangapi watatokea kanda ya kaskazini? Chama hakiwezi kufa kwa sababu tu wachumia tumbo wachache hawakusikilizwa! Majungu hayajengi zaidi ya kuchochea chuki za kijinga ndani ya jamii.

Ukishajuwa wa kanda ipi ujuwe pia ni wa dhehebu lipi.
 
Wewe mtoa mada umekurupuka,hujui ulichoandika. Fanya utafiti acha kukurupuka.
 
Mapunda+padri.jpg


Malalamiko mengi yamezuka hususani ugawaji wa viti maalumu ya ubunge na udiwani ndani ya chama kikuu cha upinzani nchini. Mitandoni maoni na malalamiko yamesheheni kiasi kwamba mtu unaweza kuanza kufikiria 'Chadema mbioni kufa'? Watu wanatoa hoja mbalimbali na zingine ni za msingi kabisa, ni vema sababu hizi zikachukuliwa kwa uzito wa hali ya juu, badala ya kuzipuuza na hivyo kuhatarisha uhai wa chama hiki kinachoonekana ni tumaini la Watanzania kwa mabadiliko ya nchi hii.



Siku moja asubuhi nilipigiwa simu kutoka Dar es Salaam na mwanachama mmoja aliyelalamikia suala la upendeleo wa kikanda katika ugawaji vyeo na viti maalumu vya ubunge na udiwani. Ukipita katika kona nyingi za nchi yetu hutakosa kusikia watu wakilijadili suala hili la upendeleo ndani ya Chadema hasa katika kipindi cha kuanza kipindi kipya cha uongozi katika nchi yetu.

Mimi najiuliza je, malalamiko hayo ni ya kweli au ya kutungwa. Ni muda mrefu sasa watu wengi wamekituhumu Chadema kuwa kina mbegu ya upendeleo kwa wanachama wake. Ni vema viongozi wakuu wa chama hicho na washauri wao wakalichukulia jambo hili kwa uzito mkuu.

Kinachoonekana ni kwamba kuna baadhi ya wanachama katika maeneo mbalimbali ya nchi wametumia muda wao, akili na hata mtaji wa pesa zao kukijenga chama, lakini linapokuja suala la uteuzi wa vyeo na viti maalumu wanajikuta wanaachwa. Je, suala hilo lipoje ndani ya chama hicho kikuuu cha upinzani nchini.

Watu wanahoji inakuwaje, mtu anakuwa kiongozi ndani ya chama na anajitahidi kufanya yale yanayompasa kufanya kwa bidii na akachukua fomu ya kugombea kiti maalumu, lakini fomu yake ikapotea ofisini? Hujuma kama hii inaweza kuelezwaje na watendaji wakuu? Kama ni kweli mambo hayo yapo hata ndani ya Chadema wakati tulizoea kuyasikia yakitendeka zaidi ndaniya chama kikongwe CCM, kumbe sasa huo ugonjwa unaonekana kusambaa hata ndani ya Chadema.

Inakuwaje, watu wanahoji viongozi karibu wote makao makuu, viti maalumu ni kutoka Kaskazini, hili linatoa taswira gani ya chama kinachojinasibu ni chama mbadala wa chama tawala (CCM). Ukweli ni kwamba kama Chadema inataka kueleweka kama ndiyo chama mbadala cha CCM katika nchi hii lazima kijaribu kuepuka mitego yote ya chama tawala, kama upendeleo wa kikabila, udini, ukanda , na u-familia, urafiki na upambe. Watanzania tulilelewa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kutaka sote tuwe sawa, tuheshimiane, tujaliane, tusaidiane na tusibaguane katika jambo lolote lile. Na dini zetu zisiwe ndiyo chanzo cha kuvuruga amani yetu kwani nchi hii haina dini ila kila mtu ana dini yake kitu ambacho ni imani yake binafsi isiyoingiliwa na itikadi yoyote na hata Serikali haiingilii.

Watanzania wanafikiri kwamba katika sehemu ambazo Chadema bado haijaeleweka ilikuwa ni muda mwafaka kuteua wanachama wa sehemu hizo ambao wametumia nguvu na muda wao kukijenga chama hicho kushika nafasi mbalimbali. Watanzania wanasema hii ingekuwa ni njia mojawapo ya kukijenga chama badala ya kukibomoa kwa kufanya upendeleo kama unavyoelezewa na kulalamikiwa na baadhi ya wanachama na wananchi kwa ujumla. Ni wazi kwamba Chadema bado ina kazi kubwa ya kujisambaza katika kila kona ya nchi hii yenye ukubwa mwingi na mahitaji tofauti ya wananchi wake.

Wananchi na baadhi ya wanachama wanalalamikia suala la kuachwa vijana ambao ndiyo moyo au nguzo ya chama cha Chadema katika teuzi za hivi karibuni. Inafahamika wazi kwamba taifa lolote bila kujali vijana basi linakuwa limekufa kabisa. Vijana ndiyo taifa na leo na kesho ambao lazima watazamwe kwa jicho la pekee katika jamii yoyote ile. Vijana wasiwe wanatumika tu kuwavusha wanasiasa (vigogo) wakati wa uchaguzi kama huo uliopita, halafu baada ya hapo wanawekwa kando na kusubiria tena miaka mitano ijayo watakapohitajika. Ni vema Chadema ikaanza kuamka kutokana na makosa yanayofanyika ili kiweze kujirekebisha kama vile waswahili wasemavyo ?kosa siyo kufanya, bali kulirudia kosa.?

Chadema acheni kujifanya viziwi wa kutosikia malalamiko na vilio wanavyotoa wananchi na baadhi ya wanachama wenu kwani ?lisemwalo lipo na kama halipo, linakuja.? Chadema acheni kujifanya vipofu wa kutokuona ukweli wa yale yanayofanyika ndani ya chama chenu, chukueni hataua sasa. Kwa upande wangu hali hii inatisha katika medani ya siasa zetu za demokrasia na utawala bora, na ndiyo maana naandika kwa kuthubutu kwamba ?Chadema mbioni kufa?? Najua makala haya hayatapendwa na baadhi yenu katika chama, lakini huwa nina amini kuwa ukweli utakuweka huru.Na wataalamu wanasema kwamba ?mtu anayekupenda ni yule anayekukosoa na kukuambia ukweli, badala ya yule mnafiki anayekuchekea na kukusifia mambo ya nje tu, au anayekupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.?

Napenda kuwaasa Chadema kuchukulia kwa uzito wa pakee yale yanayosemwa katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu uliokwisha ili kuweza kujipanga vizuri zaidi. Ukweli ni kwamba pamoja na mikakati na mbinu lazima zipangwe, lakini Chadema lazima kisome alama za nyakati mapema zaidi. Kwa mfano sasa baada ya uchaguzi huu ambao unasemwa na baadhi ya wananchi umepora ushindi wa Ukawa lazima chama kijiulize ni kwa nini kilishindwa uchaguzi huo? Je, ni makosa gani chama kimefanya katika uchaguzi huo? Na sasa ni wazi kwamba wananchi wengi wanaona wazi kwamba bila kuwa na Katiba Mpya ambayo ina tume huru ya uchaguzi , CCM itaendelea kutawala milele. Hiyo ni changamoto kubwa kwa Ukawa na wapenda mabadiliko wote nchini, sasa kazi ni moja tu kudai Katiba Mpya yenye tume huru ya uchaguzi na kanuni safi za uchaguzi.


Mungu ibariki Tanzania na watu wake.

Chanzo; Makala Mwananchi


 
Mbona anaihuisha chadema wakati watu tulishakaa na arobaini siku kibao. Wapeni tu taarifa Dr. Magufuli na CCM wanachapa kazi siyo mchezo.
 
Umeongea ukweli na sioni kama kuna atakae kusikiliza upande wa uongozi, CDM siasa ni biashara Mbowe & Co wanaangalia masilahi hayo ya ukombozi na chama mbadala ni yenu.
 
Back
Top Bottom