Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,353
- Thread starter
- #21
Utamaduni katika jamii ni suala la msingi katika kukuongoza ni jinsi gani utachukua maamuzi yako.
Ukipanda basi mara nyingi kama sio zote utakuta wameandika "abiria chunga mzigo wako". Ukiingia kwenye nyumba za watu Kuna jumbe zinasema "ya humu tuachie wenyewe". Tukiwa kwenye chumba cha mitihani haturuhusiwi kuonyeshana majibu au kujadili. Kwa maana hiyo mfumo wa makuzi na malezi yetu umejengwa katika "usiri (ubinafsi?)
Kwa maana hiyo Tatizo sio sisi wanaume bali ni makuzi na malezi tuliyopewa na kurithi katika jamii.
Unajua tatizo la huu ugonjwa ni kuwa unahusisha social contacts. Unaweza kusema waache wauane lakini katika huo mzunguko wa maambukizi utampata mtu aliye karibu na wewe na itakugusa.