BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,331
Asilimia kubwa ya wasomi wa kibongo wanauzika sana na wengi wanafanya vitu vyao katika nchi za US, UK, UAE , Canada na nyingine nyingi duniani tena wana vyeo vya juu. Hata baadhi ya waajiri kuwaomba Wabongo waliowaajiri kuwapendekeza Wabongo wengine kwa waajiri hao ili nao waajiriwe. Wabongo hao wengi wamejijengea sifa ya uchapakazi, uaminifu, uelewa mkubwa wa kazi zao, kutokuwa walalamikaji.
Hii ni zaidi ya dharau.....na hii inaonesha how far you still lag behind in thinking!
Wacha sijazungumzia usomi wangu,mimi nachosema ni kwamba hata kama Zinduna hajaja na data ila ukweli upo palepale,maana yake kwa mfano mdogo tu wa matumizi ya kompyuta msomi wa leo hawez,ina maana muajiri akishakupa kazi akupeleke kompyuta kozi???
Usisimamie kwenye data,,,liangalie hila jambo kwa uhalisia lipo au halipo,na kwa miaka ya karibun wameibuka wanafunz wetu wanaenda form I hawajui kusoma wala kuandika,na hawa kwa miaka ijayo utataka data kama hawauziki,,,,,
isije ikawa wewe ndo unachekesha bila kujijua,,,,,
Hapana!! Huyu atakuwa bado yupo nchini!! Tena kule maeneo ya manzese!! hahaaa
Hawa wasomi ninaowazungumzia mimi ni wale ambao walizaliwa, kukulia na kusomea Tanzania mpaka degree yao ya kwanza. Baada ya hapo baadhi wakapata scholarships za Serikali kwa ajili ya Masters na labda Phd na wengine walizitafuta wenyewe kupitia balozi mbali mbali zilizo nchini. Kwa maoni yangu aliyezaliwa, kukulia na kusomea Tanzania kutoka shule ya msingi hadi 1st degree (katika vyuo vyetu nchini) ambayo ndiyo iliyomwezesha kupata scholarship nchi za nje kamwe huwezi kumtenga huyu kwamba si msomi wa Kitanzania.
That's precisely my point. Wewe umeamua kuwaita ni wasomi wa Kitanzania lakini ukweli ni kuwa kilichowapa hizo kazi SIO DEGREE (AU SECONDARY EDUCATION) ZA TANZANIA bali ni hiyo nyongeza ya elimu waliyoipata huko walikoipata - ambako si Tanzania. Nitajie mtu unaemfahamu ambae education qualifications zake zote ni za Tanzania na ambae amepata kazi hizo unazozitaja hapa.
Btw: Hata hizo admission za masters/PhD mara nyingi hazitolewi kwa kigezo cha elimu ya Tanzania pekee. Mara nyingi uki-submit first degree toka kwetu ili upate admission kwenye vyuo vya maana hasa watakulazimisha usome kozi kadhaa kabla hujawa admitted properly. This proves Zinduna's point in this thread.
Nyongeaza, Elimu ya tanzania inafundisha story za masomo tuyasomayo na ndi maana wengi wetu unaweza kuta performance yake ipo vizuri ila ukimpeleka kwenye vitendo hamna kitu.
Kinachoniudhi zaidi ni pale ninaposikia matangazo kwenye vyombo vya Habari kuwa kuna nafasi ya kusomea UALIMU kwa wenye DivIV 27,Form six kwa wenye Subs-jury pass 2 N.k Mimi hapo hasira kama ni TV au redio na switch OFF hadi hapo baadae na kama ni Gazeti nachana.Tangu lini mtu alishindwa akaandaa mtu wa kupata Div 1???????pleaseeeeeeeeee
LET CHANGE THIS!!!!!!! KWANZA ,mabadiliko mengine yafate
Nyongeaza, Elimu ya tanzania inafundisha story za masomo tuyasomayo na ndi maana wengi wetu unaweza kuta performance yake ipo vizuri ila ukimpeleka kwenye vitendo hamna kitu.
hapa kuna ukweli....BAK uko sahihi sana mkuu, yaani mimi ninamarafiki ambao wameajiriwa UK, USA, CANADA NA SA ambao kwanza utashangaa mambo wanayoyafanya. yaani mimi nilimshangaa mama mmoja anaitwa Hulda swai yaani ukiona team yako na jins alivyo excell utashangaa. ana run centre yenye watu zaid ya 100 ambao wanafanya kazi chini yake na wote wanaperform vizuri.
Nilisikitika sana alipoambiwa arudi Tz na mkuu wa nchi watu wakamtisha ukirudi Tz utafanyiwa majungu bora uendelee kujilia bata wako huko CSIR.
Najua kauli yangu hii itawakera wengi hususan hao wanaojiita wasomi, lakini najua kwamba ukweli mara nyingi huwa unauma sana.
Katika orodha ya nchi za Afrika ambazo wasomi wake wanaibwa na kusombwa na kupelekwa huko Ulaya na Marekani kufanya kazi , Tanzania haitajwi kabisa.
Watanzania wengi wanaokwenda nje kufanya kazi, ni vibarua zaidi, wenyewe wanajiita wabeba mabox, na hata kama ni wasomi, basi utawakuta wanafanya kazi ambazo huwezi kusema zitaweza kuisaidia nchi.
Hata hivyo wapo Watanzania wachache sana ambao wamenunuliwa nje na kufanya kazi huko kwa sababu ya uwezo wao kiufahamu katika taaluma zao.
Lakini hii yote ni kutokana na mfumo wetu wa elimu ambao kwa miaka mingi umekuwa ukidumaza akili zetu.
Mara nyingi wadau mbalimbali wakiwemo baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakipiga kelele kuhusu haja ya Serikali kubadili mfumo wa elimu ili kuweza kuwashindanisha wasomi wake na wasomi wa nchi nyingine duniani lakini jambo hilo limeonekana kama vile halina maana.
Najua serikali kupitia wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi imeshawahi kubadili mitaala ya elimu mara kdhaa, lakini ninachojaribu kusema hapa ni je tabia ya wanafunzi kukariri ili wafaulu mitihani badala ya kuelewa imekomeshwa kwa kutafuta chanzo chake?
Ukweli ni kwamba, ni vigumu kwa wasomi wengi wa Tanzania kushindana kwenye soko la dunia kitaaluma kwa sababu, hawakuandaliwa kuwa watu wanaofahamu, bali wameandaliwa kuwa watu wanaokariri
Hapo kwenye performance na vitendo tofauti yake nini?
Wanafunzi wengi wa kitanzania wanafuata vyeti shuleni/vyuoni na sio KNOWLEDGE & SKILLS!!!!!!!!!!!!!!