View attachment 240091
Jicho la tatu ndilo linalotufanya tuone vitu kwenye ulimwengu wa 4D.
Kwa sababu ni mda mrefu sana haujawahi kulitumia jicho hilo ni vyema kuanza kufanaya mazoezi jinsi ya kulitumia. Tafuta sehemu iliyotulia. ambayo hakuna kelele kelele. Au ikiwezekana jifungie chumbani na uzime taa.
Hatua utakazo fanya ni unakaa vizuri mikono yako weka kwenye magoti.
Fumba macho yako haya mawili. Kaa kimya kwa mda wa dakika kama 6 - 10 hivi. Vuta hewa kwa kutumia pua na itoe kwa kutumia mdomo. Fanya hivyo taratibu taratibu. wakati mwingine ukiwa unaanza utasikia kichwa kinauma. Usihofu hiyo ni kawaida.
Anza kutoa sauti kwa taratibu ukisema
MEYIIIIIIIIIIIIII, MEYIIIIIIIIIII. Bada ya mda jicho la tatu litaanza kufunguka taratibu. Kwa sababu mda mrefu hujawahi kulifumbua utaona giza giza vitu vitu usivyo vielewa. Fanya hivyo kwa mda wa wiki mbili tayari utakuwa umezoea utaanza kuwa na uwezo sana.
Utaanza kujua vitu vingi sana na kuanza kujielewa sasa wewe ni nani na unanguvu gani. Nitakueleza siri hiyo wanatumia akina nani na inaleta matokeo gani. Hakuna uchawi hapa mtu asikudanganye. Ni wewe tu jinsi ya kujielewa.