Baada ya malalamiko mengi sana jukwaani juu ya vijana kuchezea kipigo cha kwenda toka kwa wake zao na migogoro mingine ningependa kushirikisha juu ya kidogo kile ambacho nakifahamu kuhusu mambo ya ndoa.
1.Wanawake wengi sikuhizi wanaolewa ili kutimiza fantasy na sio kwa kujua ndoa ni nini haswa. na ukiwa makini utagundua wengi ni walengaji. Haolewi na mtu yeyote bali wanatakaga ambaye ana maisha mazuri yanayotosheleza kufanya show off kwa mashosti na marafiki hata kama jamaa ana fake. When reality hits ni kilio.
2.Umri wa mwanaume kuoa ni limitless. Kigezo kikubwa tu ni kuwa na uchumi na hii itaprove point namba moja. Ni rahisi kwa mstaafu wa shirika la umma kuoa binti wa umri wa mjukuu wake ila ni ngumu sana kwa shoe shine mwenye miaka 60 kuoa binti mbichi wa kimjini mjini.
3.Vijana wa kiume wanashindwa kutofautisha mapenzi ya kweli na tamaa. Ukuta uliopo baina ya mapenzi halisi na tamaa za fedha na ngono ndio yanayotumaliza katika ndoa. Interests zinapokuwa tofauti ni hatari sana kwa ustawi wa ndoa.
4. Licha ya age differences Family backgrounds, malezi vina play role kubwa sana kwenye kustawisha na kudumisha mahusiano ama kuyabomoa. Exposure baina yenu pia inaingia humu.
5. Ndoa hazina tatizo ila wanandoa ndio wenye matatizo. Huwezi kuyajua madhaifu ya mtu kwa muda mchache na bila kutumia intelijensia za kimedani. Kukurupuka kuoa mtu ambaye huzijui rangi zake kwa uhalisia ni mbaya sana. Compatibility issues ndio zinapelekea ndoa kuwa na changamoto kubwa sana ya kudumu. Wazungu wanasema Marry your type.
6. Hakuna mtu mwenye perfection by 100% ila angalia rate ya defect. Je unaweza kuvumilia madhaifu ya mtu huyo. Hili eneo ndio litakupa majibu ya point namba 5 kwamba how far are you and your spouse compatible? Madhaifu yake ni 1,2,3 how can you deal with them. Kumbuka kuibadili tabia ya mtu ni kazi ila angalia je, katika sifa unazotaka kwenye 100% anafaa kwa asilimia ngapi. Nikizungumzia sifa naomba tuondoe mawazo ya kipuuzi kama shepu, hipsi ama urembo wa sura. Hivyo ni ziada ila core matter ni jinsi ambavyo ana behave kwako na kwa watu wengine. Tabia zake za asili ambazo kwa intelijensia umeweza kuzing'amua kama uchoyo, kupenda ngono sana, kuongea sana, ukimya sana, kuweka vitu moyoni, hasira na reactions, umalaya na flirting around, communication issues,vision and thinking, uvivu na mengineyo. Kuna mengi unaweza ukajifunza ukikaa na mtu kwa muda mrefu.
Tujiulize haya maswali.
1. Je, mtu unayetaka kumuoa ana tabia ambazo unaweza kuzivumilia. Tabia ni kama ngozi haijifichi. Eti demu kisa ana sura na tako tu siku usipompa hela analalamika kama kafiwa na wazazi halafu unamuoa hivyo hivyo siku ukitimuliwa kazi mambo yakayumba unakuja kulia lia umenyimwa K. Mara mke anakujibu shiti. Mzee pambana uliyataka mwenyewe



!
2.Mwanamke unajua kabisa hakupendi ila kwa tamaa zako unamlaghai na viela vya mshahara na madili ofisini ili aingie laini unampora kijana wa watu demu. Unakuja kugundua kuna boya flani anamkata wakati ushamuweka ndani. Ujinga kama huo pambana nao mwenyewe.
3. Wewe sio mtu wa kutoka ila unaokota demu mlevi. Inaanza kupambana kumbadilisha asinywe pombe. Eti kisa umempenda. Acha upuuzi utakuja kupigwa makofi. Umemkuta na tabia huipendi usioe. Acha atampata mlevi mwenzie wataelewana. Sio kazi yako kumbadilisha mtu tabia.
4.Mwanamke humjui vizuri ushamtia mimba kisa nyege zako. Kuua soo unaona bora muhitimishe ndoa ifungwe eti muwe mke na mume ujilie vyako. Unakuja kugundua demu ni mchoyo kishenzi na mbinafsi hapendi ndugu zako waje hata kidogo. Unaishia kudhalilika tu.
5. Mzee umeishi kama kinega kwenye ujana wako wote unafikia miaka 60 eti unataka kuoa mjukuu wako. Show huwezi unakuta unagongewa hovyo tu. Kisa sifa umechukua mtoto mbichi. Mwishowe anakuwekea kisumu anakuua unaacha balaa kwenye ukoo. Acheni upuuzi wazee oeni mapema ili mkiwa watu wazima mcheze na wajukuu.
6. Unajijua riziki yako papatu papatu, tafta mwanamke mwenye uvumilivu ili uishi nae kwa amani. Mwanamke asiyebabaishwa na maisha ya kisanii. Anayejua kuwa maisha yana ups and downs. Wewe unahondomola ma slay queen kisa wanakusifia ni handsome na kula hela zako hovyo kwenye ma bar. Siku ukiishiwa mbinu za kivita unaanza kulialia oh mke wangu akinipa buku tu analalamika na ananisonya. Fala mmoja wewe enjoy show ya kizombi.
7. Mtoto wa kike unapoona hela tu kicimy kinawika hujui jamaa hela katoa wapi, je ana mke au familia? Kakupa offer za savanah kakulaza hotelini ushaanza kuwaza ujibebeshe mimba. Utakuja kuumia bwege wewe. Unakuja kugundua late kumbe ni dalali wa katalunya tu aliuza Prado akaotea million zake 3 za genji. Mwishowe ni kuanza kusumbuana ustawi wa jamii.
Tubadilike na tutumie akili zetu vizuri kupunguza malalamiko yasio na maana. Mjue mtu wako vizuri kabla hujaamua kukaza mkanda nae kwenye maisha.