Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,473
- 13,624
Hiyo ya facebook ni mifano tu, katika kujenga hoja huwezi kukwepa mifano.Hujajibu swali nililokuuliza na swali ulilojibu sijakuuliza.
Unaelewa maana ya methali ya Kiswahili inayosema "Usiige tembo kunya, utapasuka msamba"?
Facebook walioanzisha waliparamia biashara wasiyoiweza?
Unafananisha Shirika la Ndege Tanzania na Facebook?
Sent from my typewriter using Tapatalk
Hakuna anayeiga kunya kwa tembo, waliopewa majukumu ya kufufua shirika la ndege wanajua wanalolifanya, ila sisi humu JF ni kama tunataka kuwapotezea malengo waliyonayo kiutendaji.
Sisi humu JF ni kama tunawawangia katika kitu wanachokifanya, kuyumba kwa biashara ya ndege kwa sababu ya corona sio kumuiga tembo kunya. Njia wanazotumia Ethiopia kuendesha shirika lao sizo zinazotumiwa na Kenya, sizo zinazotumiwa na Tanzania, hivyo tuepuke kuishi kwa kukariri zile stori tunazozisoma magazetini na katika maongezi ya jioni wakati tukiwa bar.
Hakuna aliyeparamia biashara asiyoiweza, tatizo mtu mmoja anakuwa hamjui yule aliyepewa dhamana ya biashara, hili suala la corona ni upepo tu na utatulia na maisha yataendelea kama kawaida.