Ukweli kuhusu mpaka wa Tanzania na Malawi

Hivi kuna faida gani kuingia vitani kugombania mipaka ilhali kwa kiasi kikubwa wakazi wa maeneo husika wanaingiliana kwenye shughuli zao za kila siku? Mmalawi akitaka mafuta ya taa anakuja Tanzania kuchukua, hivyo hivyo kwa mtanzania anayeishi mpakani. Hebu tujifunze kutumia Diplomasia jamani. Nguvu zenyewe za kupigana hatuna, mpaka leo tumeshindwa kupigana na maradhi, na umasikini. Adui ujinga ndiyo anatupiga kila kukicha, hadi Rais wa nchi naye ujinga umemshinda nguvu na sasa ndiyo unaomuongoza kwenye kila analofanya na kusema..
Wewe kichwa chako kibovu sana! Tukiwa wajinga wataendelea kumega mipaka kama akina Iddi Amini alivyodai kwamba Kagera Salient iko Uganda! Sasa hivi nako Warundi wameumega mpaka wetu! Kamuzu Banda naye aliwahi kudai kuwa Wilaya yote ya Kyela iko Malawi! Kwa hiyo wewe kwa akili yako finyu tukae kimya tu ili "kuogopa malumbano na vita?" Open your mind please!
 
Hao google wana yao uku mambo shwari wamalawi wanakwao nasi kwetu.Uku ritui,mbambabay,manda na itungi operation zaendelea hawa jamaa hatuna kwele nao kabisa.Kwanza karonga yote wanaoishi apo ni watz so suala la mpka kwao sio issue kabsaaa
Hapa sio suala la kuingiliana, ni suala la mipaka yetu! Hao Watz wanaokaa Karonga wanalipa kodi wapi?
 
Jana Membe amedai eti kuna kamati imeteuliwa kuhusu suala hilo! Pinda pia aliwahi kudai eti kuna timu ya wataalamu imepelekwa kukutana na wenzao wa Malawi! Hata hivyo niliwahi kusoma kitabu kimoja kilichoandikwa "Boundaries of East Africa" mwandishi aliandika ku-suggest kwamba kisheria Tanzania haina hata tone la la maji Ziwa Nyasa (wamalawi huliita Lake Malawi)! Wamalawi wamekuwa wajanja sana kusambaza Ramani hapa nchini zinazoonesha upuuzi kama huo! Mimi nionavyo, hakuna haja ya kujadiliana na wamalawi, ni vema tukakaa kwenye "state of conflict" tukawa na sehemu ya Ziwa kuliko tukaingia kwenye mjadala na kulikosa kabisa lile Ziwa!
Fact ni kwamba ktk ramani ya tanganyika tulyopeleka un wakati uleeee, hilo ziwa lote lipo malawi-who to be blamed, hatuna ziwa hapo wazee tuwe wapole tu. By ze way Tngnyika haina haja ya kupigania raslmali kwani proved hata tukipewa raslimali zote duniani still hazitosaidia watz chini ya system hii ya magamba, in fact natamani kwa sasa hii nchi isiwe hata na raslimali moja kwa sasa ili kuepusha hizi intervention za majizungu wanaowapa sifa za kiongo magamba ili wazidi kuchota raslmali zetu. Let kwanza tuondoe magamba then tuta-accumulate resource zetu ikiwa pamoja na huko mpakani kwa ajil ya ziwa nyasa kwa faida ya wote! Ok
 
Sawa basi, wamalawi chukueni ziwa lenu! Lakini kumbukeni tutawa-charge kila wakati wimbi likipiga na kumega ardhi yetu. Let say 1ml usd kwa sqm 1.
 
Mkuu huo mpaka ndo ulivyo sio kwenye google earth tu hata ukiangalia kwenye ramani zetu wenyewe ziwa lote liko malawi ingawa watanzania wanafanya shughuli zao mule, sijui kama ndo mpaka unavyotakiwa kuwa au ni makosa ya kiuchoraji.
 
Fact ni kwamba ktk ramani ya tanganyika tulyopeleka un wakati uleeee, hilo ziwa lote lipo malawi-who to be blamed, hatuna ziwa hapo wazee tuwe wapole tu. By ze way Tngnyika haina haja ya kupigania raslmali kwani proved hata tukipewa raslimali zote duniani still hazitosaidia watz chini ya system hii ya magamba, in fact natamani kwa sasa hii nchi isiwe hata na raslimali moja kwa sasa ili kuepusha hizi intervention za majizungu wanaowapa sifa za kiongo magamba ili wazidi kuchota raslmali zetu. Let kwanza tuondoe magamba then tuta-accumulate resource zetu ikiwa pamoja na huko mpakani kwa ajil ya ziwa nyasa kwa faida ya wote! Ok
Watu wa Mbinga, Ludewa na Kyela wanafaidi sana hili Ziwa kwa upande wa usafiri, shughuli za uvuvi na recreation (km Beach iliyopo Matema)! Sasa wewe unavyodai tu-accumulate resources unamaanisha nini, unataka tuwe na "Time Machine" ili kurudisha muda nyuma?
 
Mkuu huo mpaka ndo ulivyo sio kwenye google earth tu hata ukiangalia kwenye ramani zetu wenyewe ziwa lote liko malawi ingawa watanzania wanafanya shughuli zao mule, sijui kama ndo mpaka unavyotakiwa kuwa au ni makosa ya kiuchoraji.
Hizo Ramani nasikia zimesambazwa na Wamalawi wenyewe hapa nchini!
 
Hivi kuna faida gani kuingia vitani kugombania mipaka ilhali kwa kiasi kikubwa wakazi wa maeneo husika wanaingiliana kwenye shughuli zao za kila siku? Mmalawi akitaka mafuta ya taa anakuja Tanzania kuchukua, hivyo hivyo kwa mtanzania anayeishi mpakani. Hebu tujifunze kutumia Diplomasia jamani. Nguvu zenyewe za kupigana hatuna, mpaka leo tumeshindwa kupigana na maradhi, na umasikini. Adui ujinga ndiyo anatupiga kila kukicha, hadi Rais wa nchi naye ujinga umemshinda nguvu na sasa ndiyo unaomuongoza kwenye kila analofanya na kusema..
Nashukuru kwa mchango wako, maisha yanaendelea tu huko. Mfano kyl, shughuli za uvuvi usio na tija zinaendelea.
 
Watu wa Mbinga, Ludewa na Kyela wanafaidi sana hili Ziwa kwa upande wa usafiri, shughuli za uvuvi na recreation (km Beach iliyopo Matema)! Sasa wewe unavyodai tu-accumulate resources unamaanisha nini, unataka tuwe na "Time Machine" ili kurudisha muda nyuma?
Wazungu wanafaidi sana beach zetu,je ni za kwao? Plz soma post yangu ili upate ujumbe wangu-uspige meza tu ikiwa umetoka "kutafakari"
 
Waziri muhusika hana habari,mbunge hajui na mkuu wa mkoa ana majukumu mengi!
kwani waswahili wote wanajua mambo ya google earth kama rahisi mwenyewe ndo aliifahamu google earth baada ya kuzulu ofisi za microsoft..kwa hiyo sasa hata hizo habari sijui kama waziri atazijua..
 
Jana Membe amedai eti kuna kamati imeteuliwa kuhusu suala hilo! Pinda pia aliwahi kudai eti kuna timu ya wataalamu imepelekwa kukutana na wenzao wa Malawi! Hata hivyo niliwahi kusoma kitabu kimoja kilichoandikwa "Boundaries of East Africa" mwandishi aliandika ku-suggest kwamba kisheria Tanzania haina hata tone la la maji Ziwa Nyasa (wamalawi huliita Lake Malawi)! Wamalawi wamekuwa wajanja sana kusambaza Ramani hapa nchini zinazoonesha upuuzi kama huo! Mimi nionavyo, hakuna haja ya kujadiliana na wamalawi, ni vema tukakaa kwenye "state of conflict" tukawa na sehemu ya Ziwa kuliko tukaingia kwenye mjadala na kulikosa kabisa lile Ziwa!
Mwandishi huyo alikuwa sahihi. Suala la mpaka wa Malawi na Tanzania, Wamalawi wapo sahihi kisheria. Ingawa sheria za kimataifa zinasema mahali penye maji kama maziwa na bahari mpaka ni katikati ya maji hayo hali ni tofauti kwa Malawi na Tanzania. Kwa mujibu wa mkataba baina ya Tanzania na Malawi uliosainiwa wakati wa ukoloni (kumbuka kote Tanganyika na Malawi mkoloni alikuwa Mwingereza) mpaka ni kingo za ziwa Malawi kwa upande wa Tanzania. Na huo ni mkataba rasmi nashangaa tu serikali inapiga porojo haitaki kusema ukweli. Isipokuwa kuna mazungumzo yamekuwa yakiendelea kwa muda mrefu sasa ili kuondoa utata uliopo juu ya mkataba huo.
 
Fact ni kwamba ktk ramani ya tanganyika tulyopeleka un wakati uleeee, hilo ziwa lote lipo malawi-who to be blamed, hatuna ziwa hapo wazee tuwe wapole tu. By ze way Tngnyika haina haja ya kupigania raslmali kwani proved hata tukipewa raslimali zote duniani still hazitosaidia watz chini ya system hii ya magamba, in fact natamani kwa sasa hii nchi isiwe hata na raslimali moja kwa sasa ili kuepusha hizi intervention za majizungu wanaowapa sifa za kiongo magamba ili wazidi kuchota raslmali zetu. Let kwanza tuondoe magamba then tuta-accumulate resource zetu ikiwa pamoja na huko mpakani kwa ajil ya ziwa nyasa kwa faida ya wote! Ok

sentensi yako ya kwanza hapo juu sijaielewa ,ramani ya Tanganyika tuliipeleka UN ili iweje? mipaka iliyopo leo nchi za kiafrika ziliamua kuirithi kama ilivyo toka kwa wakoloni mwaka 1884 huko Berlin ujerumani

sasa Google inahusikaje kufanya hayo?

Italeta fujo sana endapo kila nchi itajiamulia mambo kienyeji-enyeji kama Malawi inavyotaka kufanya,vita vya Uganda vilipiganwa kwa mambo kama haya
 
Wewe kichwa chako kibovu sana! Tukiwa wajinga wataendelea kumega mipaka kama akina Iddi Amini alivyodai kwamba Kagera Salient iko Uganda! Sasa hivi nako Warundi wameumega mpaka wetu! Kamuzu Banda naye aliwahi kudai kuwa Wilaya yote ya Kyela iko Malawi! Kwa hiyo wewe kwa akili yako finyu tukae kimya tu ili "kuogopa malumbano na vita?" Open your mind please!

Mkuu labda hao kina Idd Amini ndio wajinga, labda binadamu wote ni wajinga.., hivi unajua ni pesa kiasi gani inatumika kwenye majeshi dunia yote?, hivi unajua ni madhara kiasi gani yanatokana na vita, na ni nini hasa huwa sababu ya kugombana zaidi ya tamaa na upuuzi wa mtu mmoja ?

Hivi unajua binadamu tungekuwa na busara, upendo na sio ubinafsi na tamaa tungeweza kutumia malighafi za dunia yote tukala na kusaza na kila mtu akawa na maisha mazuri...

Najua sometimes jeshi ni la muhimu ili kuweka amani na kuepukana na vichaa, lakini kama binadamu tungekuwa na busara labda kungekuwa na Jeshi kubwa la dunia (United Nations) ambalo lingekuwa kama kiranja wa dunia kwa kumfunza adabu yeyote anaekiuka maadili... au maybe LOVE ndio njia pekee ya kuepuka vita

Maybe dunia nzima na watu wote ni wajinga na tunafight the wrong war between people badala ya kufight against the environment and betternment ya kila mtu hivi hii mipaka ni nani aliyoiweka na kwanini mtu yoyote asiweze kwenda popote pale kutafuta maisha so long wenyeji wa hapo wanamkaribisha.
 
Hako kaziwa NYASA kenyewe hakana faida yoyote ya kiuchumi kwa taifa letu zaidi ya kutujazia nafasi tu. Waache wamalawi walichukue tu, sisi tuna fursa nyingi sana za kiuchumi mfano Ziwa Victoria, Mlima Kilimanjaro, Serengeti n.k. Tusijaribu kushawishi jeshi kuingia vitani, lina kazi nyingi nyingine za kufanya kwa taifa letu.
 
Wakati wa Banda alidai eneo lote la Mkoa wa Mbeya ni sehemu ya Malawi!na kuna chama kimoja siku za miaka ya Mwinyi bado walidai sehemu hiyo ya Tanzania ni ya malawi na hata hivyo wanyakyusa na watu wa Kalonga malawi wote wanaongea lugha moja na ni ndugu na ndiyo maana kunakuwa natuhuma watu wengine wanadhaniwa ni wamalawi sio watanzania,kuna Mtanzania amewahi kuchukua madaraka makubwa ktk serikali ya malawi wakati alikuwa ni Mtanzania, Hapa ndipo inapokuja umuhimu wa vitambulisho vya kitaifa,watu wamekuwa wakiangalia zaidi mikoa ya kagera ktk tatizo hilo lakini wamesahau Mbeya na Ruvuma! Hata zambia nani anajua kwamba Mwanawasa alikuwa ana asili ya Tanzania? kwa taarifa yenu Baba yake alikuwa ni Mnyakyusa wa TZ, Zambia nako lipo hilo Tatizo hasa kwa Watanzania wengi ambao wameshika madara zambia,wabunge,mawaziri na wafanya biashara wengi tu.Kuna wimbi kubwa sana la watanzania waliohamia zambia wakati wa uchumi ulioshamili wa shaba na sasa wengine watoto wao wanarudi Tz na ni wengi sana.kuna mmoja aliwahikuniambia Baba yao aliwaambia kabla hajafa hapa TZ kwamba ikiwa siku moja wakiona maisha magumu TZ wanaweza kurudi kuishi zambia maana wana uraia wa kuzaliwa Zambia na wana vyeti vya kule vya kuzaliwa,Tatizo kubwa hapa kwa utafiti mdogo niliofanya wengi wana uzalendo wa Tanzania waliko toka wazazi wao na hapo najifunza jambo kuhusu Wanyarwanda wa kitusi kwanini wanakuwa na uzalendo sana wa Rwanda kwao.

Kitu cha muhimu nikuwa makini sana na mambo kama haya maana yanaweza kuleta matatizo makubwa sana kati ya nchi na nchi,kumbuka kuna watanzania wengi sana malawi na kama walivyo wamalawi kwa hiyo busala nikuwa na maelewano, wazungu walitugawa tu kama mbuzi huku wakigawa ndugu upande huu wengine upande mwingine,ktk malawi wilaya ya karonga wale ni wanyakyusa kule wanaitwa Wangonde na wanyakyusa wa Kyela ni wangonde pia,wale wa Rungwe ni wanselya,wengine ni wandali wa ileje na wakinga lakini hayo majina yametokana na maeneo woote hao ni kabila moja na utamaduni mmoja. Wakinga wanakuwa na tofauti kidogo zaidi sababu ya kuingiliana na wabena lakini ukiwasikiliza wanaongea lugha moja na makundi mengine haya.

Mwisho swala la ziwa inabidi serikali kulitatua mapema tusije kuingia kwenye vita,uchumi utaharibika kama vita ya Uganda ilivyo tuhalibia ingawaje sio sababu ya kuwa masikini mpaka sasa maana rwanda wamepigana miaka yote na sasa wanatuacha mbali kabisa.

I stand to be challenged!
 
MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI! Ileje wilaya iliyopakana na Malawi kila kitu wanategemea Malawi kuanzia Radio zote ni za Malawi,sukari,Chumvi na comodities zote zinatoka Malawi tuwape hiyo wilaya kwani wakazi wake woote ni maskini sana...
 
Ziwa Nyasa ni mali ya Tanzania na Malawi mpaka ni katikati ya ziwa full stop.
 
Google earth!!!!kwa hiyo tuufuate huo!kasema nani,ni ziwa lao kwa maana ya jina lakini kama ni kulitumia kwa shughuli za maendeleo mbona hiyo ni toka enzi ya banda samaki zinavuliwa humu na usafiri pia kama kawaida,kyela hadi mbambabei maana halisi ya kuwa lakwao watu wangezuiwa kuvua samaki na meli zingekatiza hilo ziwa kwa kuomba kibali malawi kitu ambacho hakipo na hakijawahi kuwa.nijuavyo mimi dai kuu la malawi kwa tz wala halikuwa ziwa ila wilaya nzima ya kyela miaka hiyo ya sabini mwishoni lakini toka tz ishinde vita ya uganda banda aliufyata.wacha walianzishe maana kuna mtafaruku wa kimaisha huko nina hakika karonga yote siku moja itakuwa mali yetu sema wanajeshi wetu wa sasa aaaaaaaaahh!!sijui kwa vile hatuna vita wanapiga raia wakubwa zao nao shimbo wamekuwa wafanya biashara ya zana za kilimo MBOMBO NGAFU.
 
Hivi kuna faida gani kuingia vitani kugombania mipaka ilhali kwa kiasi kikubwa wakazi wa maeneo husika wanaingiliana kwenye shughuli zao za kila siku? Mmalawi akitaka mafuta ya taa anakuja Tanzania kuchukua, hivyo hivyo kwa mtanzania anayeishi mpakani. Hebu tujifunze kutumia Diplomasia jamani.

Nguvu zenyewe za kupigana hatuna, mpaka leo tumeshindwa kupigana na maradhi, na umasikini. Adui ujinga ndiyo anatupiga kila kukicha, hadi Rais wa nchi naye ujinga umemshinda nguvu na sasa ndiyo unaomuongoza kwenye kila analofanya na kusema..
Naona hata aibu ku argue na mtu kama wewe usiyejua maana ya mipaka ya nchi, taifa na utaifa
siku moja utasema haina maana kugombea mlima kilimanjaro tuwaachie kenya si limlima tu watalipeleka wapi hata ukiwa Moshi mjini unauona, pole sana.
 
Mwaka jana kuna chi 2 za Amerika Kusini; Nicaragua/Honduras, nusura waingie vitani baada ya mojawapo kufuata ramani ya Google na kutangaza kuwa ndio mpaka wao rasmi.

Hawa jamaa wa Google, msitari wa mpaka wamechora na rangi nyekundu kisha wanaonyesha LAke Nyasa yote imebaki Malawi, hii imekaaje? Nadhani hili la ugomvi wa mpaka halina itikadi, nakumbuka miaka ya nyuma enzi za Hayati Mwalimu nusura tuzipige na Malawi wakati wa Dr. Banda kwa ajili ya mpaka huu.

Unashangaa hilo

Mbona waKenya wanasema mlima Kilimanjaro upo kwao waziri mhusika yupo kimyaa anavimbiwa posho tu hata kulisemea anashindwa kwa vile kavimbiwa posho
 
Back
Top Bottom